Barclays bank na noti bandia

Upanga

Senior Member
Jun 18, 2007
145
50
Ndugu zangu,kwanza nawasalimu na kuwapa pole za kujenga Taifa.

Ningependea kuwapa mkasa nilioupata jumamosi iliyopita katika ATM ya Barclays pale OHIO karibu na MOVE N PICK.
Nilifika majira ya saa 4:16asubuhi kutakakutoa fedha.Nilienda moja kwa moja kwenye ATM ya mwisho mkono wa kushoto kama un face hizo ATM.

Kama kawaida nikaingiza kadi na kutaka kutoa tsh 300,000.Mashine ikaandika itatoa ths 200,000 katika mfungu ya ths 5,000,ikawa hivyo.Kisha
nikaingiza tena kadi na ku_draw tshs 200,000 kwa mafungu hayo hayo ya ths 5,000.
Jumla nikawa na tsh 300,000 za mafungu ya tsh 5,000.

Nikaona ngoja niingie ndani nikabadili kwa ths 10,000 bills. Cha ajabu cashier alipoziingiza zile fedha kwenye machine yake akaniambia moja kati ya zile tsh 5000 ni feki. Nikahoji imekuaje iwe hivyo wakati ni ATM yao wenyewe ndo imenipatia? Akaniambia niende kwa SUPERVISOR kwa msaaada.

Nilipojieleza nikachukuliwa maelezo na kuambiwa nirudi jumatatu saa nane, niliporudi nikaambiwa Machine zao haziwezi toka hela Bandia ingawa wanaendelea kufanya uchunguzi nirudi leo jumatano saa tisa.

Sasa cha ajabu mimi nimeripoti kuwa hayo ndiyo yaliyotokea lakini wao wanakazania kuwa haliwezekani, wakati mimi ni shahidi kwa hili, ninachoogopa kama ukichukua hela nyingi kisha ikagundulika ni madudu je mimi kama mteja nianzie wapi kudai haki yangu?

MSAAADA TAFADHALI
 
Mkuu pole kwa yaliyo kukuta. Just dont waste your time and go on with other businesses Provided hujakamatwa kwa kosa La kuwa na noti bandia.

Its only last week nimedraw pesa from one bank to another nakuta Kuna Noti ya Elfu kumi ya Bandia. Kilichofanyika yule Teller aliikunja ile noti kama mara kumi hivi akaipiga paper Punch.

Sasa ningerudije kwenye ile Bank ya kwanza ku claim nilipewa noti Bandia?

Nili conclude Labda one of the Tellers aliichukua hiyo noti mtaani akaamua kuja kuibadilishia kwangu.- Hivi ile sheria inayosema hesabu pesa zako dirishani kabla hujaondoka si mzaha ule? yaani uchukue Burungutu la milioni kumi ukae dirishani uanze kuhesabu na kucheki kama noti zote ni genuine?

Mi nafikiri wangetusaidia tu kwenye ile mashine yao. The have to place it in such away that you can see the numbers During counting.
 
Wakati mwingine jaribu kutumie teller ndani. Barcrays imelalamikiwa sana, hata sijui kwa nini hawajirekebishi.

Tanzania yote yanawezekana. Mtu anakuja na linoti lake feki, na uwezo wa kuichomeka apate genuine kwa nini asifanye hivyo? Bila kuja anaumiza mteja.
 
HAMA BARCLAYS,MIMI NILISHAHAMA
1-Huduma mbovu kichefuchefu
2-wameibiwa pesa nyingi ,internal theft.wafanyakazi wameshiriki ktk utapeli
3-kwa sababu tajwa hapo juu,ukipeleka malalamiko hayasikilizwi.
4-Mteja wa vilaki na vimilioni siyo issue,wateja wa milioni 50 plus huwa wanatoa Tipu nzuri etc.so huduma huwa mbovu kwa style hiyo hiyo.

mwisho ,Pole sana Mkuu.
 
Siku nyengine nenda ndani,

Mie safari moja kuna dada wa CRDB alitaka kunizika laki 7 au sijui tuseme alikosea sijamuelewa mpaka sasa. Nilikwenda katika tawi la CRDB tawi la PPF tower na kutaka kudraw milioni 10. Nikamchukua mdogo wangu mmoja na wakati anazihesabu na kunipa nikawa nahesabu na kuziweka pembeni nikagusa baadhi ya noti nikawa naona baadhi ya zina shaka. Isitoshe hela alizonipa zilikuwa pungufu kama laki sita hivi. Kumrudishia zile noti zake nilizokuwa na shaka nazo akastukia haraka haraka akanipa nyengine zile akaziweka pembeni na nikamwambia hela zako pungufu nikamrudishia zote akaona kweli zilipungua karibia laki sita na ushee.

Ushauri wangu wa bure hesabu hela yako kwa teller kwani sheria ya benki inasema hela unayoihesabu kwa benki bado iko mikononi mwa benki. Hivyo kabla hujaiweka katika mfuko au kuihamisha kokote zihesabu pale pale akiwa anaziona bank teller. Ukitilia shaka noti zozote mrudishie au goma kuchukua hela zote hawawezi kukufanya kitu. Usijali foleni nyuma yako au labda bank teller ana haraka kwani ni kazi yake hesabu hela zako kwa umakini na uangalifu. Kuhusu ATM fanya kama ninavyofanya mimi siku hizi mwisho wa kudraw hela ni Shillingi 15,000. Kuanzia 20,000 na kuendelea naingia ndani ya Bank na kupanga foleni kwa benki teller.

Pole sana na shukuru mungu hujakamatwa kwa kuwa na hela ya bandia.
 
wakuu nafikiri kuna wafanyakazi wasio waaminifu ndani ya bank
jamani watanzania tuache deal za hovyo,tufanye kazi zinazoheshimika!
 
Halafu mi naichukia ile bank kwa ajili ya network yao ni tata sana. Wezi tupu. Na ni hofu ni magamba tu!
 
barclays ya arusha nayo ni uozo mtupu! kuna jamaa yangu alikuwa na deni la mkopo, kuna kipindi kama miezi minne halikuwa hajalipia deni lake kwahiyo kwenye akaunti yake ikainaonyesha deni la nyuma. cha ajabu mfanyakazi wa barclays kitengo cha mikopo akaomba rushwa ili jamaa afutiwe deni la nyuma la laki 9. jamaa alimpa huyo mfanyakazi elfu 40!!!! duuu, nilishangaa !!!! kichefuchefuuuu!!!!
 
Back
Top Bottom