Bandarini si wizi bali kufuru: Meli nzima 'yaibiwa'

Bandarini si wizi bali kufuru: Meli nzima 'yaibiwa'

Mkuu...Hivi unaelewa unachosema?

Hakujawahi kutokea tangu bandari ianzishwe meli za makontena toka china zikashusha mzigo wote Dar..Home shopping alikuwa haagizi meli nzima..Bali makontena yanapakiwa kwenye meli
Mkuu unaambiwa hilo limetokea wewe unaweka ufahamu wako!
Wapi na wapi!
 
Makubwa yamezidi kugundulika kwenye sakata la upotevu wa makontena Bandari ya Dar na sasa inadaiwa kuwa kuna nyakati wahusika wamewahi kufuta kumbukumbu za meli nzima ya makontena na kuiba makontena yote.

Taarifa hizo zinavuja wakati kukiwa na mvutano kati ya chama cha Mawakala wa Forodha Tanzania (TAFFA) kinachodai kutohusika kwa namna yoyote na upotevu wa makontena zaidi ya 11,000 ambayo hayakulipiwa ushuru bandarini (Wharfage charges).

TAFFA wanaitaka Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), kuwajibika katika upotevu huo ulioinyima Serikali kupitia mamlaka hiyo mabilioni ya fedha.


Chanzo: Raia Tanzania
hatary sana hiyooo
 
na hili swala litaisha hivi hivi kwasababu waliofanya hivyo ndio walio muweka pale makufuri na hamna wa kuuliza.
 
Hii kitu kama ni.kweli basi tupo jehanam. Ni kwanini Polisi kitengo cha bandari wengi wana ma prado? Tra longroom wengi wanapesa ya kufa mtu. TPA hata ajira pale hupati bila connection ya mtu fulani kiongozi. Kwanini ma Port Manager wote waliowahi kuwa TPA ni mabilionea. TUTAFAKARI NA HATUA ZICHUKULIWE
 
Soon bandari nzima itaibiwa.
Siyo siri, soon tutaambiwa kuwa kumbe bandari ya Dar es Salaam inamilikiwa na Rwanda..., na serikali inalipwa fedha za pango tu kama landlord! Tanzania hii ni zaidi ya tuidhaniavyo.
 
Ni wakati muhimu sasa wa kuunda Nasacco mpya japo nakumbuka miaka ile pia walichoma moto jengo lote kupoteza ushahidi wa ubadhirifu wao.
 
Duh! Kikwete sina cha kukuambia! Ila nimeamini ule usemi usemao Sura sio Roho. Watu wanakufa kwa kukosa Antbiotic na muda huo huo kuna mabilioni yana pigwa bila hata ya Huruma! Mkwere ameweka historia aisee.
 
Anayeyafurumua ulimpa kura?
Na uliyempa kura angeweza spidi hii ?
Sipidi toka wapi? Maana aliyekuwa anampigia Kampeni ndiye yeye anayesemwa kufanya yote hayo! Jee yeye kakamatwa kwa kuendesha kiholela serikali hadi yote hayo yanatokea?
 
Ikulu iibiwe? Ina thamani ya sh ngapi mtaa wa congo kariakoo?Vinavyoibiwa vina thamani kubwa na kutafutwa mitaa ya kariakoo.
Ina thamani kubwa kwa sababu yule mzito mwenye makazi yake pale ndiye bosi wa mambo yote yenye thamani mtaa wa Kongo kariakoo. Tusishangae kusikia kuwa hao 'walioiba meli' waliweza kufanya hivyo baada ya 'kuiiba ikulu' kwanza.
 
Magufuli hebu Nyonga watu basi, Nchi inadharirika mchana kweupe, meli nzima watu wanapakua hebu rausi fanya haya yafuatayo
Futa ajira za wafanyakazi wote wa bandaini uajiri upya, maana waneitia nchi aibu kubwa sana, jambo lingine la kushangaza watu wanaiba meli nzima halafu wakipelekwa mahakamani wanaachiwa kwa dhamana, jamani pamoja na kuwa kila mhimili unajitegemea lakuni mahakamani kunanuka Rushwa kubwa sana.
 
Jakaya ninmtu mmoja mtabaki kumkumbuka ila magufuli awezi ongoza nchi ccm ndio baba yake atulie wajanja wale nchi
 
Back
Top Bottom