BAKWATA na Mauaji Arusha

BAKWATA na Mauaji Arusha

Jamani udini huko wapi hapa!!! Aliyekataliwa kutambuliwa na maaskofu ni mkristo wala sio muislamu. Je angekuwa ni muislamu ingekuwaje???? Ni wapi maaskofu wa Arusha wametamka kwamba hawamtaki Kikwete kwa kuwa ni muislamu? Huu ni ujinga uliokithiri na kujaribu kutafuta mchawi wakati ukweli unajulikana!!! Hawa wanasahau kwamba ni kanisa hilo hilo liliowahi kutamka kwamba Kikwete ni chaguo la Mungu? Mbona waislamu hawakuipinga hiyo kauli? This sounds like cheap politics to me!!!

Tiba

Nikuulize wewe maaskofu wanawakilisha chama gani? Kama hawamtambui meya wa Arusha? It is a cheap politics but combine with massive poverty, stupidity, and gross injustice towards muslims it will lead to something no one anticipated. Kumbuka vita vingi duniani huanza kimzaha zaha hivi hivi wakukemewa ni maaskofu kwa kulianzisha na sio masheikh wao wanaweka sawa na tu na kuwastua maaskofu hii SIO NCHI YA KANISA!!!
 
... ukweli ni huu hapa... NDIO KIKWETE HAFAi... wote tulopiga kura kutaka mabadiliko tulifanya hivyo kwa zaidi ya asilimia 60!! Hafai, hatumtaki. Ndio
 
Kwa taarifa yenu ni kuwa wakuu wa polisi wanalaumu Usalama wa taifa uliowapenyezea taarifa potofu za kiintelijensia zilizosababisha kusitisha maandamano bila kutathmini madhara ya kuzuia dakika za mwisho. Wanasema usalama wa taifa kweli sasa unaelekea kuwahalibia kazi maana wao(usalama wa taifa) wanafanya kazi za CCM zaidi kuliko za taifa
 
Ndg zangu wana JF salaam kwenu.

ccm nadhani sasa tumetambua mdini ni nani, aua nani anainitiate udini Tanzania. Ni ukweli ulio wazi kwa yoyote ambaye anachambua bila kushabikia dini yoyote, wala chama chochote wala mtu yoyote, atagundua kuwa wanaoanzisha udini ni viongozi wa ccm kwa maslahi yao binafsi.

huku mtaani hakuna udini mnaoutamka nyie walafi wa madaraka sisi tunaishi kwa amani na dini zote, na kwa taarifa yenu we need Changes.

MAASKOFU,MASHEHE, MAIMAMU NA WACHUNGAJI, endeleeni kuikosoa na kuikemea serikali na vyama vingine vyote bila kuogopa lolote maana tunajua mwisho wao umefika. WE NEED CHANGES

mimi ni muislam safi kabisa lakini simfagilii Kikwete japo ni dini moja na pia siwapendi Lowasa na mafisadi wengine weather waislam au wakristo, na kuna rafiki zangu wengine ni wakristo nao wako kama mimi au tofauti na mimi.

ccm wanapenda mara zote kusifiwa, wakikemewa au kukosolewa wanaanza kuzungumzia udini, mbona wakisifiwa wanafurahi na kuwapongeza viongozi wa dini?

wamegundua mwisho wao umekaribia na sasa wanatafuta njia za kujikomboa, moja ya njia ni kuwagawa watu kwenye udini huku wao wakijifanya neutral...,
 
Wewe kweli unatumia makalio kufikiri,Hapa JF unamjua nani kuwa ni mkristo au mwislamu? au unakutana nao kwenye kuswali au kusali? acheni ujinga basi! dini inawafanya hata kufikiri mnashindwa? mmeng'ang'ania kubishana ukristo na uislamu, mbona kuna dini nyingi tuu, Budha,hindu nk na hawana kelele? Kama kiongozi mbovu asiambiwe kwa vile ataonekana anaambiwa kwa vile dini ni tofauti? mawazo ya kipumbavu ya aina hiyo sijui yametoka wapi! mbona awamu hii ujinga umezidi sana? hivi ujinga huu ni asili yenu au umepandikizwa kwa maslahi fulani?

First of all ukae ukilijua na wenzio walifahamu kuwa WAISLAMU NI WENGI KUSHINDA WAKRISTO TANZANIA na wamekuwa kimya muda mrefu sasa the sleeping giant is awakening my friend. Pili wakristo na waislamu ndio dini mbili kuu Tanzania wahindu na wengineo wanapercentage yao but wakichambuliwa hawafikiii wengi kama waislamu na wakristo sasa it is important for these two groups to reconcile.
 
Wana siri ya pamoja, lengo likiwa ni kuhakikisha wanashika nchi ili kanisa liendelee kushika hatamu na UTAMU wa nchi hii. JK kawanyang'anya utamu kupitia MoU kati ya kanisa na serikali. JK alitaka awanyime utamu baada ya mwaka jana kutaka mali zinazoingizwa na makanisa nchini zilipiwe kodi. Leo wanasema hawamtambui Meya Arusha kisa mauaji. Mbona hawakumtambua Rais baada ya mauaji ya januari 21 ambapo watu 27 waliuawa na wanawake kubakwa. AU NI SIASA ZA UZANDIKI?

Kwa post hii, sitaki kuamini kwamba sehemu kubwa ya Waislam wana uwezo mdogo sana kufikiria mambo kisayansi, Pia sitaki kuamini kwamba sehemu kubwa ya waislam wanaamini kwamba muislam akifanya kosa akihojiwa na Mkristo inamaanisha kupiga vita uislam hata kama kwa kufanya hivyo kuna maslahi ya kitaifa. Pia sitaki kuamini kwamba Sehemu kubwa ya waislam wanaamini Jk Yupo madarakani kihalari na yeyote anaye charange utaratibu uliotumika kumuweka madarakani anapiga vita Uislam. Nasisitiza sitaki kuamini hivyo japo kuna watu wana lazimisha watu tuamini hivyo rasmi.
 
Vatican imekiri wapi kuhusika na mauaji ya Rwanda? Tuwekee japo link au source ya maneno yako?
[/SIZE][/FONT]

Nimeitoa hapa:
Pope must acknowledge role in Rwanda genocide

Sasa mwenzetu hizo apologies umezisikia wapi?

Kwani kuna mtu anabisha kuwa kuna raia waliuawa Pemba, Unguja na Dar es Salaam kama ilivyotokea Arusha?

Amandla....

Mkuu naomba unifafanulie hichi kipengele katika nondo uliyotoa:-

Fifteen years ago, tens of thousands of Catholics were hacked to death inside churches. Sometimes priests and nuns led the slaughter. Sometimes they did nothing while it progressed. The incidents were not isolated. Nyamata, Ntarama, Nyarubuye, Cyahinda, Nyange, and Saint Famille were just a few of the churches that were sites of massacres.

Hapa huoni hata hawa maaskofu wetu nao wanataka kutupeleka huko huko?

Na hii nimeitoa Wikipedia je unasemaje?

Though religious factors were not prominent (the event was ethnically motivated), the Human Rights Watch reported that a number of religious authorities in Rwanda, particularly Roman Catholic, failed to condemn the genocide at the time.[22] Some in its religious hierarchy have been brought to trial for their participation by the International Criminal Tribunal for Rwanda and convicted.[21] Bishop Misago was accused of corruption and complicity in the genocide, but he was cleared of all charges in 2000.[23] The majority of Rwandans, and Tutsis in particular, are Catholic, so shared religion did not prevent genocide.


Hebu tupe upeo wako wa ufahamu.
 
Uislamu ni dini ya kinafiki sana!...................kwani oic imefikia wapi?
 
First of all ukae ukilijua na wenzio walifahamu kuwa WAISLAMU NI WENGI KUSHINDA WAKRISTO TANZANIA na wamekuwa kimya muda mrefu sasa the sleeping giant is awakening my friend. Pili wakristo na waislamu ndio dini mbili kuu Tanzania wahindu na wengineo wanapercentage yao but wakichambuliwa hawafikiii wengi kama waislamu na wakristo sasa it is important for these two groups to reconcile.

Vile vile sitaki kuamini kwamba Mdondoji ni Mwislaam, maana kwa kufanya hivyo nitamaanisha Waislam wana uwezo kama wake katika kutafakari mambo,
 
Mimi natowa tamko la kuwalaani wote walioanzisha na kushadidia maandamano yaliyozuiliwa na polisi kufanyika.

Walaaniwe wote waliolazimisha ya fanyike na damu za hawa waliofariki ziwasute maisha yao yote.

we vp?kwani walioandamana walilazimishwa??
 
Sikujua kuwa hujui kuwa polisi hawana mamlaka ya kuzuia mikutano wala maandamanoya viumbe wowote achilia mbali ya vyama vya siasa kwa mujibu wa katiba na sheria za nchi hii ambazo zimetungwa kwa matakwa ya CCM. Nchi haiendeshwi kwa amri tena amri haramu, tuambieni polisi walpata wapi mamlaka ya kuzuia maandamano au mnashbikia wauaji kwa vile walouawa si wa chama chako? Kumbuka risasi hazikuchagua dini
Walaaniwe na damu ya waliokufa iwe juu yao. hivi wanajisikia aje kuona maandamano yalikatazwa wao wakalazisha watu waandamane badala ya kuwenda tu kuhudhuria mkutano. hivi hawa viongozi wa chadema wa dini kweli???? na je huwa wanaenda kusali????? na je wanajua kuwa bible inawataka kutii amri ya mamlaka kwani nisawa na amri ya mungu. je hao viongozi wanajua kwamba walishakubali matokeo na kumtambua raisi hivyo wanatakiwa kutii mamlaka yake.

Hivi wanakula na kulalal vizuri na familia zao kweli wakati wanajua kauli ya kulazimisha kuandama na kiburi chao cha kutotii mamlaka sababu ya uchu wa madaraka na kutafuta umaarufu ndivyo vimeleteleza watu kufa, kimsingi walitaka watu wafe ili wapate umaarufu nje ya nchi.
 
wajinga ndio wali wao huo! demokrasia inavunjwa wao wanalilia kikwete kutotakwa...
 
Tuache ushabiki usiokuwa na mbele wala nyuma! Kuna watu hapa jamii forums wao kazi yao ni kufuata mkumbo na kuchangia pasipo hata kufikiri. Hata kama ulijariwa akiri kidogo mno, zitumie hizohizo kuchambua mambo maana hayaitaji akiri nyingi, yako wazi mno! Mtu anayesema swala la udini awe kiongozi wa dini au muumini wa dini nadiriki kumshauri asome na kuvielewa vitabu vya dini yake kadiri ya imani yake alafu aangalie historia ya dunia! Katika historia ya dunia ni dhahiri kabisa kuwa wanasiasa pale wanaposhindwa kutawala huangalia ni sehemu ipi wanaweza kuegemea ili kuficha udhaifu wao. Mojawapo ya vitu wanavyoweza kuvitumia ni pamoja na kuwagawa watu kidini, kikabila, kikanda (regions) n.k. Kwa kuwa Tanzania si rahisi kuigawa kikabila na kikanda kwa jinsi ambavyo tumeingiliana ni dhahiri kabisa kuwa sasa wanasiasa wanatumia dhana ya dini kutugawa watanzania. Ieleweke kabisa kuwa kwa muumini yoyote yule anayeishi tanzania apime mwenendo na mafanikio ya viongozi yetu kisiasa hawezi kusema eti wakristu au waislam hawamtaki Kikwete! Anayesema haya ni mpuuzi na huenda akiri zake zina matatizo. Hakuna Mwislamu au Mkristu au mpagani anayefurahia mwenendo mzima wa uendeshaji nchi kwa sasa! Kama ni mfumuko wa bei sote unatugusa, kama ni kukaa gizani sote tunakaa gizani, kama ni suara la richmond/dowans sote tunahusika katika ulipaji, kama ni huduma mbaya za jamii sote tunahusika, kama ni mabomu na risasi hazichagui wewe ni mkristu au mwislam au mpagani! Ni dhahiri kabisa kuwa pale viongozi wa dini wanapokemea uovu kwa watawala istaafsiriwe kuwa ni udini! Kiongozi wa din anayeona binadamu anauwawa kwa kudai haki yake yake, na kwa kupigwa risasi hadharani akabeza na kushangilia, hafai kuwa kiongozi wa dini. Mojawapo ya majukumu ya viongozi wa dini ni kuhakikisha kuwa siku zote haki inatendeka ili amani iweze kupatikana, kama haki haipo amani haiwezi kuwepo.

Suara la kukemea uovu lisitafsiriwe kuwa ni udini na serikali ikalikumbatia! Mimi ninaishi na waislamu ni marafiki zangu, tunateseka wote pale mtaani kwangu, hatuna maji, umeme unakatika kila mara, hakuna barabara, hakuna hospitali, kula ni taabu! Iweje leo inapotokea viongozi wa dini wanapokemea uovu itafasriwe kuwa ni udini! Haijalishi anayekemea uovu serikalini ni kiongozi wa dhehebu gani, kila mtu kwa uwezo wake wa kuchambua mambo anayopicha halisi ya maisha ya mtanzania kuanzia nafsi yake mwenyewe na jamii inayomzunguka! Leo UDOM wamegoma kwa sababu ya ufinyu wa mawazo yetu tutasema wakristu hawamtaki Kikwete! TUCTA Wataandama tutasema wakristu hatumataki Kikwete! CHADEMA wameandama mnasema Wakristu hawamtaki Kikwete! Hivi huyu Kikwete alichaguliwa na nani kama si wewe, mimi na yule! (Mkristu, Mwislamu na Mpagani). Wekeni mambo ya dini pembeni ongelea hali halisi ya maisha unayoishi kuanzia ndani ya familia yako, jamii inayokuzunguka na taifa kiujumla then utapata jibu kuwa kweli kuna udini ama utawala umeshindwa kutawala na sasa unataka kuwagawa watanzania wamoja kwa kutumia dini. Kimsingi hili halikubaliki maana wote tunaumia!
 
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Arusha, kinatuhumiwa kuanza mchezo mchafu wa kuufanya mgogoro wa uchaguzi wa Meya wa jiji la Arusha uliosababisha vifo vya watu watatu, kuwa wa kidini.

Habari za uhakika kutoka ndani ya chama hicho, zimebainisha kuwa katika kufanikisha njama hiyo, baadhi ya viongozi wamefanikiwa kuwashawishi baadhi ya masheikh jijini Arusha, kutoa tamko la kulaani vurugu na kupinga kile wanachodai kuwa ni viongozi wa dini kujiingiza katika siasa.


Mpango wa kuwatumia baadhi ya Waislamu kuingilia mgogoro huo ulianza tangu juzi, siku moja baada ya umoja wa viongozi wa dini ya kikristo, kutoa tamko la kutomtambua Meya ya jiji hilo kwa tiketi ya CCM, Gaudence Lyimo.


Maaskofu hao pia waliaani kitendo cha polisi kutumia nguvu kubwa kupita kiasi kuvunja maandamano yaliyoandaliwa na Chadema kupinga mchakato wa uchaguzi huo.


Juzi jioni baadhi ya wanaCCM waonekana wakiwa kwenye harakati za kuwaalika waandishi wa habari kuhudhuria mkutano wa mashekhe uliofanyika jana mchana jijini Arusha, kulaani tamko la maaskofu.


"Kesho mashekh wanatoa tamko....Huu ni mgogoro wa kidini, maaskofu hawamtaki Kikwete ndio sababu wanampinga hadi Meya...Hali hii itatufikisha pabaya,"alisema kiongozi mmoja wa CCM (jina tunalo).


Kama ilivyodokezwa na viongozi hao wa CCM juzi, jana baadhi ya masheikh wa Msikiti Mkuu wa Arusha, waliitisha mkutano na waandishi wa habari na kutoa tamko la kulaani vurugu, ghasia na uvunjifu wa amani uliotokea wakati wa maandamano ya Chadema.


Katika tamko hilo ambalo nakala imesambazwa kwa jeshi la polisi, Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Usalama wa Taifa, Mkuu wa wilaya ya Arusha, Ofisi ya Mbunge wa Arusha Mjini, Ofisi ya Meya wa Arusha na Ofisi ya Mkurugenzi, lililosomwa na Imamu wa msikiti huo, Mohamed Hambali Waislamu hao walisema tukio hilo liliwaathiri sana.


"Tumeshindwa kufanya ibada zetu msikitini kwa amani na utulivu, uharibifu wa mali ikiwa pamoja na kuchomwa moto majengo, kutupiwa mawe msikitini na watoto na wazee kuathirika," inasomeka sehemu ya tamko hilo.


Tamko hilo, pia lilisomeka "Sisi viongozi wa dini ya Kiislamu tunawakumbusha wenzetu kwamba hatupaswi kuingilia maswala ya kisiasa kwa kutoa matamko ambayo yatapelekea uvunjifu wa amani."


Kauli hiyo, ambayo inaungana na kauli ya Katibu wa CCM mkoa wa Arusha, Mary Chatanda, aliyoitoa juzi, inaaminika kuwa ililenga kuwasema maaskofu ambao walitoa tamko la kutomtambua Meya wa CCM kutokana na kuchaguliwa bila kufuata utaratibu.


Tamko hilo, liliendelea kusema, " sisi viongozi tunatakiwa tuwe washauri wa kiroho na kusisitiza amani iliyopo. Ni vyema watu wakafuata kanuni na sheria za nchi kama inavyosomeka katika katiba ya nchi.


Taarifa hiyo, ilinukuu ibara ya 19(2) inayosomeka,"Kazi ya kutangaza dini kufanya ibada na kueneza dini itakuwa ni huru na jambo la hiari la mtu binafsi na shughuli za uendeshaji wa jumuiya za dini zitakuwa nje ya mamlaka ya nchi"


Tamko hilo la kwanza la aina yake kwa Waislamu wa Arusha ambao kwa miaka mingi wamekuwa na misuguano na serikali ilieleza kuwa, waislamu watatii mamlaka iliyochaguliwa kwa mujibu na kanuni za nchi.


"Tunatambua ibara 107(1) mamlaka yenye kauli ya mwisho ya utoaji haki katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, itakuwa ni Mahakama." ilisomeka taarifa hiyo.


Mwisho taarifa hiyo, ilitoa pole kwa wote walioathirika katika maandamano hayo yaliyofanyika juma iliyopita jiji Arusha ikiwamo familia za watu waliofariki dunia kwa kupigwa risasi za moto.


Hata hivyo mwenyekiti wa Kamati ya Msikiti Mkuu wa Arusha, Abdulaziz Mkindi, alikanusha tamko hilo kutolewa kwa shinikizo la CCM.


"Hili ni tamko letu sisi hatutumiwi na CCM wala serikali....Sisi waislamu wa Arusha Mjini tumeathirika sana na hizo vurugu na tunataka amani," alisema Mkindi ambaye alikuwa pamoja na Imamu Hambali.

SALAAM ALAEIKUM.Ndugu zangu waislamu wakati mwingine tusishabikie maswala kama ligi ya mpira. Inabidi tuwe analytical. Hivi tumesahau pale Askofu Polikapi Pengo alipomwambia Mkapa kuwa CCM ni kichaka cha majambaz???!!! Wakati Mkapa naye ni Mkristo!!Sasa hapo kulikuwa na udini gani hapo. Hivi kupanda kwa bei ya umeme na hali mbaya tunayoipata sasa hivi inawaathiri wakristo peke yao?? Hela ambazo serikali inataka kuipa DOWANS, hujui itawafaidia akina LOWASA,ROSTAM NA CHENGE?? Sasa hao mapapa watatu na wengine wanyonyaji wanadini hao?
Kama tusiposhikamana pmoja hawa mafisadi wataendelea kutugawa kusudi watunyonye na tubaki na chuki za kidini.
Mafisadi hawana dini,
 
:angel:Hivi nani wakulaumiwa kwa lililotokea Arusha
1.ni serikali iliyonyima watu wasiandamane bali wafanye mkutano ambao kwa maoni yangu ndo ungezungumza yale yalitaka kuzungumzwa,kwa utulivu na amani na bila kuvuruga hata shughuli za watu wengine????
2.Ni CHADEMA walioamua kwenda kinyume na tamko la serikali na polisi wakatumia fact kwamba wamekiuka taratibu na kwa hiyo wakatumia nguvu?
3.Ni polisi waliotumia nguvu kwa watu waliokiuka agizo la kutokuandamana?
4. Ni kosa kwa BAKWATA kukaa kimya au kuona kama wanavyoona wengine kuwa CHADEMA ilikosea kukiuka agizo la serikali?
5.Kuna haja gani ya kutafuta mchawi na kuacha kujadili hoja za msingi ambazo CHADEMA wanazidai ambazo zinatugusa watanzania wote kama DOWANS, suala la uchaguzi wa Meya na Katiba??????
6.Nani awajibishwe na ni namna gani ya kumwajibisha?
 
Back
Top Bottom