Barua ya wazi kwa Inspector General wa Polisi Tanzania

kamili

JF-Expert Member
Feb 10, 2011
1,213
849
Mheshimiwa nina taarifa mbili kama ifuatavyo:
Tarehe 24/10/2023 kati ya saa tatu na saa nne nilipita Moshi na gari binafsi nikitokea Arusha. Safari yangu hiyo ilikuwa ni safari ndefu iliyoanzia Tanga, Dar, Morogoro, Dodoma, Manyara, Arusha na siku hiyo nilipita Moshi katika safari ya Kurudi Dar. Taafira yangu ni kuwa siku hiyo kati ya Moshi mjini na njia panda nilipigwa faini mara tatu kwa madai ya mwendo kasi! Pamoja na kwamba nililipa faini kupitia mtandao lakini nina mashaka makubwa sana na utendaji wa polisi wetu maeneo haya kwa sababu zifuatazo:

1. Nillipata leseni mwaka 2016 mkoani Mbeya na nimetembea mikoa mingi ya Tanzania lakini hii ni faini ya nne kupigwa nikiwa kati ya Moshi na njia panda na sijawahi kupigwa faini sehemu yoyote Tanzania nje ya Mkoa wa Moshi inayohusiana na mwendo kasi sehemu ya spidi 50!

Picha zote tatu zinazodaiwa zilipigwa maeneo tofauti yenye spidi 50 zinaufanano wa mashaka ufuatao:
(a.) picha zote zilipigwa, mpiga picha akiwa upande wa kulia wa dereve (b) mpiga picha alikuwa nyuzi 45 na uelekeo wa gari (c) gari inaonesha dirisha la dereva lilikuwa limefungwa licha ya kwamba dirisha la gari yangu halikuwa limefungwa tangu tumetoka Arusha. (d) picha zote tatu zilionesha nilikuwa spidi 59!!!. Hizi sababu zinanitia mashaka sana huenda kuna ujanja wa kuedit picha Mkoani Moshi, nasema hivyo kwa sababu sijawahi pigwa faini mahali popote nje ya Moshi na mwendo wangu ni wa kutii sheria bila shuruti. Na tarehe hiyo nilitii sheria vyema ndio maana hata mikoa mingine nilipita salama.

2. kilometa moja au mbili kabla ya kufika Mwanga ukiwa unatokea Korogwe kuna kibanda cha polisi mkono wa kulia. Hapa napo sijawahi pita salama nikiwa natokea upande wa Korogwe kuelekea uelekewo wa Moshi. Hapa nimelipa faini mara sita kati ya 2020 na 2022!!!!. Kimsingi zilikuwa sita, hiyo ya sita ilikuwa June 2022 ambapo walidai kuna daraja nilipita na spidi 65!!! Nilipowauliza hilo daraja lipo wapi walisema lipo nyuma umbali wa KM 15! Baada ya maongezi ya muda mrefu ikiwa ni pamoja na kuwaonesha kitambulisho changu cha kazi ya serikali walinisamehe!

Hii safari yangu ya mwisho ya tarehe 24/10/2023 nikiwa natokea Moshi sikukuta askari hapo nilitamani kupiga picha hicho kibanda but Tanzania imebadilika sana, kuweka picha hapa chochote kinaweza tokea (eg. kukamatwa!, kushtakiwa! kubambikiwa kesi nk) sina hakika ni sheria zimebadilika au utendaji umebadilika.
Kati ya 2016 na Octoba 2023 nimeshapigwa faini mara 10. moja ni ya Tanga sehemu inayoitwa Amboni mwaka 2019 ambapo Bima ya gari ilikuwa ilikuwa imeisha kwa kiasi cha siku 11. Nne ni za kati ya Moshi kuelekea njia panda. Tano ni za Mwanga. Mikoa mingine yote pamoja na Dsm sina faini!

Ombi langu kwako ni kwamba naomba idara yako ijiridhishe juu ya uadilifu wa hawa askari wetu wa Mkoa wa Moshi, na ubora wa vitendea kazi vyao. Binafsi nitaendelea kulipa faini hata kama ni za kubambika kwa sababu kinyume na hapo askari wanasema niende mahakaman kama sijaridhika. But mfumo wa mahakama utachukua miaka kutoa haki, huko ni kupoteza muda na fedha nyingi.
 
Mheshimiwa nina taarifa mbili kama ifuatavyo:
1. Tarehe 24/10/2023 kati ya saa tatu na saa nne nilipita Moshi na gari binafsi nikitokea Arusha. Safari yangu hiyo ilikuwa ni safari ndefu iliyoanzia Tanga, Dar, Morogoro, Dodoma, Manyara, Arusha na siku hiyo nilipita Moshi katika safari ya Kurudi Dar. Taafira yangu ni kuwa siku hiyo kati ya Moshi mjini na njia panda nilipigwa faini mara tatu kwa madai ya mwendo kasi! Pamoja na kwamba nililipa faini kupitia mtandao lakini nina mashaka makubwa sana na utendaji wa polisi wetu maeneo haya kwa sababu zifuatazo:
1. Nillipata leseni mwaka 2016 mkoani Mbeya na nimetembea mikoa mingi ya Tanzania lakini hii ni faini ya nne kupigwa nikiwa kati ya Moshi na njia panda na sijawahi kupigwa faini sehemu yoyote Tanzania nje ya Mkoa wa Moshi inayohusiana na mwendo kasi sehemu ya spidi 50!
Picha zote tatu zinazodaiwa zilipigwa maeneo tofauti yenye spidi 50 zinaufanano wa mashaka ufuatao:
(a.) picha zote zilipigwa, mpiga picha akiwa upande wa kulia wa dereve (b) mpiga picha alikuwa nyuzi 45 na uelekeo wa gari (c) gari inaonesha dirisha la dereva lilikuwa limefungwa licha ya kwamba dirisha la gari yangu halikuwa limefungwa tangu tumetoka Arusha. (d) picha zote tatu zilionesha nilikuwa spidi 59!!!. Hizi sababu zinanitia mashaka sana huenda kuna ujanja wa kuedit picha Mkoani Moshi, nasema hivyo kwa sababu sijawahi pigwa faini mahali popote nje ya Moshi na mwendo wangu ni wa kutii sheria bila shuruti. Na tarehe hiyo nilitii sheria vyema ndio maana hata mikoa mingine nilipita salama.
2. kilometa moja au mbili kabla ya kufika Mwanga ukiwa unatokea Korogwe kuna kibanda cha polisi mkono wa kulia. Hapa napo sijawahi pita salama nikiwa natokea upande wa Korogwe kuelekea uelekewo wa Moshi. Hapa nimelipa faini mara sita kati ya 2020 na 2022!!!!. Kimsingi zilikuwa sita, hiyo ya sita ilikuwa June 2022 ambapo walidai kuna daraja nilipita na spidi 65!!! Nilipowauliza hilo daraja lipo wapi walisema lipo nyuma umbali wa KM 15! Baada ya maongezi ya muda mrefu ikiwa ni pamoja na kuwaonesha kitambulisho changu cha kazi ya serikali walinisamehe!
Hii safari yangu ya mwisho ya tarehe 24/10/2023 nikiwa natokea Moshi sikukuta askari hapo nilitamani kupiga picha hicho kibanda but Tanzania imebadilika sana, kuweka picha hapa chochote kinaweza tokea (eg. kukamatwa!, kushtakiwa! kubambikiwa kesi nk) sina hakika ni sheria zimebadilika au utendaji umebadilika.
Kati ya 2016 na Octoba 2023 nimeshapigwa faini mara 10. moja ni ya Tanga sehemu inayoitwa Amboni mwaka 2019 ambapo Bima ya gari ilikuwa ilikuwa imeisha kwa kiasi cha siku 11. Nne ni za kati ya Moshi kuelekea njia panda. Tano ni za Mwanga. Mikoa mingine yote pamoja na Dsm sina faini!

Ombi langu kwako ni kwamba naomba idara yako ijiridhishe juu ya uadilifu wa hawa askari wetu wa Mkoa wa Moshi, na ubora wa vitendea kazi vyao. Binafsi nitaendelea kulipa faini hata kama ni za kubambika kwa sababu kinyume na hapo askari wanasema niende mahakaman kama sijaridhika. But mfumo wa mahakama utachukua miaka kutoa haki, huko ni kupoteza muda na fedha nyingi.
Asante
 
Hilo swala ni kweli kabisa na huwa wanapiga picha hapo maeneo ya uchira sijui then unakamatiwa njia panda hata leo walikuwepo na ukicheki zile picha vizuri huwa wanapiga ukiwa umeshavuka kibao cha kuruhusu 50 na hapo unaanza kugain momentum ya speed ndo wanakupiga picha tulishatokewa hivyo mara 2 tukabishana sana hadi kurudi sehem ya kupigia picha ambapo mpiga picha huwa anajificha kwenye majani anawarushia njia panda kesho nikipata muda nitapiga picha hapo mpigaji anapojifichaga
 
Polisi wakati mwingine huwa wanakua na vitabia vya ovyo sana kiasi kwamba hata yakitokea matukio ya wao kufanyiwa unyama jamii inachukulia poa tu. Najua sio wote wenye michezo hiyo ila wenye tabia chafu badilikeni inakera sana aseeh
 
Hilo swala ni kweli kabisa na huwa wanapiga picha hapo maeneo ya uchira sijui then unakamatiwa njia panda hata leo walikuwepo na ukicheki zile picha vizuri huwa wanapiga ukiwa umeshavuka kibao cha kuruhusu 50 na hapo unaanza kugain momentum ya speed ndo wanakupiga picha tulishatokewa hivyo mara 2 tukabishana sana hadi kurudi sehem ya kupigia picha ambapo mpiga picha huwa anajificha kwenye majani anawarushia njia panda kesho nikipata muda nitapiga picha hapo mpigaji anapojifichaga
polisi wetu (sina hakika kama ni wetu) wana mambo ya ajabu sana
 
Hapo n machame darajan km unakuja kwa sadalaa
Pale kweye darajan kuna trafiki huwa wanajificha
Ukifika pale usiovatake wala kuzidisha speed
Huko kujificha maana yake wanateleleza majukumu kinyume na sheria na taratibu zetu. Trafiki nayefanya kazi yake kihalali hawezi jificha
 
Back
Top Bottom