BAKWATA na Mauaji Arusha

BAKWATA na Mauaji Arusha

Dini zinafundisha kukubali ukweli na wewe ungekubali ukweli. Si ulinyamaza kimya hadi sasa?

Huyu fundi mchundo hawezi kukubali ukweli asilani, bcz ubongo wake ni wa kifuu,jaribu kusoma kwa makini post zake utaona, shortly wa kupuuzwa!
 
Mimi natowa tamko la kuwalaani wote walioanzisha na kushadidia maandamano yaliyozuiliwa na polisi kufanyika.

Walaaniwe wote waliolazimisha ya fanyike na damu za hawa waliofariki ziwasute maisha yao yote.

Walaaniwe na damu ya waliokufa iwe juu yao. hivi wanajisikia aje kuona maandamano yalikatazwa wao wakalazisha watu waandamane badala ya kuwenda tu kuhudhuria mkutano. hivi hawa viongozi wa chadema wa dini kweli???? na je huwa wanaenda kusali????? na je wanajua kuwa bible inawataka kutii amri ya mamlaka kwani nisawa na amri ya mungu. je hao viongozi wanajua kwamba walishakubali matokeo na kumtambua raisi hivyo wanatakiwa kutii mamlaka yake.

Hivi wanakula na kulalal vizuri na familia zao kweli wakati wanajua kauli ya kulazimisha kuandama na kiburi chao cha kutotii mamlaka sababu ya uchu wa madaraka na kutafuta umaarufu ndivyo vimeleteleza watu kufa, kimsingi walitaka watu wafe ili wapate umaarufu nje ya nchi.
 
Unataka kuniambia kuwa viongozi wa dini hawaruhusiwi kukemea uovu uliofanywa na vyombo vya Serikali, km Jeshi la Polisi, eti kwa hofu ya kuogopa kuchanganya dini vs siasa?
Ndugu zangu wana jamvi kwanza nasema HAPPY NEW YEAR japo nimechelewa kuwatakiwa mwaka mpya mwema, ninauhakika kabisa lilotokea Arusha limemkera hata Kikwete japo hasemi, mmoja wa watu waliokerwa ni Sitta ameamua kulipiza kwa kumkaanga Ngereja mchana kweupe,Kuhusu tamko la BKWATA wachangiaji baadhi yao haiwapasi kusema kidini badala ya kiukombozi wa nchi zaidi.
Dini zina watu na watu ni waserikali, kusema au kutosema kusiwe na hisia kuwa wanaugana na wajanja wajanja walosemwa na Sitta, kama Chatanda kwetu husema huyu ni mtanda wa nyama hana cha maana yoyote anapaswa achukuliwa hatua na Kanyaga twende, yaani vijana wenye uchungu na wafanyao mabaya kwa wenzao, wapige gari lake, hata kumfanyia umafia ajue kuwa juu ya jamii si kuwakandamiza bali kuwaheshimu sn watu.
Bakwata arusha ni kweli wameumia sn, kwani ni jambo lilomgusa kila mtu, kwahiyo jamvi lisilete mfarakano wa kidini bali liwe muunganiko wa mawazo kwa kulikomboa taifa letu kama mzee wetu Sitta alivysema jana kwenye Haabari leo ya Jumapili.
Nawshukuru sn kwa utulivu wenu.
Nawakilisha.
 
nani kakuongopea? "muislam ndugu yake muislam" kwa vyovyote tutaipinga bakwata lakini hatutoisaliti ni tofauti za kawaida si kwamba bakwata haitakiwi na waislam. alafu yalipofanyika mauwaji kule pemba hao wagala wa kwanza kupinga tamko waliongea nini?
au ndo mkuki kwa nguruwe?

l.o.l
 
Acheni jazba na matuzi ndugu zangu. Kila mtu anahaki ya kusema anachodhani ni sahihi. Si lazima aseme kama wewe. Kuwa mzima au mgonjwa yote ni mipango ya Mungu. Utaratibu bora na wakiungwana ni kuchambua hoja ya msemaji badala ya wajihi au sifa za msemaji. Maana wakati mwingine mlevu anaweza kusema ukweli na mtu mzima akasema uongo. Vile vile mwendawazima anaweza kusema neno bora kuliko mwenye akili timamu. Tuache personal attack bali to attack hoja kwa hoja.
 
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Arusha, kinatuhumiwa kuanza mchezo mchafu wa kuufanya mgogoro wa uchaguzi wa Meya wa jiji la Arusha uliosababisha vifo vya watu watatu, kuwa wa kidini.

Habari za uhakika kutoka ndani ya chama hicho, zimebainisha kuwa katika kufanikisha njama hiyo, baadhi ya viongozi wamefanikiwa kuwashawishi baadhi ya masheikh jijini Arusha, kutoa tamko la kulaani vurugu na kupinga kile wanachodai kuwa ni viongozi wa dini kujiingiza katika siasa.


Mpango wa kuwatumia baadhi ya Waislamu kuingilia mgogoro huo ulianza tangu juzi, siku moja baada ya umoja wa viongozi wa dini ya kikristo, kutoa tamko la kutomtambua Meya ya jiji hilo kwa tiketi ya CCM, Gaudence Lyimo.


Maaskofu hao pia waliaani kitendo cha polisi kutumia nguvu kubwa kupita kiasi kuvunja maandamano yaliyoandaliwa na Chadema kupinga mchakato wa uchaguzi huo.


Juzi jioni baadhi ya wanaCCM waonekana wakiwa kwenye harakati za kuwaalika waandishi wa habari kuhudhuria mkutano wa mashekhe uliofanyika jana mchana jijini Arusha, kulaani tamko la maaskofu.


"Kesho mashekh wanatoa tamko....Huu ni mgogoro wa kidini, maaskofu hawamtaki Kikwete ndio sababu wanampinga hadi Meya...Hali hii itatufikisha pabaya,"alisema kiongozi mmoja wa CCM (jina tunalo).


Kama ilivyodokezwa na viongozi hao wa CCM juzi, jana baadhi ya masheikh wa Msikiti Mkuu wa Arusha, waliitisha mkutano na waandishi wa habari na kutoa tamko la kulaani vurugu, ghasia na uvunjifu wa amani uliotokea wakati wa maandamano ya Chadema.


Katika tamko hilo ambalo nakala imesambazwa kwa jeshi la polisi, Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Usalama wa Taifa, Mkuu wa wilaya ya Arusha, Ofisi ya Mbunge wa Arusha Mjini, Ofisi ya Meya wa Arusha na Ofisi ya Mkurugenzi, lililosomwa na Imamu wa msikiti huo, Mohamed Hambali Waislamu hao walisema tukio hilo liliwaathiri sana.


"Tumeshindwa kufanya ibada zetu msikitini kwa amani na utulivu, uharibifu wa mali ikiwa pamoja na kuchomwa moto majengo, kutupiwa mawe msikitini na watoto na wazee kuathirika," inasomeka sehemu ya tamko hilo.


Tamko hilo, pia lilisomeka "Sisi viongozi wa dini ya Kiislamu tunawakumbusha wenzetu kwamba hatupaswi kuingilia maswala ya kisiasa kwa kutoa matamko ambayo yatapelekea uvunjifu wa amani."


Kauli hiyo, ambayo inaungana na kauli ya Katibu wa CCM mkoa wa Arusha, Mary Chatanda, aliyoitoa juzi, inaaminika kuwa ililenga kuwasema maaskofu ambao walitoa tamko la kutomtambua Meya wa CCM kutokana na kuchaguliwa bila kufuata utaratibu.


Tamko hilo, liliendelea kusema, " sisi viongozi tunatakiwa tuwe washauri wa kiroho na kusisitiza amani iliyopo. Ni vyema watu wakafuata kanuni na sheria za nchi kama inavyosomeka katika katiba ya nchi.


Taarifa hiyo, ilinukuu ibara ya 19(2) inayosomeka,"Kazi ya kutangaza dini kufanya ibada na kueneza dini itakuwa ni huru na jambo la hiari la mtu binafsi na shughuli za uendeshaji wa jumuiya za dini zitakuwa nje ya mamlaka ya nchi"


Tamko hilo la kwanza la aina yake kwa Waislamu wa Arusha ambao kwa miaka mingi wamekuwa na misuguano na serikali ilieleza kuwa, waislamu watatii mamlaka iliyochaguliwa kwa mujibu na kanuni za nchi.


