BAKWATA ni tawi la Kanisa

BAKWATA ni tawi la Kanisa

Status
Not open for further replies.

Kipenzi Changu

Platinum Member
Joined
Aug 24, 2011
Posts
58,015
Reaction score
134,217
Jamani makubwa nayasikia hapa kupitia Star TV.Wachambuzi maustaadh wanaeleza hadith za Mtume hasa mfungo na sikukuu ya Idi.Sasa hapa kwenye hitimisho ndio wamesema waislam waachwe waunde chombo chao wenyewe na si hii BAKWATA.

Wamesema Uundwaji na BAKWATA umechambuliwa vizuri na mwenzetu Mohamed Said kwamba malengo ya BAKWATA sio mazuri.Mwisho kabisa wamesema BAKWATA ni tawi la Kanisa....

My Take:

R.I.P Mwalimu Nyerere na mafunzo yako juu ya mshikamano
 
wanapenda vurugu sana hao, wanatafuta kiki kupitia bakwata
 
Dunia nzima waislam wanalia kuonewa. Na hii ni kwa sababu duniani kote sharia za kiislam hazitekelezeki. Hata mataifa ya kiislam yenyewe yameshindwa kutekeleza sharia za kiislam, ndio maana utaona huko huko uarabuni kuna vikundi vinapigana na serikali ili kutekeleza utawala wa sharia. Kwa kifupi ni kwamba utawala wa sharia hautekelezeki. Na kama wakilazimisha basi watu wengi watahama nchi hizo kwenda kwenye nchi za kikristo kama tunavyoona leo waarabu na wasomali wanakimbilia ulaya
 
Waislamu wananishangaza wanadai BAKWATA imeundwa na Serekali na ni tawi la Kanisa.Nasema sawa Waislam hao hao kila siku wanataka kuundiwa Mahakama ya Kadhi na serekali sijui nayo itakuwa tawi la Kanisa.

Nani kawazuia waIslam kuunda chombo chao.
 
Muongee vizuri na Rashid Othman (Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa).

Kama serikali inawachukulia waislamu kama security threat, basi mjue kuwa itaendelea kutaka iwe na control kwenye vyombo vyenu. Hata mkiviunda wenyewe, bado watahakikisha wanaweka 'watu wao' au pia wanaweza kuwa 'divide' ili msiwe na nguvu ya pamoja.
 
Jamani makubwa nayasikia hapa kupitia Star TV.Wachambuzi maustaadh wanaeleza hadith za Mtume hasa mfungo na sikukuu ya Idi.Sasa hapa kwenye hitimisho ndio wamesema waislam waachwe waunde chombo chao wenyewe na si hii BAKWATA.Wamesema Uundwaji na BAKWATA umechambuliwa vizuri na mwenzetu Mohamed Said kwamba malengo ya BAKWATA sio mazuri.Mwisho kabisa wamesema BAKWATA ni tawi la Kanisa....My Take:R.I.P Mwalimu Nyerere na mafunzo yako juu ya mshikamano
Waislam ukiwaacha wenyewe bila usimamizi madhubuti watamalizana na watamaliza wasio waislam, waislam wanahitaji kuongozwa na sio kujiongoza,mwl alilijua hilo ndio maana akaamua kuwaanzishia bakwata, vinginevyo wangemalizana, maana wao kwa wao hawaelewani,washia hawaelewani na wasuni nk.
 
Last edited by a moderator:
he! Kanisa lipi hilo. Mbona hatujaona mchungaji huko au anaenda kwa siri, ila kuita bakwata ni tawi la kanisa ni u.t.o.t.o.
 
Waislamu wananishangaza wanadai BAKWATA imeundwa na Serekali na ni tawi la Kanisa.Nasema sawa Waislam hao hao kila siku wanataka kuundiwa Mahakama ya Kadhi na serekali sijui nayo itakuwa tawi la Kanisa.

Nani kawazuia waIslam kuunda chombo chao.

mkuu hwa jamaa wajitathmini maana hata wao kuibia elimu zama zile na kuishia kufuga ndevu na kucheza bao leo wanailaumu serikali kwa wao kukosa elimu na wanasemani mfumo kristo
 
Kanisa,Msikiti..
yote ni majengo ya imani zilizochipukia kwa watu weupe wanaotuita sisi WAAFRIKA manyani.
Walileta imani hizi wakidai Waafrika hatuna ustaarabu wala imani sahihi ya Kimungu.
Mungu alileta Mitume kwenye jamii zilizozama katika dimbwi la maovu.
fungua macho uone nani alipotea kati ya watu weupe na weusi.
Mpende Mungu mpende ndugu yako mpende jirani yako.
Madhehebu unayoyabeba ni imani yako tu juu ya hatima yako baada ya maisha haya.
 
Kua BAKWATA ni tawi la serikali na imeundwa kuisaidia serikali pamoja na Chama Tawala (CCM) hii naiamini kabisa, haina shaka na ni ukweli mtupu. Bakwata ni taasisi mojawapo tu kundi moja na Jumuia ya Wazazi CCM, UWT & UVCCM.

ila Kua BAKWATA ni tawi la kanisa hii siiamini na haina ukweli wowote.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom