MWANANCHI inahitaji kutufafanulia zaidi kuhusu hili.
Tunakumbuka mjadala wa posho ulichukuliwa ni wa kitaifa. Ni mjadala ambao umeacha makovu ndani CHADEMA hasa ukimtaja Shibuda. Lakini vilevile ulitikisa hata nje ya CHADEMA, taja jina la January Makamba.
Suala hilo lilipamba magazeti kwa kuwa habari iliyojaza kurasa mbili au zaidi.
Nimeisoma habari yote a MWANANCHI leo.
Kwanza kuna utata wa kujaza fomu na kuchukua posho. Pendekezo la CHADEMA lilikuwa ili kuepuka mtego wa kubambikiziwa kwamba mbunge amechukua posho basi zitenganishwe fomu za mahudhurio na za kupokea posho. Je, fomu za kupokea posho zimeshatenengezwa?
Kama fomu hazijatangenezwa basi ndiko kulekule kwa masuala a mahudhuriao ambayo hatuna haja ya kuyarudia maana nchi nzima iliyajadili labda kama humu JF kuna wasinziaji kama wale wabunge wachapa usingizi.
Mambo ya kusema habari za kuaminika toka mahala fulani ndiyo Nape Nnauye anapigana nayo kuhusu kukataa mwandishi aliyemuuliza kuhusu barua ya Tendwa kuitwa kwa masuala ya muafaka na CHADEMA
Hivyo, MWANANCHI itafute mbinu za kupata wasomaji kuliko kukimbilia kupachika sentensi moja kujibu mjadala wa posho uliochukua wiki kadhaa na kujaza kurasa za magazeti yote East Africa.
Na ukiangalia kwa makini utaona inasema "taarifa toka ofisi ya Bunge". Ninavyowajua MWANANCHI wameandika habari nyingi wakisisitiza neno "Barua ambayo MWANANCHI imeiona". Hapa wanasema ni taarifa. Hawasemi kama wameona signed document ambao CHADEMA wamepokea posho hizo.
Hivyo gazeti kama hili litambu kuwa umakini wa wasomaji umeongezeka na si rahisi kuwapata vipofu wa kuishia kusoma juujuu. Ni hali hii ya uandishi inayofanya gazeti moja leo lilalamike kuwa mitandao imesababisha magazeti yapungue soko.