Orketeemi
JF-Expert Member
- Feb 12, 2013
- 4,340
- 10,087
Baraza la Waislamu Tanzania limeitaka Serikali kufafanua maeneo yanayotiliwa shaka kuhusu uwekezaji bandari.
Dar es Salaam. Katibu Mkuu wa Baraza la Waislamu Tanzania (Bakwata), Nuru Mruma ametoa wito kwa Serikali kupokea maoni ya wananchi kuhusu sakata la Bandari, huku akiitaka ifafanue maeneo yote yanayotiliwa shaka.
Hayo ameyasema leo Alhamis Juni 29, 2023 akihutubia Baraza la Eid El-Adh'haa lililofanyika katika Msikiti wa Mfalme Mohammed wa VI wa Morocco jijini hapa.
"Pia Serikali inapaswa kutoa elimu kwa wananchi ili waendelee kuuelewa mradi huu (uwekezaji bandari)," amesema.
Mruma amesema kubainika kwa mradi huo kuliibua mjadala na taharuki kwa wananchi ambao hawakuwahi kuwa na taarifa sahihi kuhusu mradi huo.
Mruma ameitaka Serikali kupokea maoni ya wananchi na kutoa ufafanuzi kwenye maeneo yote yanayotiliwa mashaka.
Hiyo ni kauli ya kwanza kutoka Bakwata tangu uanze mjadala baada ya Serikali kusaini mkataba wa awali wa ushirikiano wa uwekezaji na uboreshaji bandari na Serikali ya Dubai kupitia kampuni ya Dubai Port World.
Dar es Salaam. Katibu Mkuu wa Baraza la Waislamu Tanzania (Bakwata), Nuru Mruma ametoa wito kwa Serikali kupokea maoni ya wananchi kuhusu sakata la Bandari, huku akiitaka ifafanue maeneo yote yanayotiliwa shaka.
Hayo ameyasema leo Alhamis Juni 29, 2023 akihutubia Baraza la Eid El-Adh'haa lililofanyika katika Msikiti wa Mfalme Mohammed wa VI wa Morocco jijini hapa.
"Pia Serikali inapaswa kutoa elimu kwa wananchi ili waendelee kuuelewa mradi huu (uwekezaji bandari)," amesema.
Mruma amesema kubainika kwa mradi huo kuliibua mjadala na taharuki kwa wananchi ambao hawakuwahi kuwa na taarifa sahihi kuhusu mradi huo.
Mruma ameitaka Serikali kupokea maoni ya wananchi na kutoa ufafanuzi kwenye maeneo yote yanayotiliwa mashaka.
Hiyo ni kauli ya kwanza kutoka Bakwata tangu uanze mjadala baada ya Serikali kusaini mkataba wa awali wa ushirikiano wa uwekezaji na uboreshaji bandari na Serikali ya Dubai kupitia kampuni ya Dubai Port World.