Barua: Zitto akataa posho za vikao

Barua: Zitto akataa posho za vikao

inasaidia nini alivyokataa kuchukua posho za ubunge kwa upande mmoja, na upande wa pili anachukua mabilioni ya rushwa za tss ili kuuza chama chake? kunyamazia buzwagi?

Ni mnafiki tu!

Mbowe na Zito nani mnafiki?Mbowe alirudisha gari lakin akalichukua tena na leo anatembelea,acha propaganda
 
Butola, huwezi kusema eti Mbowe ameshindwa kuachia posho ya shilingi 70,000 kwa siku ambayo kwa siku 50 za ubunge ni sawa na shilingi milioni tatu na nusu 3,500,000 kwa kipindi chote cha bunge la bajeti halafu ujenge hoja hapa.

Hii ni kutokana na ukweli kuwa Mbowe alionyesha kwa vitendo kwa kuachia Shangingi V8 Jipya , mafuta ya shangingi hilo,dereva na ukiangalia kimahesabu unaweza kuona kuwa hata mafuta aliyoweka KWENYE gari lake kwa safari zake wakati akiwa Dodoma kama zile za kwenda Arusha , Igunga, DSM kwenye vikao mbalimbali vya chama ni zaidi ya hizo milioni tatu na nusu , penye ukweli tuuseme na penye sppining tuseme wazi kwanio hata habari ilivyotolewa kwenye gazeti linaloheshimika ni kuwa kwa mara ya kwanza linasema bila kuonyesha kuwa nani kasema ila wanasema tuu ni Bunge ... huu ni mkakati wa ...........

Pamoja na kumpa pongezi Zitto , ila Mbowe anapaswa kupewa pongezi pia kwani alipinga mashsngingi na kuamua kuliacha bila masharti na nafikiri kuna haja kuliangalia hili pande zote.

Hivi aliacha kweli au ilikuwa ni mbwembwe za kisiasa?
 
Zitto ana akili sana, nani mzalendo wa kweli.

Kumbe wewe huna akili basi ni shida.kuna mtanzania ambaye hana akili.kama zzk angekuwa na akili sana basi angepata distinction au first class wakati anamaliza chuo kikuu.kumbe kwa tanzania ukiwa mpiga tarumbeta basi unaakili.kazi kweli kweliii
 
Zitto aache janja yake! Anatupiga tu wananchi changa la macho. Hii Kigoma Development Initiative(KDI) ni NGO yake mwenyewe! So hizo allowance zinamrudia yeye mwenyewe!

Hapo ulikuwa na maono. Rejea ukurasa wa pili wa form ya mali na madeni ya Zitto iliyotolewa na ACT siku kadhaa zimepita. Mh Zitto anamiliki 50% ya hisa za KDI.

Ni wazi sasa kuwa kukataa posho ilikuwa ni political kick lakini uhalisia ni kwamba mastahili ya Zitto yaliendelea kuwa yake kwa sababu yalikuwa yakijenga hiyo 50% ya KDI.

Wengi tuna tatizo la kusahau na hili limetumiwa na wanasiasa kututia upofu.
 
ZITO bahari nyingi,hata NASARI alimtabiria makubwa makubwa mbeleni.
 
Akiwa mwenyekiti wa PAC hakuhitaji posho maana alikua na njia ya kupata fedha zaidi kwa cheo chake.
 
Issue ya Mbowe Mwigulu alishaimaliza bungeni ya kua Mbowe alikataa shangingi kwa kua lilikua kuu kuu na baada ya kununuliwa jipya akalikubali na analitumia. Kwa hiyo tusimpe Mbowe sifa ambayo hana
 
Mbowe na Zito nani mnafiki?Mbowe alirudisha gari lakin akalichukua tena na leo anatembelea,acha propaganda


Nani aliyefukuzwa kwenye chama chake kwa ajili ya unafiki kati ya Zitto na Mbowe?

BTW, hakuna mwanachama yyte wa upinzani (hasa viongozi) ambaye hajakumbana na misukosuko ya kukamatwa au kusingiziwa kesi na Polisi isipokuwa Zitto, hii ni koisidensi tu au "ajenti wetu tutamkamataje?"

Ukionana naye tusaidie watanzania kumwuuliza, yale majina ya vigogo wenye fedha walizoficha nje (aliyosema anayo) yako wapi?
----

Sio Propaganda mkuu, ila ipo wazi sana kuwa inabidi mbadilisheni CODE ili mfikie lengo maana cover limeshafunguka, kuendelea kumng'ang'ania ni kubeba mzigo mwingine, na mda uliobaki ni mdogo sana, ama arudishe fedha, maana kazi kashindwa, wapinzani hawamwamini tena na halikadhalika wananchi!
 
Hizo zilikuwanibwebwe juu ya usanii kumbe kaelekeza zitangulie kwenye taasisi yake ya KDI amakweli nchi yangu nilijua hazitaki kabisa kumbe.... atakutana nazo mbele kama katoa pasi kaiwahi kwambele >>>>>>>>>>:bump2:
 
Wadau,
Nimejaribu kujiuliza hili
Hivi ingekuwaje kila mmbunge wa bunge la Jamhuri ya muungano wa Tanzania angefanya maamuzi kama ya Ndugu ZZK ya kutochukua hata senti moja ya Posho bungeni then iundwe kamati ya bunge ya kusimamia miradi ya kimaendeleo itakayotekelezwa kwa kutumia fedha za ujumla za Posho ambazo ilikuwa wapewe hawa wabunge
Nimewaza kwa jicho la 3 tu sijiu mnasemaje?
 
Sijapata kuona Katibu anayeweka mafaili au kuvujisha/kugawa nakala original za barua zake mitandaoni kama huyu Mukovwa

Kwa kuzingatia historia na tabia kama UKAWA wangekuwa na hiki kirusi hakika hata leo Gazeti la Mtanzania lingeweza kutoa nakala original za yote yaliyokwisha zungumzwa kwenye vikao vya siri vya viongozi waandamizi wa UKAWA. Mfano halisi mwaka 2010, baada ya Spika Sitta kuipiga chenga CHADEMA, ni waandamizi wachache sana ndani ya CHADEMA walijua mapema kwa hakika kwamba Dr. Slaa ndiye atakayekuwa mgombea wa Urais. Mukovwa wangu hakuwa na hakika mpaka ilipotangazwa na kukubaliwa kwenye Kamati Kuu. Lakini the moment amejua, instantly aka-tweet hata hakusubiri kikao kiishe wala taarifa itolewe rasmi kwa utaratibu wa chama. Huu ndiyo umekuwa utaratibu wake wa kufanya kazi hata ndani ya PAC. Ukipewa kazi ya kuwa Afisa Habari wa Mkovwa wangu we hesabu huna kazi. Maana yeye anajua kupasha habari hata kabla hazifanywa kuwa habari rasmi. Mtu kama huyu UKAWA wakimkaribisha, wawe na hakika kuwa maneno “SIRI, MBINU, MIKAKATI” yatakuwa misamiati adimu.


5508318.jpg

attachment.php

image.jpg

BARUA+YA+MNYIKA+KWA+ZITTO+1.jpg

barua-ya-polisi-kwa-zitto.jpg


 
Ungeweka na juzi alitangaza mali feki bila kuweka nyumba iliyoko Mbezi anakoishi mzazi Mwenzie .
 
Wacha leo nitapike ya moyoni yaliyoniganda miaka ya hivi karibuni na nizawadie adhabu ambayo sijawahi kuonja. Nyinyi watu Cookie,Mhariri,Active,Moderator ni wachenzi na wapuuzi sana. Nimevumilia miaka mingi mnanidhalilisha kwa kuunganisha kila thread ninayoanzisha. Hivi mkusanyiko niliofanya mnaona unaendana na hili thread? You are ------. Since when the the collection (universal set) became the subset? Hovyo kabisa. Ban me today..now its too much and intolerable anymore.
 
Wacha leo nitapike ya moyoni yaliyoniganda miaka ya hivi karibuni na nizawadie adhabu ambayo sijawahi kuonja. Nyinyi watu Cookie,Mhariri,Active,Moderator ni wachenzi na wapuuzi sana. Nimevumilia miaka mingi mnanidhalilisha kwa kuunganisha kila thread ninayoanzisha. Hivi mkusanyiko niliofanya mnaona unaendana na hili thread? You are ------. Since when the the collection (universal set) became the subset? Hovyo kabisa. Ban me today..now its too much and intolerable anymore.

Mkuu pole, ila c vyema kumtukana mtu usie mjua, unaweza kukuta unamtukana baba yako..

Nadhan pia hao wapo ku regulate, hzi thread nyingi, maana zinaingiliana.. kwa hyo kama hukutendewa haki zipo njia nyingi ila matusi si usitarabu...pole sana kwa kukerwa, ila shukuru pia maana ingeweza hata kufutwa..
 
Mhh! Kweli?
Lkn mie nadhan pamoja na kuwa kweli posho hizo ni kubwa, kwa cdm bado zinahitajika sana kwani chama bado hakina vyanzo vya kutosha vya mapato vya kutosha. Hivyo basi posho hizo pamoja na ruzuku kidogo inayopatikana itakisaidia chama kujiimarisha zaidi.
Sa wakizikataa wataanza tena kuwaomba kina Sobodo!

Vipi leo mapato yametosha hadi muombe posho zifutwe.!?
 
Back
Top Bottom