Kasheshe
JF-Expert Member
- Jun 29, 2007
- 4,694
- 787
. Bila shaka ndiyo mwanzo mkubwa wa kusambaratika kwa CCM. Wapinzani kwa ujumla kwanini kusifanyike kwa maandamano nchi nzima ya kumuunga mkono aliyefichua bomu hili na kulaani vikali wizi na uzembe wa CCM?..
Unamjua aliyefichua hilo bomu kabla hujaiitisha maandamano! Au unakurupuka tu? Angalia quote hii kutoka page 2 ya thread hii!!!
Sakata la BoT lilianza kufukuta kwa muda mrefu kupitia vyombo vya habari vilivyokua vikihoji hasa ujenzi wa majengo pacha ya benki hiyo na matumizi mabaya ya fedha za umma kupitia mifuko na dhamana kwa wakopaji wakubwa ambao walianza kuonyesha dhahiri kuwa ukopaji wao ulikuwa wenye shaka kubwa.
Baada ya kujadiliwa kwa muda na vyombo vya habari, jina la BoT lilianza kuingia pole pole ndani ya vikao rasmi ikiwa ni pamoja na vikao vya Bunge ambako Mbunge wa Karatu kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Dk. Willibrod Slaa, aliongeza kasi ya waandishi wa habari kujua undani wa matumizi mabaya kupita kiasi ya fedha ndani ya Serikali kupitia Benki Kuu na Hazina.
Dk. Slaa alifikia hatua ya kutaka kuwasilisha hoja binafsi akitaka kuundwa kwa Kamati Teule ya Bunge kuchunguza matumizi mabaya ya kutisha ndani ya BoT, hoja ambayo iligonga mwamba hata kabla ya kuwasilishwa na badala yake kambi nzima ya Upinzani kuamua kuanza kutoa baadhi ya vipengele katika mikutano ya hadhara.
Hata hivyo, wakati Dk. Slaa akizungumzia BoT ndani ya Bunge, tayari Serikali kupitia Waziri wa Fedha, Zakia, ilikwisha kutangaza kufanya uchunguzi wa kuhusu matumizi ya fedha za Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) lakini bila kufanya uchunguzi katika maeneo mengine pamoja na kuwa maeneo hayo yamekuwa yakichunguzwa na vyombo vya dola.