Mbona mbowe hakwenda mahakamani lakini wenzake slaaa na Ndesamburo na Lema walikwenda. Kwa nini hawakufanya maamuzi ya pamoja kwenye hili . Punguzeni conspiracy theory zenu
Mambo ya posho ni kitu binafsi wakiona inafaa ila mtu ataamua naye afanyie posho zake jamabo analoona linafaa jimboni kwake au wenye chama chake
Jamani, sio nyinyi mliokuwa wa kwanza kumtaka aziache hizo posho? Kaziacha imekuwa maneno!
Hata nyinyi acheni unafiki
Sioni mantiki yoyote kwa hili. Posho ni haki yake. Jimbo kwake kuna matatizo kibao ya huduma za wananchi. Angeweza kutangaza kuwa anaelekeza posho hizo kwenye huduma za jamii jimboni kwake. Hivi kumgekuwa na ubaya gani kama angeeleza posho hizo hospitali ya jimbo lake? Asilewe sifa ingawa ana ubora.
Hiki ndicho kilikuwa kinakosekana kwa wanasiasa wetu. Maneno bila vitendo. Zitto ametupeleka hatua 100 mbele katika mustkabali wa siasa zetu-tunampongeza. Asirudi nyuma. Mwanasiasa hapaswi kufanya jambo ambalo haliamini. Hata kama wengine wataendelea kupokea waendelee, lakini usikubali kusaliti utashi wako.
Tunataka afanye marekebisho aziachie bila masharti yoyote, ndio tutampa Big Up. Haiwezekani ukakataa mali haramu, halafu ukatoa maagizo ikanunue kitoweo nyumbani. Zitto nan maslahi mapana na KDI na jimbo lake , hivyo kitendo chochote cha fedha hizo harama kupelekewa huko tena kwa maagizo yake hakiwezi kuchagia kuondoa mfumo huo mbovu wa kifisadi. At least he gets 50% credit.
Sasa hiyo NGO Kama ni yake na ipo kwa ajili ya kuwasaidia wengine pana tatizo gani hapa!!?au umeamua tu kuchafua hali ya hewa.Mimi na wewe tuwe na mawazo mazuri ili tulijenge hili taifa la Tanzania lisilokamilika kila siku matatizoZitto aache janja yake! Anatupiga tu wananchi changa la macho. Hii Kigoma Development Initiative(KDI) ni NGO yake mwenyewe! So hizo allowance zinamrudia yeye mwenyewe!
Tunataka afanye marekebisho aziachie bila masharti yoyote, ndio tutampa Big Up. Haiwezekani ukakataa mali haramu, halafu ukatoa maagizo ikanunue kitoweo nyumbani. Zitto nan maslahi mapana na KDI na jimbo lake , hivyo kitendo chochote cha fedha hizo harama kupelekewa huko tena kwa maagizo yake hakiwezi kuchagia kuondoa mfumo huo mbovu wa kifisadi. At least he gets 50% credit.
Tena unafiki wa kutaka kuoneka mzuri machoni pa watanzania,,leo kuna familia ngapi, huko jimboni mwako maskini wa kutupwa
kwa nini usingepeleka hizo posho moja kwa moja kwenye familia maskini kabisa, ili ziweze kuwasaidia kwa sababu ni pesa zao?
Narudia huo ni unafiki wa kutaka kuoneka mzuri machoni pa Watanzania.
Mkuu ina maana wabunge wengine wote wa CHADEMA ambao wataendelea kupkea posho watakuwa wanafanya jambo ambalo hawaliamini? Hii ni kwa sababu kwa mujibu wa Budget Mubadala ya CHADEMA posho zinatakiwa zifutwe na hivyo walikubaliana kwamba hiyo ndio imani yao hadi wakaiweka kwenye badget kivuli. Wakiendelea kupokea tuamini kuwa wanafanya jambo ambalo hawaliamini?
Mkuu ina maana wabunge wengine wote wa CHADEMA ambao wataendelea kupkea posho watakuwa wanafanya jambo ambalo hawaliamini? Hii ni kwa sababu kwa mujibu wa Budget Mubadala ya CHADEMA posho zinatakiwa zifutwe na hivyo walikubaliana kwamba hiyo ndio imani yao hadi wakaiweka kwenye badget kivuli. Wakiendelea kupokea tuamini kuwa wanafanya jambo ambalo hawaliamini?
Mkuu, katika lugha yetu ya kiswahili hakuna kitu kama "kwa niaba yake binafsi".
Lakini jambo la msingi nililotaka kusema, mbona huelweki?? mara useme zitto kapeleka pesa kwenye NGO yake hapo hapo unasema hujui hiyo KDI ni ya nani. Mara useme NGO za bongo ni usanii mtu, kwahiyo unataka tuamini kwamba hapa bongo hakuna NGO iliyo serious? hapa dude hebu kuwa mkweli.
Ghafla tena unaanza kuhamisha mada kutoka kwa KDI na kuielekeza kwa chadema, mbona unaruka ruka? hebu jielekeze kwenye hoja ya msingi, zitto kaamua posho yake ielekezwe kwenye shughuli za maendeleo ya wananchi wake wa kigoma, wao ni sehemu ya watanzania wanaohitaji maendeleo, kwani kila kitu anachofanya zito lazima uwe msimamo wa chama?mambo mengine ni yake yeye na wapiga kura wake.
Yaani fedha wizi ziklete maendeleo Kigoma?Kuziacha bila maelekezo ni kuwaachia wajanja wale, Ztto Mhe. anaakili sana. Ndo maana anazielekeza kwenye kazi za maendeleo KDI amabpo anaweza nkuziona wazi kazi zinazofanya.
Mi nadhani inatupasa tupongeze hatua aloipiga Zitto ni ajabu kukuta eti mtu anadhihaki kwa kua KDI ipo chini ya uongozi wa zitto. Hvi tulitarajia apeleke fedha za posho yake jimboni kwa chiligati, Nyambari,January au kwa Majaliwa na wengineo wa CCM? Kila mbunge ana watu anawawakilisha ambao anawajibika kwao. Zitto kaonyesha njia apongezwe na si kukatishwa tamaa.BINAFSI NATOA PONGEZI ZANGU STAHILI.......(ANGALIZO) KAMA ALIPOELEKEZA ZIPELEKWE KWELI IKAWA NI NGO YAKE BINAFSI (hiyo ni sarkasi katuchezea) SI SAHIHI SANA.....! BALI NINGEMWELEWA ANGEPELEKA KATIKA TAASISI AMBAZO HANA MKONO WAKE KWA NAMNA MOJA AMA NYINGINE!TUHESHIMU MCHANGO WAKE NA PIA LOLOTE AMBALO AENDA KINYUME TUWE KINYUME NALO
zitto huyu jamaa anafaa kuwa rais wetu 2015
tunataka kopy ya barua hapa na sababu zake