Kichuguu
Platinum Member
- Oct 11, 2006
- 17,825
- 24,481
Bakwata yataka ustahimilivu viongozi wa dini
Mwandishi Wetu
BARAZA Kuu la Waislam (Bakwata), limewataka waumini wa dini za Kikristo na Kiislamu na madhehebu mengine nchini kuendelea kustahimiliana katika mustakabali mzima wa maendeleo ya taifa.
Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, jana jijini Dar es Salaam, Mufti wa Tanzania, Sheikh Issa Shaaban Simba alisema, ustahimilivu ni suala la msingi sana na hasa kwa kuwa tangu nchi imepeta uhuru kumekuwapo tabia njema ya kuvumiliana bila kujali dini ya mtu.
"Watanzania tunatakiwa tuendeleze tabia ya uvumilivu na kuwatazama viongozi hao si kwa dini bali kwa uadilifu na utendaji wa kuwatumikia wananchi,"alisema.
Aliendelea, " tunawaomba Watanzania waendelee kuwa wastahamilivu kwa sababu nchi hii tunaiendesha kwa kuvumiliana."
"Tusiwatazame viongozi kwa dini zao na tunaomba linapotokea jambo linalohitaji kukosoa kiongozi basi busara itumike na wala siyo jazba, kejeli au dharau," alisema.
Katika taarifa hiyo, Mufti Simba alisema kuvumiliana na kustahimiliana kwa madhehebu mbalimbali Tanzania ndiyo nguzo ya amani na utulivu ambao umedumu tangu taifa lipate uhuru wake mwaka 1961.
"Tunaombeni ndugu zetu Watanzania tuendelee ta tabia njema ya kuvumiliana ili tuendeleze mustakabali mwema wan chi yetu,"alisema Mufti.
NOTES: Mufti ameonyesha kuwa mtu mwenye busara sana kuliko Masheikh wotee waliokuwa wakitoa matamko siku za hivi karibuni. Hivi matamko hayo yaliyotolewa na waislamu siku za nyuma hayakuwa na baraka za BAKWATA? Na kama yalikuwa na baraka za BAKWATA, ujumbe huu wa Mufti unawalenga nani zaidi. Kwa vyovyote hauwalengi maaskofu kwa vile wao walikosoa serikali na wala hawakutamka lolote kuhusu dini ya kiislamu, ila matamko ya mashehe ndiyo yalikuja na kushambulia dini za kikristo hasa katoliki.
Mwandishi Wetu
BARAZA Kuu la Waislam (Bakwata), limewataka waumini wa dini za Kikristo na Kiislamu na madhehebu mengine nchini kuendelea kustahimiliana katika mustakabali mzima wa maendeleo ya taifa.
Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, jana jijini Dar es Salaam, Mufti wa Tanzania, Sheikh Issa Shaaban Simba alisema, ustahimilivu ni suala la msingi sana na hasa kwa kuwa tangu nchi imepeta uhuru kumekuwapo tabia njema ya kuvumiliana bila kujali dini ya mtu.
"Watanzania tunatakiwa tuendeleze tabia ya uvumilivu na kuwatazama viongozi hao si kwa dini bali kwa uadilifu na utendaji wa kuwatumikia wananchi,"alisema.
Aliendelea, " tunawaomba Watanzania waendelee kuwa wastahamilivu kwa sababu nchi hii tunaiendesha kwa kuvumiliana."
"Tusiwatazame viongozi kwa dini zao na tunaomba linapotokea jambo linalohitaji kukosoa kiongozi basi busara itumike na wala siyo jazba, kejeli au dharau," alisema.
Katika taarifa hiyo, Mufti Simba alisema kuvumiliana na kustahimiliana kwa madhehebu mbalimbali Tanzania ndiyo nguzo ya amani na utulivu ambao umedumu tangu taifa lipate uhuru wake mwaka 1961.
"Tunaombeni ndugu zetu Watanzania tuendelee ta tabia njema ya kuvumiliana ili tuendeleze mustakabali mwema wan chi yetu,"alisema Mufti.
NOTES: Mufti ameonyesha kuwa mtu mwenye busara sana kuliko Masheikh wotee waliokuwa wakitoa matamko siku za hivi karibuni. Hivi matamko hayo yaliyotolewa na waislamu siku za nyuma hayakuwa na baraka za BAKWATA? Na kama yalikuwa na baraka za BAKWATA, ujumbe huu wa Mufti unawalenga nani zaidi. Kwa vyovyote hauwalengi maaskofu kwa vile wao walikosoa serikali na wala hawakutamka lolote kuhusu dini ya kiislamu, ila matamko ya mashehe ndiyo yalikuja na kushambulia dini za kikristo hasa katoliki.