Balozi Dr. Dau (PhD), mtumishi wa kupigiwa mfano

Valencia_UPV

JF-Expert Member
Mar 31, 2016
6,223
7,409
Kwenye ukweli tuseme ukweli, msomi na mwanadiplomasia nguli Dr. Dau (PhD) amefanya kazi nzuri ya kulirekebisha shirika/mfumo wa hifadhi ya jamii NSSF.

Ameanzisha miradi mingi yenye tija kwa taifa na wanachama wa NSSF.

Wakati akielekea kwenye majukumu ya Kidiplomasia kama Balozi wetu ughaibuni, tunamtakia kila la heri na akatuwakilishe vema huko Kuala Lumpur.
 
Jamani, kila watu wakijaribu kusahau machungu ya NSSF, ghafla anatokea mpuuzi mwingine kutukumbusha kitu kile kile! Please, watu wamepumzika kusubiri kauli ya wenye dhamani na mahakama ya nchi hii (kama itafikia hatua hiyo). Dont take us back kujadili upuuzi huu, PLEASE.
 
Mwenyekiti wa African Union Commission ni ulaji mwingine sema sasa kule utapiga dili gani? majengo wanayo tayari hamna ujenzi mpya
 
Kwenye ukweli tuseme ukweli, msomi na mwanadiplomasia nguli Dr. Dau (PhD) amefanya kazi nzuri ya kulirekebisha shirika/mfumo wa hifadhi ya jamii NSSF ameanzisha miradi mingi yenye tija kwa taifa na wanachama wa NSSF. Wakati akielekea kwenye majukumu ya Kidiplomasia kama Mwenyekiti mpya wa African Union (Tetesi - baada ya Dr. Nkosazana Zuma kumaliza muda wake mwezi july, 2016) tunamtakia kila la heri na akatuwakilishe vema huko Addis Ababa.

Wewe ama zuzu kichaa au siasa kali a.k.a ISIS au una Phd meaning parmanent head damage!
 
Kwenye ukweli tuseme ukweli, msomi na mwanadiplomasia nguli Dr. Dau (PhD) amefanya kazi nzuri ya kulirekebisha shirika/mfumo wa hifadhi ya jamii NSSF ameanzisha miradi mingi yenye tija kwa taifa na wanachama wa NSSF. Wakati akielekea kwenye majukumu ya Kidiplomasia kama Mwenyekiti mpya wa African Union (Tetesi - baada ya Dr. Nkosazana Zuma kumaliza muda wake mwezi july, 2016) tunamtakia kila la heri na akatuwakilishe vema huko Addis Ababa.
Umetumwa kuja kupima upepo??? Watu bado tuna machungu na 1.3t zetu.. Nyau weeeee!!
 
wivu unawasumbua nyie wagalatia!!! acheni hizo! daraja mnaliona na UDOM imejengwa shida nini tena? mbona hamuhoji RICHMOND?
 
nchi hii kama si mgalatia basi ni unapikiwa majungu mpaka uchoke, kaingia Mhe. Prof. Alhaji CAG yameanza makelele utadhan anachinjwa nguruwe parokiani. jamani hii nchi ni yetu wote
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom