Kijana Hussen Mohamed Bashe! maarufu hapa kwetu Nzega" KAYANDA"! anazidi kuwaonyesha wakazi wa Nzega na Taifa kwa ujumla kuwa pamoja na maswaibu yote yanayomkuta katika medani za kisiasa bado ni kipenzi cha wana NZega baada ya jana kushinda nafasi nyeti pasipo yeye kuwepo, Bashe ambaye ni mjumbe wa halmashauri kuu ya ccm wilaya ya Nzega kwa mujibu wa katiba ya ccm anaruhusiwa kugombea ujumbe wa kamati ya siasa ya wilaya ambacho ni kikao kikubwa na chenye maamuzi ya mwisho kwa ccm kwenye ngazi zote za wilaya.
Katika kikao hicho cha halmashauri ya ccm ya wilaya ambacho pia Mbunge wa jimbo Ndg (Mh) Kigwangalla ambae ni hasimu mkubwa wa Hussen Bashe katika siasa za NZega hasa baada ya Bwana Bashe kupata zaidi ya kura 14,000 katika kura za maoni za ccm huku zikimuacha bwana Kigwangalla akiambulia kura zisizo zidi 1,500(elfumoja miatano tu) na baadae chama cha mapinduzi kumteua Mbunge aliyepo hali ilizaa masononeko kwa wakazi wengi wa Nzega bila kujali vyama vyao. jana Kwa mara nyingine Bwana Bashe alishinda kwa kura nyingi kuwa mjumbe wa kamati ya siasa ya wilaya bila kuwepo Nzega wala ukumbini.
Aidha Mbunge kigwangala alitumia nafasi yake kuwapigia debe baadhi ya wajumbe wanaoaminika ni wafuasi wake waanifu washinde nafasi hiyo lakini wote hawakushinda moja ya sms toka kwa kigwangala kwenda kwa wajumbe ilisomeka hivi" kwa heshima na taadhima naomba unisaidie kutafuta kura za wafuatao Mh Pele(hakushinda) Mh Mama Dotto(hakushinda) Mh Bazilio(hakushinda) Mh Sofia(hakushinda) katika uchaguzi huo walioshinda wote ni wana ccm wakaida wasio penda makundi ndani ya chama lakini pia wasiomuunga mkono Dr Kigwangala kwa kuendekeza makundi
Katika kikao hicho cha halmashauri ya ccm ya wilaya ambacho pia Mbunge wa jimbo Ndg (Mh) Kigwangalla ambae ni hasimu mkubwa wa Hussen Bashe katika siasa za NZega hasa baada ya Bwana Bashe kupata zaidi ya kura 14,000 katika kura za maoni za ccm huku zikimuacha bwana Kigwangalla akiambulia kura zisizo zidi 1,500(elfumoja miatano tu) na baadae chama cha mapinduzi kumteua Mbunge aliyepo hali ilizaa masononeko kwa wakazi wengi wa Nzega bila kujali vyama vyao. jana Kwa mara nyingine Bwana Bashe alishinda kwa kura nyingi kuwa mjumbe wa kamati ya siasa ya wilaya bila kuwepo Nzega wala ukumbini.
Aidha Mbunge kigwangala alitumia nafasi yake kuwapigia debe baadhi ya wajumbe wanaoaminika ni wafuasi wake waanifu washinde nafasi hiyo lakini wote hawakushinda moja ya sms toka kwa kigwangala kwenda kwa wajumbe ilisomeka hivi" kwa heshima na taadhima naomba unisaidie kutafuta kura za wafuatao Mh Pele(hakushinda) Mh Mama Dotto(hakushinda) Mh Bazilio(hakushinda) Mh Sofia(hakushinda) katika uchaguzi huo walioshinda wote ni wana ccm wakaida wasio penda makundi ndani ya chama lakini pia wasiomuunga mkono Dr Kigwangala kwa kuendekeza makundi