Baridi ya Njombe

Baridi ya Njombe

makambako kuna upepo mkali unatokea upande wa njombe ila nikiwa njombe upepo siusikii ina maana ile baridi ya njombe huwa inasukumiziwa makambako au!
Ukiwa njombe baridi lake halina upepo, linaingia kimya kimya, utashtukia tu mifupa ina lalamika, kwangu mimi hili ni baridi baya kuliko la makambako ambalo linaambatana na upepo, ukiukwepa upepo unaipata afadhali
 
Wakuu naombeni ushauri, kajua kametoka sasa shemeji yenu ananilazimisha nikaoge eti kisa keshachemsha maji. Me nimemwambia sijisikii kuoga maana sio lazima. Hapa tumekwazana kwa ajili ya hilo.
Eti jamani kuna haja ya kulazimishana kuoga wakati kila mtu na mwili wake halafu siku zenyewe ambazo sijaoga ni tatu yaani siku tatu tu.
Huo ni mtego usikubali, ukioga maji ya moto huwa raha sana mambo hubadilika pale maji yakaisha kwenye ndoo, ule muda wajifuta maji mpka ukavae nguo utajuta.... Enzi nikiwa Njombe sec, njoss, tulikuwa tunachemshiwa maji jikoni, sufuria nzima ila hakuna anaeenda yagusa, bora uoge tu yabaridi kuliko ya moto
 
Ukiwa njombe baridi lake halina upepo, linaingia kimya kimya, utashtukia tu mifupa ina lalamika, kwangu mimi hili ni baridi baya kuliko la makambako ambalo linaambatana na upepo, ukiukwepa upepo unaipata afadhali
Ya Makambako inapausha,kuumiza macho kwa vumbi na takataka nyingine,shida kwenye usafiri bora ya Njombe ni kuvaa makoti makubwa ya Sufi kama uko Siberia vile
 
Huo ni mtego usikubali, ukioga maji ya moto huwa raha sana mambo hubadilika pale maji yakaisha kwenye ndoo, ule muda wajifuta maji mpka ukavae nguo utajuta.... Enzi nikiwa Njombe sec, njoss, tulikuwa tunachemshiwa maji jikoni, sufuria nzima ila hakuna anaeenda yagusa, bora uoge tu yabaridi kuliko ya moto
Sijawahi oga maji ya baridi whether Niko Dar au Njombe
 
Home sweet home baridi Hilo halitutishi kusarvive!

Nimekulia nyumbanitu huko
Baridi kwetu ni Kama upepo wa Beach tu!

Nadanganya wana Njombe wenzangu?
😂😂😂😂
 
Sijawahi oga maji ya baridi whether Niko Dar au Njombe
Ukiwa njombe ukioga maji ya baridi ni bora unapata shida muda ule wa kuanza oga tu baada ya hapo mwili unazoea, maji ya moto labda kwenye bafu zile zilizotengenezwa kutunza joto tena ndani ya nyumba sio bafu za shule
 
Back
Top Bottom