"Tunatambua ibara 107(1) mamlaka yenye kauli ya mwisho ya utoaji haki katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, itakuwa ni Mahakama." ilisomeka taarifa hiyo.


Mwisho taarifa hiyo, ilitoa pole kwa wote walioathirika katika maandamano hayo yaliyofanyika juma iliyopita jiji Arusha ikiwamo familia za watu waliofariki dunia kwa kupigwa risasi za moto.


Hata hivyo mwenyekiti wa Kamati ya Msikiti Mkuu wa Arusha, Abdulaziz Mkindi, alikanusha tamko hilo kutolewa kwa shinikizo la CCM.


"Hili ni tamko letu sisi hatutumiwi na CCM wala serikali....Sisi waislamu wa Arusha Mjini tumeathirika sana na hizo vurugu na tunataka amani," alisema Mkindi ambaye alikuwa pamoja na Imamu Hambali.
 
Wana siri ya pamoja, lengo likiwa ni kuhakikisha wanashika nchi ili kanisa liendelee kushika hatamu na UTAMU wa nchi hii. JK kawanyang'anya utamu kupitia MoU kati ya kanisa na serikali. JK alitaka awanyime utamu baada ya mwaka jana kutaka mali zinazoingizwa na makanisa nchini zilipiwe kodi. Leo wanasema hawamtambui Meya Arusha kisa mauaji. Mbona hawakumtambua Rais baada ya mauaji ya januari 21 ambapo watu 27 waliuawa na wanawake kubakwa. AU NI SIASA ZA UZANDIKI?
 
KAUMZA....kuna tafsiri tatu juu ya wewe na ujumbe wako huu.

1. Wewe ni fisadi au unafaidi matunda ya ufisadi unaotekelezwa na CCM
2. Wewe unaweza kuwa na tatizo la kusoma, kuelewa, kufikiri na kuoanisha mambo
3. Wewe ni mdini na udini wako umeuweka wazi bila kificho.

Therefore, without hesitation, I call this a MALEVOLENCE
 
Jamani udini huko wapi hapa!!! Aliyekataliwa kutambuliwa na maaskofu ni mkristo wala sio muislamu. Je angekuwa ni muislamu ingekuwaje???? Ni wapi maaskofu wa Arusha wametamka kwamba hawamtaki Kikwete kwa kuwa ni muislamu? Huu ni ujinga uliokithiri na kujaribu kutafuta mchawi wakati ukweli unajulikana!!! Hawa wanasahau kwamba ni kanisa hilo hilo liliowahi kutamka kwamba Kikwete ni chaguo la Mungu? Mbona waislamu hawakuipinga hiyo kauli? This sounds like cheap politics to me!!!

Tiba
 
Dini yeyote yenye kutaka kumkingia kifua kiongozi dhaifu, eti kwasababu ni muumini wake, ni dini isiyotoka kwa Mungu. Ni dini mfilisi na siwezi kupoteza muda wangu kujifunza inachofunza.

Kikwete ni dhaifu, na madhara ya madhaifu yake yanampata kila mtu na dini yake. Waliokingiwa madhara ya udhaifu wake ni marafiki zake, wanamtandao na hao ni wa dini zote. Baadhi ya watu wanaofaidika ni pamoja na wale wanaokuja kupiga debe hapa JF. Orodha yao inazidi kuongezeka kadiri kashfa za Kikwete zinavoongezeka na kuhitaji watetezi.

Ipo siku ambayo haihitaji mpiga debe, ukweli utachambuliwa kama karanga na kila mtu atavuna aibu ya misimamo yake ya kipuuzi au furaha yake kwa kusimamia hoja za msingi na mstakabali wa watu na nchi yetu.

Mungu ametupatia nchi, kisha akatuagiza tuilinde na kuitunza. Hatuwezi kuilinda nchi yetu kwa kuruhusu wabakaji waendelee kubaka kadiri ya wanavyotaka na sisi tukaendelea kuwatizama tu.

Mimi baba yangu ni kiongozi mkubwa huko msikitini kwao, na mjomba wangu ni askofu mkubwa huko kanisani kwao, lakini inanisaidia nini mimi kama nchi yangu inaibiwa na ninakaa gizani na baba na mjomba wangu? Upuuzi watuondolee huko....

Viongozi wetu wasipoangalia saa ya kupingana kwa maneno inakwisha na muda wa kupigana kwa vitendo inakimbia kuja... ole wenu mnaocheza na amani iliyojengwa...

akha! ...........
,,,,,,,,,
 
Jamani udini huko wapi hapa!!! Aliyekataliwa kutambuliwa na maaskofu ni mkristo wala sio muislamu. Je angekuwa ni muislamu ingekuwaje???? Ni wapi maaskofu wa Arusha wametamka kwamba hawamtaki Kikwete kwa kuwa ni muislamu? Huu ni ujinga uliokithiri na kujaribu kutafuta mchawi wakati ukweli unajulikana!!! Hawa wanasahau kwamba ni kanisa hilo hilo liliowahi kutamka kwamba Kikwete ni chaguo la Mungu? Mbona waislamu hawakuipinga hiyo kauli? This sounds like cheap politics to me!!!

Tiba

Mijitu yenye fikra fupi inatuhangaisha siku zote ...nchi hii ni nchi nzuri lakini kuna aina ya watu wanataka kutuharibia nchi yetu ...hao naomba walaaniwe wote, na kila mpenda amani aseme ... amina.
 
KAUMZA....kuna tafsiri tatu juu ya wewe na ujumbe wako huu.

1. Wewe ni fisadi au unafaidi matunda ya ufisadi unaotekelezwa na CCM
2. Wewe unaweza kuwa na tatizo la kusoma, kuelewa, kufikiri na kuoanisha mambo
3. Wewe ni mdini na udini wako umeuweka wazi bila kificho.

Therefore, without hesitation, I call this a MALEVOLENCE

Amani Katoshi: Labda nimesahau. Hivi kanisa lilitoa tamko baada ya mauaji ya wana CUF? Hivi kulisema kanisa ni Udini? Nikisema kanisa lilishiriki katika mauaji ya kimbari Rwanda(Vatican wamekiri na kuomba msamaha) nitaitwa pia mdini? Na wapi nimeshindwa kuoanisha mambo? Je CUF hawakuuawa kwa sababu ya maandamano ya kupinga matokeo ya uchaguzi kama CDM walivyouawa Arusha?
 
Wana siri ya pamoja, lengo likiwa ni kuhakikisha wanashika nchi ili kanisa liendelee kushika hatamu na UTAMU wa nchi hii. JK kawanyang'anya utamu kupitia MoU kati ya kanisa na serikali. JK alitaka awanyime utamu baada ya mwaka jana kutaka mali zinazoingizwa na makanisa nchini zilipiwe kodi. Leo wanasema hawamtambui Meya Arusha kisa mauaji. Mbona hawakumtambua Rais baada ya mauaji ya januari 21 ambapo watu 27 waliuawa na wanawake kubakwa. AU NI SIASA ZA UZANDIKI?

Huu ni upupu!!! Wewe unaishi dunia gani aisee? Huoni aibu kuleta bandiko kama hili hapa? Wewe ni mdini na udini hatutakaa tuupe nafasi Tanzania kwani udini ni sumu kupita kiasi. Kupanda mbegu za udini ni kuyatafuta yale yaliyotokea Rwanda kati ya Wahutu na Watutsi ila sisi hapa itakuwa ni kati wa wakristo na waislamu. Ng'oa hii mbegu mbaya ya udini kutoka kwenye jamii ya Watanzania kwani ni hatari na mbaya kuliko ukoma!!! Wewe unasema hayo na umesahau kwamba meya wa Arusha aliyekataliwa na viongozi wa dini ya kikiristo ni mkristo mwenzao vipi angekuwa ni muislamu hapo tena si ingekuwa ni balaa? Umepewa akili itumie kuchambua mambo na wala usije hapa kuweka mabandiko kwa ajili ya kuwafurahisha waliokutuma!!!!

Tiba
 
Huu ni upupu!!! Wewe unaishi dunia gani aisee? Huoni aibu kuleta bandiko kama hili hapa? Wewe ni mdini na udini hatutakaa tuupe nafasi Tanzania kwani udini ni sumu kupita kiasi. Kupanda mbegu za udini ni kuyatafuta yale yaliyotokea Rwanda kati ya Wahutu na Watutsi ila sisi hapa itakuwa ni kati wa wakristo na waislamu. Ng'oa hii mbegu mbaya ya udini kutoka kwenye jamii ya Watanzania kwani ni hatari na mbaya kuliko ukoma!!! Wewe unasema hayo na umesahau kwamba meya wa Arusha aliyekataliwa na viongozi wa dini ya kikiristo ni mkristo mwenzao vipi angekuwa ni muislamu hapo tena si ingekuwa ni balaa? Umepewa akili itumie kuchambua mambo na wala usije hapa kuweka mabandiko kwa ajili ya kuwafurahisha waliokutuma!!!!

Nani ali-engineer mauaji ya Rwanda? Kumkataa meya wa Arusha ni kama adhabu kwa wote walio/wanaom-support JK. Ukweli unabaki palepale, KANISA lina hisa na CDM. Udini wangu uko wapi? Tusikariri kwamba kila anaekosoa dini fulani ni mdini. Hata Padri Karugendo huwa anakosoa mwenendo wa kanisa. Naye ni mdini? Umepewa akili ufikiri, FIKIRI SASA
 
Mimi siwezi kuita mawazo yako upupu lakini ni wazi kuwa mawazo yako yamepitwa na wakati.
1. Tanzania hakuna udini na udini unataka kuletwa na wana siasa hasa CCM kwa lengo la kumpiga vita Dr. Slaa kwasababu aliwahi kuwa padre wa katoliki.
2. Agenda hii ya udini ambao haupo utaiangusha CCM huko mbele, kwani huwezi kutukana watu wa dini moja wakati unawahitaji kwenye chama na ni wanachama wengi.
3. CUF ni kweli hawajasema lakini ni muda umepita na kuna mwamko sana Tanzania. Tanzania ya sasa si ya miaka 10 au mitano iliyopita. Hiki ni kitu watu wengi walio madarakani bado inawachukuwa muda kuelewa. Tanzania imebadilika na hairudi nyuma. watu wamechoka na umasikini na kikubwa kinachowasibu ni ufisadi unaofanywa na wana siasa wa kusaini mikataba mibovu. Waliosini hii mikataba ni CCM hivyo ni lazima ilalamikiwe.
Kwa wana CCM dawa ya upinzani si polisi, malalamishi wala udini bali ni maendeleo tu. Bila maendeleo yanayo onekana wananchi watawatoa wadarakani siku moja. kanda nzima ya kaskazini na ya ziwa iko kwenye huu mwamko. Ukitoa Tanga mikoa yote ya Kagera, Mwanza, Shinyanga, Mara, Arusha, Manyara na Kilimanjaro inabadilika na huwezi kuwadanganyishia watu na dini kwani Watanzania hata kwenye familia kuna dini tofauti!. Makanisa hayana utamu wowote Tanzania kwani wenyewe ndiyo wanasaidia nchi hasa vijijini kuanzia shule hadi Hospitali. Miji mingi Tanzania imeanzishwa kwasababu ya juhudi za kimaendeleo ya Kanisa. Hivyo ndugu yangu unatatizo moja tu mawazo yako yamepitwa na wakati!
 
This was bound to happen, Maaskofu walipoingilia siasa na kutoa such a statement it was totally wrong. This statement if it was made by a group of people wether affiliated with political parties or not, this would have been OK!

NOW ITS THE TIME TO STOP RELIGIOUS LEADERS FROM MAKING POLITICAL STATEMENTS THAT CAN DIVIDE US BEFORE ITS TOO LATE OR WE ARE BOUND TO START KILLING EACH OTHER !!!!
 
Back
Top Bottom