Tatizo lako ni saikolojia,najua kwa sasa una wakati mgumu! unajihisi mwenyewe pia unajiuliza watu wako wa karibu watakuonaje! pia unaepueka uunganishe juu kwa juu kabla watu wengine na marafiki hawajajua kuwa uli-disco kwani ulipata division ONE wanaamini wewe ni kichwa. Hizo ni moja ya changamoto zako nina uhakika! Ushauri wangu acha papara tulia kwa mwaka huu plz! Watu walisha disco baadae wakanyanyuka wakafanya wonders, ni vijimambo ukajikuta umeingia nyavuni mkuu! Ningeshauri mwakani uombe chuo kingine ubadili na mazingira using'ang'anie hapo Udsm ili watu wasikuulize maswali mbona umehama chuo na kujua kuwa uli-disco!
Wakuu naombeni ushauri..nimedisco mwaka huu nikiwa second year Udsm sasa nahitaji kufanya maombi upya ya chuo TCU. Kama mnavyojua inahitajika kupeleka barua huko TCU ili ufutwe kabisa kwenye system ndipo uapply,,chuoni (UDSM ) wanatoa tamko kuwa barua zitatoka officially jumatatu na siku hiyo hiyo tarehe 31 august ndiyo deadline. Kuna uwezekano wowote wa kuwahi ili niweze kuapply?
Mi pia nakushauri ukae chini kwanza utulie akili ijipange upya na ikiwezekana utafute hata tempo au shughuli yoyote mtaani ili usikae idle. Then uanze kuangalia mapema program utakayoimudu vyema darasani na ambayo ina mashiko kwenye soko la ajira then ndo uombe tena chuo. Pia kwa kipindi hiki hutakiwi kuwaza au kuangalia nani anakuona au anakusema vibaya isipokua focus zaidi kwenye kuyaandaa maisha yako ya baadae, kaa ukifahamu kwamba kila mja kapangiwa rizki yake na Mola wake hivyo usikate tamaa wala kuvunjika moyo cz maisha ni mtihani na sisi wanadamu ndo wahusika. Nikutakie kila la heri mkuu naamini utapata chuo tena!
mbona hapo ud hao wanyarwanda wanadisco vizuri tu?
Wakuu naombeni ushauri..nimedisco mwaka huu nikiwa second year Udsm sasa nahitaji kufanya maombi upya ya chuo TCU. Kama mnavyojua inahitajika kupeleka barua huko TCU ili ufutwe kabisa kwenye system ndipo uapply,,chuoni (UDSM ) wanatoa tamko kuwa barua zitatoka officially jumatatu na siku hiyo hiyo tarehe 31 august ndiyo deadline. Kuna uwezekano wowote wa kuwahi ili niweze kuapply?