M-mbabe
JF-Expert Member
- Oct 29, 2009
- 13,203
- 23,020
BBC wamekuwa wakimchafuaje rais kwa mfano?wakuu
kwa muda sasa hili shirika la utangazi kutoka uingereza BBC limekuwa likiripoti habari kwa namna ya kichochezi hapa tanzania
kwa hapa nchini BBC kupitia BBC swahili imekuwa mstari wa mbele kuuoneshea ulimwengu na watanzania yale mambo tu yenye ukakasi yanayofanywa na mh rais Magufuri hata kama hayana ukakasi huo BBC swahili hukoleza chumvi na hatimaye kuichafua serikali ya awamu ya tano
kiukweli bbc swahili ni chanzo cha uchochezi, mambo mazuri ya serikali hii hayashikiliwi na hayatangazwi sana kama hizi kauli za kawaida tu ambazo hutolewa na rais
Imefika wakati rasmi sasa, serikali iiwaadhibu na kuwadhibiti hawa Bbc kwa tabia zao za kumchafua rais. uthibiti umewezekana kwa vyombo vya habari vya ndani, kwanini BBC swahili isidhibitiwe?
Nini kinakwamisha serikali kukifungia bbc kwa uchochezi kinaoufanya?
wapi mamlaka husika? inaama hawaoni uchochezi huu kutoka bbc? au wizara ipo kwa itv startv jf, tanzania daima na media za watanzania tu
ni wakati sasa bbc kichukuliwe hatua, uchochezi wake hauvumiliki