Balozi wa Marekani nchini Tanzania atembelea Ofisi za JamiiForums

Ni wazi JF inaheshimika na kutambulika zaidi ya media nyingi hapa Tanzania, sasa JF waangalie uwezekano wa kuanzisha magazeti, luninga, na radio station yao.

Hizi ziara za hawa mabalozi zinaonesha vile kizuri kinavyojiuza...
Swadakta
 
Ni jambo jema sana kwa mabalozi mbalimbali wanapotembelea ofisi za JF. Hii inatoa taswira moja muhimu sana. Na pia inatoa ujumbe muhimu sana ndani ya jamii yetu.

Mchango wa JF ni wenye kuthaminika mno ndani na nje ya mipaka ya Tanzania.

Kazi kubwa inayofanywa na ofisi hii katika kusimamia maudhui ya habari, kusimamia "privacy" ya watoa habari, na hata kutoa habari za uhakika na zenye kuaminika kwa wakati ni alama pekee ambayo wana jukwaa tunajivunia.

Nichukue nafasi hii kuupongeza uongozi mzima wa JF na wanajukwaa wote kwa ujumla. Natoa ofa ya kinywaji kwa wanajukwaa wote, ila angalizo tu kila mmoja anywe kwa gharama zake mwenyewe.
 
Hongera sana Maxence Melo and Team JF.

Kutembelewa na ujumbe huu mzito ni kutambulika kwa kazi nzuri ya JF katika kutoa maoni yanayozingatiwa na viongozi wa nchi.
Hii ni medium ya ukweli, haraka, na kupima joto la wananchi kwa haraka haraka.

Hongereni sana.
 
Ni mawazo yako yaliyopitwa na wakati

Unafikiri ule ubalozi wa Marekani Tanzania ulijengwa na pesa za Babu yako?

Kama Balozi hatambuliki zile chanjo za korona zilitolewa kwa msaada zilitoka Marekani au kwenye Familia yako hapo Mbezi ya Tangi bovu

Unafahamu maana ya Balozi, Balozi ni muwakilishi wa Rais Katika nchi husika

Huyo Balozi ndiye muwakilishi wa Biden hapa Tanzania, Raia wa Marekani kufahamu au kutokufahamu inategemea kama wana lengo la kuja Tanzania au kuna tukio kubwa sana Tanzania

Obama alivyofika Tanzania, alifikia nyumbani kwenu hapo Tangi bovu au alielekea kwenye ubalozi wake kwanza

Kuna watu wazima humu jamii forum lakini wana mawazo ya kipuuzi na kipumbavu sana

Mimi mtanzania sina lengo la kwenda Iraq, Syria, Somalia, Au Cambodia,. Nianze kuulizia mabalozi wa huko kwa faida gani?

Balozi ana kazi zake maalum na hapo kwenda jamii forum ana mambo anayotaka kujifunza na kuyaona ili ajiongezee maarifa na uzoefu Katika maisha yake

Wewe Nyani ngabu una mfahamu Balozi wa Tanzania huko uzebakstan? au nchi ya Tajikstan?

Sasa Mimi nimeishia huko uzebakstan na Balozi anayesimamia huko namfahamu vizuri toka Tanzania, Watu ambao hawana mpango wa kwenda huko uzebakstan wamtafute Balozi wa kazi gani?
Binafsi nimemdharau na.kumpuuza huyu jamaa. Achana nae tu.
 
Kuna watu huwa nawaona wanacomment sana ujinga ila nafikiri ikitokea siku moja JAMII FORUM imepotea itawaacha na kovu la uchizi wa akili. Jamii forum ni kisiwa cha maarifa yeyote

Watanzania wengi waliopo nnje ya nchi mtandao huu ni sehemu ya familia zao

LonG live
 
Hakuna mzungu anaefanya jambo lake Kwa bahati mbaya.

Jf ni nzito sana na kama kumbukumbu zangu ziko sahihi kipindi cha uongozi wa Hayati Magufuli Melo alikuwa akisumbuliwa sana juu ya JF nafikiri ni Kwa sababu ya uzito wa Jf na watu wake.

Mambo ni mengi😄😄huwezi jua labda ndio baraka zenyewe.
👊🏿👊🏿👊🏿

Hebu fafanua kidogo, baraka za nini.
 
Hebu fafanua kidogo, baraka za nini.
Kwani Baraka ni nini?

But again mzungu hafanyi kitu bila sababu/malengo.

Hawa watu wanakuwaga na malengo ya muda mrefu😄😄juzi Sweden leo American
 
Hongera Melo, kutokusaliti jukwaa Zama za Giza za Meco. Asante Mh.Balozi Ni heshima na joto kwa wapigania Haki na Uhuru wa habari.
 
View attachment 2107919

Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Mhe. Donald Wright leo Februari 4, 2022 ametembelea Ofisi za JamiiForums na kukutana na watendaji na mwakilishi wa Bodi ya Wakurugenzi

Balozi Wright na timu yake wamepata kuelezwa namna Jamii Forums ambayo ni Asasi ya Kiraia inavyoendesha shughuli zake katika kufanya uchechemuzi wa Haki za Kidijitali, Uwajibikaji, Demokrasia na Utawala Bora nchini Tanzania

View attachment 2107923View attachment 2107924View attachment 2107925

View attachment 2107922
Kaka MM na team nzima ya JF, kwa mara nyingine tena Hongereeni sana!!

Hizi ni dalili za wazi kabisa kwamba katika ule muundo wa Kikao cha Mabalozi walio na balozi au uwakilishi wa Nchi zao hapa Tanzania, agenda ya JF imetua mezani kwao na ikaongelewa kwa umahiri na umakini mkubwa.

Kwa hayo tuyaonayo, kwa hakika JF muda si mrefu mtakuwa ktk anga (level) nyingine kabisa kwa yale mnayoyafanya kwa niaba ya Watanzania tulio wengi. Tegemeeni ushauri mkubwa sana wa Teknolojia na wa Uendeshaji wa shughuri zenu.

Nimesema hayo pia baada ya kuwaona wajumbe walioambatana na Balozi.

Hongereeni Sana JF. Pigeni Kazi.
 
Ni mawazo yako yaliyopitwa na wakati

Unafikiri ule ubalozi wa Marekani Tanzania ulijengwa na pesa za Babu yako?

Kama Balozi hatambuliki zile chanjo za korona zilitolewa kwa msaada zilitoka Marekani au kwenye Familia yako hapo Mbezi ya Tangi bovu

Unafahamu maana ya Balozi, Balozi ni muwakilishi wa Rais Katika nchi husika

Huyo Balozi ndiye muwakilishi wa Biden hapa Tanzania, Raia wa Marekani kufahamu au kutokufahamu inategemea kama wana lengo la kuja Tanzania au kuna tukio kubwa sana Tanzania

Obama alivyofika Tanzania, alifikia nyumbani kwenu hapo Tangi bovu au alielekea kwenye ubalozi wake kwanza

Kuna watu wazima humu jamii forum lakini wana mawazo ya kipuuzi na kipumbavu sana

Mimi mtanzania sina lengo la kwenda Iraq, Syria, Somalia, Au Cambodia,. Nianze kuulizia mabalozi wa huko kwa faida gani?

Balozi ana kazi zake maalum na hapo kwenda jamii forum ana mambo anayotaka kujifunza na kuyaona ili ajiongezee maarifa na uzoefu Katika maisha yake

Wewe Nyani ngabu una mfahamu Balozi wa Tanzania huko uzebakstan? au nchi ya Tajikstan?

Sasa Mimi nimeishia huko uzebakstan na Balozi anayesimamia huko namfahamu vizuri toka Tanzania, Watu ambao hawana mpango wa kwenda huko uzebakstan wamtafute Balozi wa kazi gani?
Bwahahahahahahaa, hii sasa ni kumi bila, KNOCK-OUT kabisa.
Aisee, Maxence Melo hongera sana braza, nuru imekuzukia.
 
Back
Top Bottom