Bashe ajipanga kugombea Igunga

Raia Fulani

JF-Expert Member
Mar 12, 2009
10,769
2,544
Kwa mujibu wa vyanzo vyangu vya taarifa, Bashe amepata ule wasaa aliokuwa akiutamani na ambao ulimponyoka bila yeye kutarajia-kuingia mjengoni. Vyanzo vinasema kuwa Rostam anahakikisha kuwa jimbo lile linarudi 'kwake' kupitia mtu wake wa karibu na ambaye kwa sasa ni ceo wa habari corporation. Mwenye masikio na akae mkao wa kula

Mod. UPDATE:
Response by the aforementioned:
Wana Jf naomba nitumie nafasi hii kusema sina NIA,UTASHI WA KISIASA,kugombea jimbo la Igunga wala Jimbo lingine lolote Tanzania zaidi ya Jimbo la Nzega mungu akinifikisha salama 2015, reason nitakua nimesaliti wana nzega,nitakua nimeenda kinyume na dhamira yangu.Kwahiyo nisema hizi tetesi si za kweli na mwisho ni mwana siasa gani ambae atafanya kosa kama HILO? Kwetu nzega nitabaki nzega nitagombea nzega nitawatumikia wana nzega.Ninawatakia Heri wote watakaoenda kugombea Igunga.Mwisho nitoe angalizo kwa wana jamvi hapa hizi lugha za kikaburu,za kubaguana kwa rangi,dini nadhani si njema sana kwa Taifa letu inawezekana aneziandika hapa jamvini haoni madhara leo basi ipo siku italitafuna Taifa letu zimeanza kujitokeza naziona hapa jamvini,nazisikia midomoni mwa wana siasa na sasa zimeanza kwenda ktk nyumba za dini,nilizoea kwetu kijijini kabila hutajwa wakati wa utani lakini sasa naona miongoni mwa wasomi na viongozi zikitajwa kwa nia ya kutugawa nadhani TUNAPOTOKA.ipo siku tutawajibishwa. Nasisitiza SIGOMBEI IGUNGA.
 
Igunga hawapendi kutawaliwa na mweusi,yaani mwalabu koko,muhindi nk ata mimi nkivaa maski ya kizungu watanipa tu.
 
Igunga hawapendi kutawaliwa na mweusi,yaani mwalabu koko,muhindi nk ata mimi nkivaa maski ya kizungu watanipa tu.

Duuuuh.....Ama kweli mmewachoka wanaochagua mafisadi, hapo penye red tafadhali muungwana waombe radhi watu wa Igunga huo si uungwana mwana wa ukaye
 
Labda na selelii nae anaweza kuibukia huko. Tutashuhudia kambi mbili za ccm za 6 na abdulrasul kwa upande mmoja na upinzani kwa upande wa pili. Tusubirie filamu kama lile la tmk enzi za cisco
 

Kweli mkuu kila baada ya paragraph Wazee wangu,Wazee wangu nikabaki najiuliza lini wazee wa Igunga walimzaa MuIran.

Halafu kama uliangalia vizuri ni kwamba wazee wachache waliwekwa pale mbele nyuma kulikuwa na vijana wengi tu wale wa kuzomea zomea, halafu ukumbi wa sakao ni kaukumbi kamekaa kama tree top ya zamani pale Manzese yaani ni kadogo na huenda walizimia kama athari za watoto wa Tabora walioenda disco waliokosa hewa na si masikitiko ya mbunge kuondoka
 
Kwa mujibu wa vyanzo vyangu vya taarifa, Bashe amepata ule wasaa aliokuwa akiutamani na ambao ulimponyoka bila yeye kutarajia-kuingia mjengoni. Vyanzo vinasema kuwa Rostam anahakikisha kuwa jimbo lile linarudi 'kwake' kupitia mtu wake wa karibu na ambaye kwa sasa ni ceo wa habari corporation. Mwenye masikio na akae mkao wa kula

Kwenye ile bifu yake na Kigwangalla alimwambia:

"Wapo wanahabari waliokuwa wananieleza juu ya mipango hii mliokuwa mnaifanya na ilifahamika mapema, but I said to my self sijajiunga CCM kwa ajili ya UBUNGE tu nitagombea nitashindwa nitakatwa lakini nitabaki ndani ya CCM kutimiza wajibu wangu, na unafahamu hili kwa 2015 u will face me again if god wish, politically u have never been threat to me jimbo la nzega ninafahamu mtu pekee ambae ninaamini ni threat kwangu ni LUCAS LUMAMBO SELELII not you."

Kama akiamua kugombea jimbo la Igunga mwaka huu, badala ya jimbo la Nzenga mwaka 2015 kama alivyomwambia Kigwangalla, then inaweza kuwa na implications kubwa za kisiasa kwake. Kama ana busara na hekima atasubiri mpaka 2015 agombee Nzega ili atimize ndoto yake ya kuwaendeleza wana Nzega. Pia atakuwa ametimiza ahadi yake kwa Kigwangalla kuwa, Kigwangalla will face him again mwaka 2015. Lakini kama ana uroho wa madaraka, kama hatatumia busara na hekima, then atagombea Igunga. Ikumbukwe pia, kwa yanaondelea ndani ya CCM, wale wahusik watakaopitisha jina, wanaweza kumtosa vile vile.
 
Nadhani sasa Dr Peter Kafumu, Commissioner wa Madini atakwenda gombea amekuwa akishindwa mara kwa mara na Rostam kwenye Nomination za CCM
 
Mie nafikiri kinyume chake.

Bashe atabakia kusubiri jimbo lake ambalo care taker ni Kigwangala.

Ukimsikiliza RA alisema pamoja na kwamba Tabora ina historia ya upinzani wao/yeye amehakikisha ktk kipindi chake chote cha uongozi Tabora inabaki CCM. Hiyo ni kusema kwa vile sasa sio kiongozi watarajie kinyume chake

Mlango wa fahamu wa sita unanituma kuamini kwamba RA atawaacha CCM waangukie pua kwenye uchaguzi mdogo ili wabaya wake wajue "vikielea manake vimeundwa".

Tusubiri sinema itakwendaje!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom