Barua: Zitto akataa posho za vikao

Barua: Zitto akataa posho za vikao

Uhuru ni gazeti la magamba lililowahi kusifia kauli ya JK "WANAFUNZI WANAOPATA MIMBA MASHULENI WANAVIHEREHERA'
 
Source: Gazeti Kongwe la UHURU, Juni 13, 2011......

Hakuna cha ukongwe wala nini...lilibebwa sana na ile sheria ya magazeti.....sasa hivi linachechemea kwa kukosa mbeleko
 
Mwisho wa siku mtatuletea habari zilizoandikwa kwenye Magazeti ya KIU huku. Hawa ndio watu waliotumwa na CCM kuja kuidhalilisha Jamii Forum.

CCM kwishney!
 
Monday, 13 June 2011 07:59 newsroom


NA STEPHEN BALIGEYA, DODOMA

U AMUZI wa baadhi ya wabunge kutangaza kuacha kupokea posho za vikao vya Bunge umezidi kuwagawa, huku wale wa CHADEMA wakimgeuka Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe.

Wabunge wanne wa NCCR-Mageuzi nao wametangaza kuacha kupokea posho hizo, wakisema zipelekwe kwenye fungu la 74 la fedha za maendeleo, ambalo ni maalumu kwa ajili ya mkoa wa Kigoma. Wana-NCCR hao wakiongozwa na David Kafulila (Kigoma Kusini), wameshauri posho wanazolipwa wabunge na watumishi wengine wa serikali, zikatwe kodi ili kuchangia pato la taifa. Wakizungumza na Uhuru kwa masharti ya kutotajwa majina gazetini ili kuepusha mgogoro, baadhi ya wabunge wa CHADEMA wamedai hakuna makubaliano yaliyofikiwa kutaka wabunge wa chama hicho kuzikataa posho hizo. Kwa mujibu wa wabunge hao, kilichoelezwa na Mbowe, ambaye pia ni Mwenyekiti wa CHADEMA kuhusu kauli ya Zitto Kabwe, si azimio lililofikiwa na chama kwa ajili ya utekelezaji. Wabunge hao wa CHADEMA walisema wanachofahamu ni kuwa, hakuna mbunge wa chama hicho aliyeshinikizwa kutopokea posho hizo ambazo ziko kisheria. “Hapa ieleweke kuwa tumejadili suala hilo, kama unavyojua mawazo ya wengi, wapo waliokubali na waliokataa. Hakuna muafaka uliofikiwa kuwa tukatae posho, bali kama mbunge mmoja mmoja akitaka na afanye hivyo, ndiyo maana Zitto katoa uamuzi binafsi,” alisema mbunge huyo. Alisema iwapo ungekuwa uamuzi wa pamoja, kungekuwa na utaratibu wa namna fedha hizo zitakavyotumika, lakini kwa kuwa ni hiari ndiyo maana Zitto kazielekeza kwenye mfuko wake wa Kigoma Initiative Development (KDI). Mbunge mwingine wa viti maalumu wa chama hicho, alisema Mbowe amejichanganya alipokuwa akiunga mkono hoja ya Zitto kwa kudai hilo ni azimio la CHADEMA. Alisema haina mantiki kwa mbunge kukataa posho za vikao na baadae kuelekeza fedha hizo ziwekwe kwenye mfuko wa maendeleo ambao anaumiliki.

“Ungewekwa utaratibu maalumu kwamba fedha hizi tunaziweka kwenye mfuko wa maendeleo wa jimbo, na tuhakikishe zinatekeleza miradi iliyokusudiwa. Ukisema utazitumia wewe hapa unakuwa unadanganya watu, kwani usipotekeleza hakuna wa kukuwajibisha,” alisema.
Kafulila kwa upande wake akizungumza na waandishi wa habari jana alisema wameandaa barua ambazo leo wataziwasilisha kwa Spika wa Bunge Anne Makinda na Waziri wa Fedha, Mustafa Mkulo.

Alisema wanataka fedha hizo zipelekwe kwenye fungu linalohusu mkoa wa Kigoma ili kuharakisha miradi ya maendeleo. Wabunge wote wa chama hicho wanatoka mkoa huo.

“Lazima ieleweke kuwa mbunge anapata malipo ya aina tatu, moja ni mshahara wa mwisho wa mwezi, mbili ni pesa ya kujikimu kwa siku akiwa nje ya jimbo na tatu ni posho ya kikao wakati anahudhuria Bunge ambayo ni sh. 70,000 kwa siku,” alisema.

Kafulila alisema wanapinga kulipwa posho ya vikao vya Bunge kwa kuwa wanalipwa posho ya kijikimu, hivyo wanalipwa mbili zinazofanana.

“Mbunge yuko Dodoma anapewa posho ya kujikimu kwa kuwa yuko nje ya jimbo, lakini bado akihudhuria kikao analipwa, huu ni mwingiliano na matumizi mabaya ya fedha za umma, lazima posho ya kikao iondoke, maana huwezi kulipwa posho mara mbili,” alisema.

Mbunge mwingine wa chama hicho, Felix Mkosamali (Kasulu Mjini), alisema licha ya kuandaa barua, wanajipanga kuwasilisha hoja binafsi bungeni kutaka kufutwa kwa posho za vikao ili kupunguza mzigo kwa walipa kodi wa Tanzania.

“Tutawasilisha hoja binafsi na wakikataa kuipitisha, itakuwa fursa kwa wananchi kutambua watu waliowatuma wanawaza kitu gani na wataamua cha kufanya,” alisema.

Aliwashauri wabunge wengine kuitazama hoja hiyo na kuijadili kwa mtazamo tofauti ili kusaidia kupunguza matumizi yasiyo ya lazima kwa serikali.

Spika Anne alikaririwa na baadhi ya vyombo vya habari juzi akisema amepokea barua ya Zitto, lakini Bunge litaendelea kumpatia fedha hizo kupitia akaunti yake ya awali na ataamua kwa kuzipeleka.

“Ni kweli Zitto ameandika barua akitaka fedha zake zipelekwe KDI, lakini hatutafanya hivyo kwa kuwa Bunge halina mamlaka ya kuingilia matumizi ya fedha za mbunge. Sheria ndiyo inayosema, hatubadilishi,” alisema.

 
Monday, 13 June 2011 07:59 newsroom


NA STEPHEN BALIGEYA, DODOMA

Wabunge wanne wa NCCR-Mageuzi nao wametangaza kuacha kupokea posho hizo, wakisema zipelekwe kwenye fungu la 74 la fedha za maendeleo, ambalo ni maalumu kwa ajili ya mkoa wa Kigoma. Wana-NCCR hao wakiongozwa na David Kafulila (Kigoma Kusini), wameshauri posho wanazolipwa wabunge na watumishi wengine wa serikali, zikatwe kodi ili kuchangia pato la taifa. Wakizungumza na Uhuru kwa masharti ya kutotajwa majina gazetini ili kuepusha mgogoro, baadhi ya wabunge wa CHADEMA wamedai hakuna makubaliano yaliyofikiwa kutaka wabunge wa chama hicho kuzikataa posho hizo. Kwa mujibu wa wabunge hao, kilichoelezwa na Mbowe, ambaye pia ni Mwenyekiti wa CHADEMA kuhusu kauli ya Zitto Kabwe, si azimio lililofikiwa na chama kwa ajili ya utekelezaji. Wabunge hao wa CHADEMA walisema wanachofahamu ni kuwa, hakuna mbunge wa chama hicho aliyeshinikizwa kutopokea posho hizo ambazo ziko kisheria. "Hapa ieleweke kuwa tumejadili suala hilo, kama unavyojua mawazo ya wengi, wapo waliokubali na waliokataa. Hakuna muafaka uliofikiwa kuwa tukatae posho, bali kama mbunge mmoja mmoja akitaka na afanye hivyo, ndiyo maana Zitto katoa uamuzi binafsi," alisema mbunge huyo. Alisema iwapo ungekuwa uamuzi wa pamoja, kungekuwa na utaratibu wa namna fedha hizo zitakavyotumika, lakini kwa kuwa ni hiari ndiyo maana Zitto kazielekeza kwenye mfuko wake wa Kigoma Initiative Development (KDI). Mbunge mwingine wa viti maalumu wa chama hicho, alisema Mbowe amejichanganya alipokuwa akiunga mkono hoja ya Zitto kwa kudai hilo ni azimio la CHADEMA. Alisema haina mantiki kwa mbunge kukataa posho za vikao na baadae kuelekeza fedha hizo ziwekwe kwenye mfuko wa maendeleo ambao anaumiliki.

"Ungewekwa utaratibu maalumu kwamba fedha hizi tunaziweka kwenye mfuko wa maendeleo wa jimbo, na tuhakikishe zinatekeleza miradi iliyokusudiwa. Ukisema utazitumia wewe hapa unakuwa unadanganya watu, kwani usipotekeleza hakuna wa kukuwajibisha," alisema.
Kafulila kwa upande wake akizungumza na waandishi wa habari jana alisema wameandaa barua ambazo leo wataziwasilisha kwa Spika wa Bunge Anne Makinda na Waziri wa Fedha, Mustafa Mkulo.

Alisema wanataka fedha hizo zipelekwe kwenye fungu linalohusu mkoa wa Kigoma ili kuharakisha miradi ya maendeleo. Wabunge wote wa chama hicho wanatoka mkoa huo.

"Lazima ieleweke kuwa mbunge anapata malipo ya aina tatu, moja ni mshahara wa mwisho wa mwezi, mbili ni pesa ya kujikimu kwa siku akiwa nje ya jimbo na tatu ni posho ya kikao wakati anahudhuria Bunge ambayo ni sh. 70,000 kwa siku," alisema.

Kafulila alisema wanapinga kulipwa posho ya vikao vya Bunge kwa kuwa wanalipwa posho ya kijikimu, hivyo wanalipwa mbili zinazofanana.

"Mbunge yuko Dodoma anapewa posho ya kujikimu kwa kuwa yuko nje ya jimbo, lakini bado akihudhuria kikao analipwa, huu ni mwingiliano na matumizi mabaya ya fedha za umma, lazima posho ya kikao iondoke, maana huwezi kulipwa posho mara mbili," alisema.

Mbunge mwingine wa chama hicho, Felix Mkosamali (Kasulu Mjini), alisema licha ya kuandaa barua, wanajipanga kuwasilisha hoja binafsi bungeni kutaka kufutwa kwa posho za vikao ili kupunguza mzigo kwa walipa kodi wa Tanzania.

"Tutawasilisha hoja binafsi na wakikataa kuipitisha, itakuwa fursa kwa wananchi kutambua watu waliowatuma wanawaza kitu gani na wataamua cha kufanya," alisema.

Aliwashauri wabunge wengine kuitazama hoja hiyo na kuijadili kwa mtazamo tofauti ili kusaidia kupunguza matumizi yasiyo ya lazima kwa serikali.

Spika Anne alikaririwa na baadhi ya vyombo vya habari juzi akisema amepokea barua ya Zitto, lakini Bunge litaendelea kumpatia fedha hizo kupitia akaunti yake ya awali na ataamua kwa kuzipeleka.

"Ni kweli Zitto ameandika barua akitaka fedha zake zipelekwe KDI, lakini hatutafanya hivyo kwa kuwa Bunge halina mamlaka ya kuingilia matumizi ya fedha za mbunge. Sheria ndiyo inayosema, hatubadilishi," alisema.


nikisoma hapo kwenye red tu nimeshamaliza kila kitu. asante mkuu kwa taarifa.
 
tanzania,tanzania anakupenda mama clinton..............,rasilimali zako zatukuka,mabepari wanatafutana........endeleeeni kuimba mi nshachoka!!!
 
Nimefurahi sasa Zito kuamua kutokuchukua kabisa posho maana kupeleka KDI haikuwa sahihi bado wangesema amechukua na kupeleka Kigoma. Sasa mnaweza kuona wabinafsi;;;;CCM wote, Mrema na TLP yake na CUF wote. NCCR nao wamebadilika wanaunga mkono mambo ya maana. Nawaomba pia watumishi wa serikali wakatae hizo posho maana wakipewa mshahara wao sitahili kama ulivyoombwa na TUCTA basi hawahitaji tena hizo posho zisizokuwa na uhalali
 
Ndugu zangu, poleni sana na shughuli zenu mnazoendelea nazo ili kujipatoa kipato kidogo mnachopata ili mwenze kujikimu na pia mlipe kodi. Tujitahidi sana kuwa wabunifu na kufanya kazi tuweze kulipa kodi ili wabunge wetu waweze kulipwa posho zao maana wamegoma kabisa kuacha kupokea posho. Mheshimiwa Zitto na chama chake wanapendekeza wabunge wasilipwe posho lakini wenzao wa upande wa pili wanagoma; hawataki tena kwa nguvu zote.

Mimi mwenzenu, sijui ninyi wenzangu, nasikitika sana sana kuona wabunge wetu tuliowachagua wapo mstari wa mbele kuhakikisha wananchi wanaendelea kuishi katika maisha magumu hivi.

Jamani, tumeambiwa kuwa kama posho za wabunge zitasitishwa, basi nchi yetu ingeweza kubaki karibu na shilingi bilioni mia tisa! Sijui kama tarakimu hizo ndo zenyewe kabisa!! Lakini ninachojua ni kuwa fedha inayolipwa kwa mbunge mmoja kwa mwezi wewe mtu wa kawaida huwezi kupata hata ungevuja jasho vipi!

Ndungu zangu mnaopenda maendeleo na nchi yetu, nchi yetu hii ni nchi iliyojaliwa kwa raslimali nyingi ambazo sasa zinavunwa na hao watu tulioletewa na wao wanawaita wawekezaji. Tunaona wenzetu wengi wanaoishi karibu na sehemu ambazo hao wanaoitwa wawekezaji wanachuma mali bila jasho, wanauawa na kuambiwa ni majambazi.

Watu hawa tuliowaamini na kuwapa dhamana ya kuiongoza nchi yetu hawatoi majibu ya kujitosheleza fedha zile za EPA zipo wapi maana tuliambiwa wale wabinafsi waliozichukua waliambiwa tu warudishe. Kuna siku moja nilimwona mtu ameiba kuku na kupewa hukumu ya muda fulani ndani ya gereza. Sasa hawa walioiba mihela mingi wakaambiwa eti warudishe tu halafu basi.

Deni la nchi yetu halipungui bali linapaa kwenda juu tu. Maendeleo ya nchi yetu hayaendi kabisa. Eti tunakopa tulipane posho; haya tutafika tu.

Hivi kweli tuseme sisi Watanzania kufikiri kwetu kunaishia hapo; kila siku kutamka eti nchi yetu maskini? Hapana, tuchukue hatua ya makusudi.

Moja kati ya hatua ya mwanzo ni kuhakikisha kuwa wabunge na wafanyakazi wote hawapewi posho yoyote muda wanapofanya kazi kwani hiyo ni sehemu ya majukumu yao na ujira wao ni mshahara wanaopewa mwisho wa mwezi.

Hebu oneni jamani; wanafunzi wa vyuo vikuu wanapata shilingi elfu tano kwa siku wakati mbunge anapata shilingi laki moja na nusu kwa siku. Kwa mtu wa akili ya kawaida kabisa ajiulize, tofauti hii ni kwa ajili ya nini? Inaonekana hii ni sababu kwa nini wagombea ubunge hutumia kila mbinu wahakikishe wanapita maana wanajua wakifika huko bungeni wanalipwa mishahara mikubwa sana.

Mimi binafsi nikiangalia mshahara ninaopata kwa kazi ngumu hii ninayofanya naishia kuhuzunika na kuona mimi si kitu mbele ya hawa waheshimiwa. Tena wengine hata kule bungeni wamekaa tu wala hawana la kufanya. Wanateuliwa, eti mmempa mtu uwezo wa kuteua watu ili wawawakilishe bungeni! Kwani nikipewa uwezo huo kwa nini nisiteue wale ninaowafahamu na ambao ni rafiki zangu? Mbona nyie mmesema niwateulie!!!

Mmepewa kofia, vilemba na vitenge ili muwatuchague! Mmewachagua! Kwani mlifikiri hizo fedha walizotumia wakati wa uchaguzi warudisheje? Lazima warudishe kwa kupeana posho.

Lakini nani alaumiwe kwa maisha haya ya taabu? Hapa kwa mawazo ya kawaida watu watasema ni hao viongozi!! Hapana, mimi na wewe. Nasema hivi kwa kuwa sisi ndo tulichagua hawa viongozi wetu!!

Haya jamani msisahau kulipa kodi maana wabunge wetu watakosa kodi!!!
 
Monday, 13 June 2011 07:59 newsroom


NA STEPHEN BALIGEYA, DODOMA

U AMUZI wa baadhi ya wabunge kutangaza kuacha kupokea posho za vikao vya Bunge umezidi kuwagawa, huku wale wa CHADEMA wakimgeuka Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe.

Wabunge wanne wa NCCR-Mageuzi nao wametangaza kuacha kupokea posho hizo, wakisema zipelekwe kwenye fungu la 74 la fedha za maendeleo, ambalo ni maalumu kwa ajili ya mkoa wa Kigoma. Wana-NCCR hao wakiongozwa na David Kafulila (Kigoma Kusini), wameshauri posho wanazolipwa wabunge na watumishi wengine wa serikali, zikatwe kodi ili kuchangia pato la taifa. Wakizungumza na Uhuru kwa masharti ya kutotajwa majina gazetini ili kuepusha mgogoro, baadhi ya wabunge wa CHADEMA wamedai hakuna makubaliano yaliyofikiwa kutaka wabunge wa chama hicho kuzikataa posho hizo. Kwa mujibu wa wabunge hao, kilichoelezwa na Mbowe, ambaye pia ni Mwenyekiti wa CHADEMA kuhusu kauli ya Zitto Kabwe, si azimio lililofikiwa na chama kwa ajili ya utekelezaji. Wabunge hao wa CHADEMA walisema wanachofahamu ni kuwa, hakuna mbunge wa chama hicho aliyeshinikizwa kutopokea posho hizo ambazo ziko kisheria. "Hapa ieleweke kuwa tumejadili suala hilo, kama unavyojua mawazo ya wengi, wapo waliokubali na waliokataa. Hakuna muafaka uliofikiwa kuwa tukatae posho, bali kama mbunge mmoja mmoja akitaka na afanye hivyo, ndiyo maana Zitto katoa uamuzi binafsi," alisema mbunge huyo. Alisema iwapo ungekuwa uamuzi wa pamoja, kungekuwa na utaratibu wa namna fedha hizo zitakavyotumika, lakini kwa kuwa ni hiari ndiyo maana Zitto kazielekeza kwenye mfuko wake wa Kigoma Initiative Development (KDI). Mbunge mwingine wa viti maalumu wa chama hicho, alisema Mbowe amejichanganya alipokuwa akiunga mkono hoja ya Zitto kwa kudai hilo ni azimio la CHADEMA. Alisema haina mantiki kwa mbunge kukataa posho za vikao na baadae kuelekeza fedha hizo ziwekwe kwenye mfuko wa maendeleo ambao anaumiliki.

"Ungewekwa utaratibu maalumu kwamba fedha hizi tunaziweka kwenye mfuko wa maendeleo wa jimbo, na tuhakikishe zinatekeleza miradi iliyokusudiwa. Ukisema utazitumia wewe hapa unakuwa unadanganya watu, kwani usipotekeleza hakuna wa kukuwajibisha," alisema.
Kafulila kwa upande wake akizungumza na waandishi wa habari jana alisema wameandaa barua ambazo leo wataziwasilisha kwa Spika wa Bunge Anne Makinda na Waziri wa Fedha, Mustafa Mkulo.

Alisema wanataka fedha hizo zipelekwe kwenye fungu linalohusu mkoa wa Kigoma ili kuharakisha miradi ya maendeleo. Wabunge wote wa chama hicho wanatoka mkoa huo.

"Lazima ieleweke kuwa mbunge anapata malipo ya aina tatu, moja ni mshahara wa mwisho wa mwezi, mbili ni pesa ya kujikimu kwa siku akiwa nje ya jimbo na tatu ni posho ya kikao wakati anahudhuria Bunge ambayo ni sh. 70,000 kwa siku," alisema.

Kafulila alisema wanapinga kulipwa posho ya vikao vya Bunge kwa kuwa wanalipwa posho ya kijikimu, hivyo wanalipwa mbili zinazofanana.

"Mbunge yuko Dodoma anapewa posho ya kujikimu kwa kuwa yuko nje ya jimbo, lakini bado akihudhuria kikao analipwa, huu ni mwingiliano na matumizi mabaya ya fedha za umma, lazima posho ya kikao iondoke, maana huwezi kulipwa posho mara mbili," alisema.

Mbunge mwingine wa chama hicho, Felix Mkosamali (Kasulu Mjini), alisema licha ya kuandaa barua, wanajipanga kuwasilisha hoja binafsi bungeni kutaka kufutwa kwa posho za vikao ili kupunguza mzigo kwa walipa kodi wa Tanzania.

"Tutawasilisha hoja binafsi na wakikataa kuipitisha, itakuwa fursa kwa wananchi kutambua watu waliowatuma wanawaza kitu gani na wataamua cha kufanya," alisema.

Aliwashauri wabunge wengine kuitazama hoja hiyo na kuijadili kwa mtazamo tofauti ili kusaidia kupunguza matumizi yasiyo ya lazima kwa serikali.

Spika Anne alikaririwa na baadhi ya vyombo vya habari juzi akisema amepokea barua ya Zitto, lakini Bunge litaendelea kumpatia fedha hizo kupitia akaunti yake ya awali na ataamua kwa kuzipeleka.

"Ni kweli Zitto ameandika barua akitaka fedha zake zipelekwe KDI, lakini hatutafanya hivyo kwa kuwa Bunge halina mamlaka ya kuingilia matumizi ya fedha za mbunge. Sheria ndiyo inayosema, hatubadilishi," alisema.


Hapo kwenye red: Wabunge wameanza kucheza vizuri ngoma lakini kwa mdundo tofauti. Kama ni kweli kwamba wanalipwa posho mbili ni vizuri wakapokea posho moja tu kati ya hizo zinazotolewa kwa kitu hicho.

Wakiendelea kuagiza ziende kwenye majimbo yao ni vizuri lakini si sawa kwababu maeneo ambayo mbunge wake hatapenda posho yake moja iende kwenye mfuko wa jimbo watakuwa wameonewa. Jambo la maana ni kupeleka hoja ya kuondoa posho moja na iwe hivyo kwa watumishi wengine wa serikali. Huko nyuma tunakumbuka TAKUKURU waliwahi kuwahoji wabunge kuhusu suala la posho mbili pale wanapolipwa na ofisi ya bunge na Taasisi zingine za serikali wanatembelea miradi kwa siku moja.

Zitto na Wabunge wa NCCR - Mageuzi mna lengo zuri lakini msituingize mkenge kwa sababu fedha za serikali zina utaratibu wake ambao uantaka zitumike kadiri ya malengo yaliyokusudiwa. Haiwezekani mtu aanze kusema fedha zangu ziende kwenye akaunti ya shemeji yangu. Kama mnawaonea huruma wananchi, kwanini msiiagize serikali ikafanya vitu ambavyo vina mantiki?
 
Pamoja na kuwa gazeti la uhuru wanaonekana kufanya uchochezi, Posho za vikao sasa ni mzigo kwenye taasisi nyingi. Imefikia mahali sasa Agenda za vikao zimeanza kugawanywa na kuwa vikao tofauti. Baadhi ya taasisi watu wanahudhuria vikao viwili hata vitatu kwa siku.

Hivi mbunge wa Dodoma mjini naye huwa analipwa hela ya kujikimu wakati wa Bunge?
 
uhuru miaka hamsini?sasa hivi libadilishe jina walau liitwe chukua chako mapema.
au magamba.
 
UAMUZI wa baadhi ya wabunge kutangaza kuacha kupokea posho za vikao vya Bunge umezidi kuwagawa, huku wale wa CHADEMA wakimgeuka Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe.Wabunge wanne wa NCCR-Mageuzi nao wametangaza kuacha kupokea posho hizo, wakisema zipelekwe kwenye fungu la 74 la fedha za maendeleo, ambalo ni maalumu kwa ajili ya mkoa wa Kigoma. Wana-NCCR hao wakiongozwa na David Kafulila (Kigoma Kusini), wameshauri posho wanazolipwa wabunge na watumishi wengine wa serikali, zikatwe kodi ili kuchangia pato la taifa. Wakizungumza na Uhuru kwa masharti ya kutotajwa majina gazetini ili kuepusha mgogoro, baadhi ya wabunge wa CHADEMA wamedai hakuna makubaliano yaliyofikiwa kutaka wabunge wa chama hicho kuzikataa posho hizo. Kwa mujibu wa wabunge hao, kilichoelezwa na Mbowe, ambaye pia ni Mwenyekiti wa CHADEMA kuhusu kauli ya Zitto Kabwe, si azimio lililofikiwa na chama kwa ajili ya utekelezaji. Wabunge hao wa CHADEMA walisema wanachofahamu ni kuwa, hakuna mbunge wa chama hicho aliyeshinikizwa kutopokea posho hizo ambazo ziko kisheria. “Hapa ieleweke kuwa tumejadili suala hilo, kama unavyojua mawazo ya wengi, wapo waliokubali na waliokataa. Hakuna muafaka uliofikiwa kuwa tukatae posho, bali kama mbunge mmoja mmoja akitaka na afanye hivyo, ndiyo maana Zitto katoa uamuzi binafsi,” alisema mbunge huyo. Alisema iwapo ungekuwa uamuzi wa pamoja, kungekuwa na utaratibu wa namna fedha hizo zitakavyotumika, lakini kwa kuwa ni hiari ndiyo maana Zitto kazielekeza kwenye mfuko wake wa Kigoma Initiative Development (KDI). Mbunge mwingine wa viti maalumu wa chama hicho, alisema Mbowe amejichanganya alipokuwa akiunga mkono hoja ya Zitto kwa kudai hilo ni azimio la CHADEMA. Alisema haina mantiki kwa mbunge kukataa posho za vikao na baadae kuelekeza fedha hizo ziwekwe kwenye mfuko wa maendeleo ambao anaumiliki.“Ungewekwa utaratibu maalumu kwamba fedha hizi tunaziweka kwenye mfuko wa maendeleo wa jimbo, na tuhakikishe zinatekeleza miradi iliyokusudiwa. Ukisema utazitumia wewe hapa unakuwa unadanganya watu, kwani usipotekeleza hakuna wa kukuwajibisha,” alisema.Kafulila kwa upande wake akizungumza na waandishi wa habari jana alisema wameandaa barua ambazo leo wataziwasilisha kwa Spika wa Bunge Anne Makinda na Waziri wa Fedha, Mustafa Mkulo.Alisema wanataka fedha hizo zipelekwe kwenye fungu linalohusu mkoa wa Kigoma ili kuharakisha miradi ya maendeleo. Wabunge wote wa chama hicho wanatoka mkoa huo.“Lazima ieleweke kuwa mbunge anapata malipo ya aina tatu, moja ni mshahara wa mwisho wa mwezi, mbili ni pesa ya kujikimu kwa siku akiwa nje ya jimbo na tatu ni posho ya kikao wakati anahudhuria Bunge ambayo ni sh. 70,000 kwa sikualisema.Kafulila alisema wanapinga kulipwa posho ya vikao vya Bunge kwa kuwa wanalipwa posho ya kijikimu, hivyo wanalipwa mbili zinazofanana.“Mbunge yuko Dodoma anapewa posho ya kujikimu kwa kuwa yuko nje ya jimbo, lakini bado akihudhuria kikao analipwa, huu ni mwingiliano na matumizi mabaya ya fedha za umma, lazima posho ya kikao iondoke, maana huwezi kulipwa posho mara mbili,” alisema.Mbunge mwingine wa chama hicho, Felix Mkosamali (Kasulu Mjini), alisema licha ya kuandaa barua, wanajipanga kuwasilisha hoja binafsi bungeni kutaka kufutwa kwa posho za vikao ili kupunguza mzigo kwa walipa kodi wa Tanzania.“Tutawasilisha hoja binafsi na wakikataa kuipitisha, itakuwa fursa kwa wananchi kutambua watu waliowatuma wanawaza kitu gani na wataamua cha kufanya,” alisema.Aliwashauri wabunge wengine kuitazama hoja hiyo na kuijadili kwa mtazamo tofauti ili kusaidia kupunguza matumizi yasiyo ya lazima kwa serikali.Spika Anne alikaririwa na baadhi ya vyombo vya habari juzi akisema amepokea barua ya Zitto, lakini Bunge litaendelea kumpatia fedha hizo kupitia akaunti yake ya awali na ataamua kwa kuzipeleka.“Ni kweli Zitto ameandika barua akitaka fedha zake zipelekwe KDI, lakini hatutafanya hivyo kwa kuwa Bunge halina mamlaka ya kuingilia matumizi ya fedha za mbunge. Sheria ndiyo inayosema, hatubadilishi,” alisema.Source: Gazeti Kongwe la UHURU, Juni 13, 2011CDM Kazi ipo!!!
Mkuu uchonganishi utaacha lini? CCM KAZI IPO!
 
Mbona wameandika habari za wabunge wa upinzani tu,wabubge waroho wa magamba hawapo,nilitegemea gazeti hili lingetoa maelezo ya kuwaridhisha watanzania kwa nini wabunge wao wanataka waendelee kuchota posho wakati wanafunzi wanakaa chini,elimu ya juu mkopo hautoshi,walimu na madaktari hawatoshi,madawa hospital hayatoshi,mtanzania wa kawaida mlo mmoja shida,njaa kali inakuja,mafuta ushuru ni siasa haujapungua n.k. ,Ama kweli tz kazi tunayo,too much ubinafsi
 
Hivi gazeti la UHURU bado lipo? linauzwa shilingi ngapi siku hizi?
 
Ningemuomba Mhe waziri wa fedha kukata paye kwenye hizi sitting allowance. Mfanyakazi/mbunge amepata income na hiyo lazima ikatwe kodi. Kuna wafanyakazi wengine huweza kupata sitting allowance mara mbili kwa siku moja. Donors wanalalamika kuwa wafanyakazi priority yao ni posho.
 
Sidhani kama walishauriana na mwenyekiti wao wa NCCR-Mageuzi
 
nikisoma hapo kwenye red tu nimeshamaliza kila kitu. asante mkuu kwa taarifa.

Haya CHINI NI HABARI TOKA MAJIRA

[h=3]POSHO ZA VIKAO: NCCR yaunga mkono CHADEMA [/h]

*Wabunge wake waandika barua nao wakatwe

Na Pendo Mtibuche, Dodoma

CHAMA cha NCCR-Mageuzi kimesema kuwa tayari kimeandaa barua ambazo kitaziwasilisha kwa Waziri wa Fedha, Bw. Mustafa Mkulo kuelekeza posho za
vikao kwa wabunge wanne wa chama hicho zipelekwe kwenye miradi ya maendeleo kwa Mkoa wa Kogoma.

Mkuu wa Idara ya Habari na Uenezi wa chama hicho, Bw. David Kafulila alisema hayo jana kuhusu Bajeti ya mwaka 2011, 2012 na kubainisha mambo mbalimbali juu ya ukuaji wa uchumi, deni la taifa, misaada na mikopo na suala zima la vipaumbele katika uchumi wa nchi.

Msimamo huo wa NCCR-Mageuzi unaunga mkono hoja ya Kambi Rasmi ya Upinzani bungeni inayoongozwa na CHADEMA ambayo tayari imeweka msimamo huo, huku Waziri Kivuli wa Fedha, Bw. Zitto Kabwe akienda mbali zaidi kwa kuwasilisha barua ofisi ya bunge kutaka posho zake za vikao zipelekwe kwenye taasisi ya Kigoma Development Initiative (KDI).

Bw. Kafulila alisema kuwa mbali na kupendekeza posho zao kuelekeza kwenye miradi ya maendeleo, pia wanapendekeza posho zote zikatwe kodi ili kuongeza mapato ya ndani kwa ajili ya miradi ya maendeleo.

Mbunge huyo alisema kuwa barua hiy leo itapelekwa kwa Waziri wa Fedha na nakala yake kwa Sipka wa Bunge, wakiwataka fedha zao za vikao vya bunge zipelekwe kwenye kifungu74 ambalo ni fungu la miradi ya maendeleo kwa Mkoa wa Kigoma.

"Uamuzi huu pia tumeamua kuufanya kwa kuwa moja ya sehemu kubwa ya mapato hutumika kushibisha mfumo mkubwa na udhaifu wa kiutawala pamoja na ufisadi, hata ukiangalia katika serikali kuna vyeo vingi kwa mfano hiki cha ukuu wa wilaya kina kazi gani, watu wanakula fedha na kazi hawafanyi huu ni mlundikano wa madaraka kwa watu ambao hawana hata kazi," alisema.

Alisema kuwa wao kama chama cha upinzani wataendelea kusisitiza mabadiliko ya mfumo wa utawala katika eneo moja tu la kuondoa wakuu wa wilaya na makatibu tarafa nchini na kubaki na uongozi wa halamshauri ambao unatosha kusimamia majukumu yote ya ndani ya wilaya na kuokoa fedha ambazo zinatosha kununulia mitambo mipya yenye uwezo wa kuzalisha umeme zaidi ya megawati 200.
 
VITA ya kufutwa posho za wabunge na watumishi wengine wa umma, imechukua sura mpya, baada ya Spika wa Bunge, Anne Makinda kusema kwamba Naibu Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Zitto Kabwe anaweza kufukuzwa ubunge kwa kutosaini karatasi za mahudhurio. Akizungumza na waandishi wa habari katika Viwanja vya Bunge baada ya kuahirisha mkutano wa asubuhi, Makinda alisema Zitto anaweza kukumbwa na adhabu hiyo iwapo hatasaini karatasi za mahudhurio ambazo ndizo zinazothibitsha uwepo wa mbunge katika mikutano na vikao vyake. "Kwa mujibu wa kanuni zetu, asipohudhuria mara tatu anakabiliwa na adhabu tena ya kufukuzwa bunge, hizo ndivyo kanuni zinavyosema." Hata hivyo, Zitto amepuuza kauli hiyo ya Spika akisema kwamba kama ni kwa ajili ya kukataa posho, yuko tayari kufukuzwa bungeni. "Nitafanya hivyo tuone. Kanuni inasema mikutano mitatu mfululizo na siyo vikao vitatu mfululizo. Nitatumia uzoefu wangu wa siasa za wanafunzi kukwepa mtego wake. Lakini kama anadhani ni sawa kunifukuza ubunge kwa kukataa posho, nipo tayari," alisema Zitto. Kauli ya Makinda inafuatia msimamo wa Zitto ambaye ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), kukataa posho za vikao na kwamba kwa kuwa kinachohalalisha yeye kulipwa posho ni karatasi za mahudhurio basi hatasaini karatasi hizo. Zitto alisema juzi mjini Dodoma kuwa, tangu Juni 10 , mwaka huu alijibu barua ya Spika akikataa " kushinikizwa kuchukua posho za vikao" na kwamba hatua atakayoichukua ni kutosaini karatasi za mahudhurio katika vikao vyote. Mahudhurio hayo ndiyo hulalalisha mbunge kupewa posho hizo. "Kuanzia kikao cha juzi cha Tume ya Mipango, sikusaini na mkitaka nendeni mkaangalie ile orodha na kesho ndani ya Bunge sitasaini ili kuondoa uhalali wa kupewa posho hizo. Sasa hapo tutaona watanilazimisha kwa njia gani," alisema Zitto.Lakini jana, Makinda alisema mujibu wa sheria malipo yote lazima yapelekwe kwa mbunge mwenyewe na kwamba ofisi yake haitafanya vinginevyo kwa wabunge ambao wamekataa posho hizo. Kanuni 143 (1) ya Bunge inabainisha kuwa kuhudhuria vikao ndiyo wajibu wa kwanza wa kila mbunge na kwamba asipohudhuria mikutano mitatu ya Bunge bila ruhusa ya Spika atapoteza ubunge wake. Kwa maana hiyo, Zitto anaweza kufukuzwa Bunge ikiwa hatasaini mahudhurio ya vikao vyote vya Mkutano wa Bunge la Bajeti, vikao vya mkutano ujao ambao kwa kawaida huwa wa Oktoba na mkutano wa kwanza wa mwaka 2012. "Mbunge yeyote atakayeshindwa kuhudhuria Mikutano ya Bunge mitatu mfululizo bila ruhusa ya Spika iliyotolewa kwa maandishi, atapoteza ubunge wake kwa mujibu wa Ibara ya 71 (1) ( c) ya Katiba na Spika ataiarifu Tume ya Uchaguzi," inaeleza kanuni hiyo namba 143 (2) ambayo iko chini ya sehemu ya 10 ya Kanuni za Bunge toleo la mwaka 2007. Kadhalika, Kanuni hiyo ya 143 (3) inakwenda mbali zaidi na kusema kuwa mbunge asipohudhuria nusu ya vikao vya mkutano mmoja bila sababu ya msingi atapewa onyo. Fasili za kanuni hizo zinamtaka mbunge asiyehudhuria vikao vya Bunge au vile vya Kamati za Bunge kupata kibali cha Spika katika Ofisi za Bunge hilo zilizopo Zanzibar, Dar es Salaam na Dodoma.Hata hivyo, kanuni hizo haziweki utaratibu wa kudhibiti mahudhurio ya wabunge na jukumu hilo ni kama limeachwa kwa Spika ambaye kwa mujibu wa Kanuni ya 5(1) amepewa uwanda mpana wa kuamua mambo mengine ambayo hayakutajwa moja kwa moja na kanuni hizo. Kauli ya SerikaliKwa upande wake, Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo alisema jana kuwa wabunge wanaokataa posho ni wanafiki wanaotafuta umaarufu kwa umma."Mtu huwezi kusema kwamba eti posho hutaki halafu unasema zipelekwe Kigoma, kama suala ni kukataa posho ili kupunguza matumizi ya Serikali basi unazikataa kabisa," alisema Mkulo katika viwanja vya Bunge. Tayari Mkulo alikuwa amesema kuwa ikiwa wapinzani watabeba ajenda hiyo, atawaandalia fomu kwa wale wasiotaka posho ili wakajaze na fedha hizo zipelekwe kwa wahitaji wa misaada mbalimbali. Awali, Zitto alitaka fedha zake za posho zipelekwe katika taasisi ya Kigoma Development Inititive ( KDI) lakini Juni 10 mwaka huu, Spika Makinda alimwandikia barua kimweleza kuwa ofisi yake haiko tayari kufanya hivyo na kusisitiza kwamba fedha hizo za posho zitaendelea kuwekwa katika akaunti yake benki. Wanaharakati nao watakaposho za wabunge zifutwe WANAHARAKATI wa taasisi mbalimbali nchini wameunga mkono uamuzi wa Chadema wa kukataa posho.Wakizungumza kwa nyakati tofauti jana, wanaharakati hao kutoka Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) na ule wa Jumuiko la Wadau wa Maendeleo (Ado), wametaka posho hizo zifutwe ili fedha zipelekwe katika shughuli nyingine za maendeleoMkurugenzi Mtendaji wa Ado, Ntamilyango Buberwa alisema taasisi yake imepanga kuzunguka nchi nzima kutafuta watu milioni moja wanaounga mkono hoja hiyo ili walipeleke suala hilo kwa Rais Jakaya Kikwete. "Baada ya kuwapata watu hao, tutawataka wasaini fomu maalumu ambayo tutaipeleka wa Rais Jakaya Kikwete kuelezea kutoridhishwa kwetu na jambo hilo. Ado itafanya na kumaliza kampeni hiyo kabla ya kusomwa kwa Bajeti ya Wizara ya Fedha. ” Alisema ni vyema wabunge wenye nia njema na taifa na ambao wamelenga kweli kuwawakilisha wananchi, wakaunga mkono hoja ya kufutwa posho hizo. Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP, Usu Mallya alisema siyo haki kwa serikali kuendelea kuongeza posho kwa wabunge na maofisa wa ngazi za juu serikalini na kwamba suala hilo linapaswa kuzingatia hali halisi ya nchi na watu wake ambao alisema wengi wao ni maskini. Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Mallya alisema kumekuwa na kasumba kwa serikali kuwalipa posho kubwa maofisa wa ngazi za juu na wabunge na kuwasahau wafanya kazi wa kiwango cha chini bila kuangalia hali halisi ya maisha. “Nchi nyingine zinaongeza* kiwango cha mshahara kwa kuangalia hali ya maisha yanavyokwenda, hapa kwetu ni tofauti, ukisafiri posho kwa mfanyakazi wa juu ni kubwa kuliko ya yule wa ngazi ya chini, posho inapaswa kuwa na uwiano sawa na si kuleta tofauti baina ya mtu na mtu.” Alikosoa* kitendo cha serikali kusamahe kodi ya mapato kwenye posho wanazolipwa baadhi ya watumishi wa serikali na wafanya kazi wa taasisi zinazopata ruzuku kutoka serikalini akidai mpango huo utawanufaisha vigogo na si wale wa ngazi za chini. Habari hii imeandikwa na Neville Meena, Dodoma; Fredy Azzah na Geofrey Nyang’oro, Dar es Salaam.
 
Back
Top Bottom