BAKWATA na Mauaji Arusha

Si busara kuwalaumu bakwata kwa sasa, nadhani wanawasiliana na arusha ili watoe taarifa yenye uzito na usahihi. Ni busara tusuburi tafakuri zao. Nadhani niwape angalizo, wasije wakajipa upange, wajiweke kwenye jamii
 
kuna vitu vinaitwa MALENGO na MKAKATI_lengo la wanaharakati wote kwasasa nikuona kunakuwa na Mabadiliko ya Kiutawala_mambo mengine yote ni Mikakati_hali kadhalika tuandikapo Posts huwa ni Mikakati kwa ajili ya mambo fulan tunayoyalenga_ni vema kufikiri sana kabla hujafanya jambo_kwa post hii nadhan umetuma wakati ukijisaidia choon_haimsaidii yeyote hata familia yako hainufaiki kwa post hii_otherwise mnatukatisha tamaa waislam tuliomo chadema kwamba inawezekana chadema ni ukiristo na sisi tunawasindikiza kwenye move zenu_kwann harakat za kisiasa zizungumzie iman wakat wanaharakat ni wenye iman tofaut na tunaunganishwa na MALENGO? Hii inanitia shaka na kunifanya niamin kuwa inawezekana mh. Zitto yupo sahih kuwa kuna udin ndan ya cdm_nimekuwa kwa muda mrefu nikikemea mambo haya na kuwaomba mods kupinga vitu_lakin posts zinazofutwa ni zile zinazokemea mambo haya ndizo hufutwa


Usipoangalia unakaribia kupata ugonjwa unaowapata wengi wanaothamini dini kuliko haki unaoitwa fikramgandoosis. Unajua mission ya dini yoyote duniani? unapoona haki inakiukwa ni wajibu wa wapenda haki wote kukemea. kumbuka leo kwa mwenzio, kesho kwako. hakuna binadamu mwenye akili timamu awezaye kukaribisha hali hatarishi ya maisha ya viumbe wenye thamani kupita wote duniani-Binaadamu. Ni jukumu siyo la wapenda haki tu, bali la watanzania wote kulaani matumizi ya nguvu katika shughuli halali zenye haki za kikatiba ili kuilinda katiba yetu pamoja na mapungufu yake. Hapa natarajia hata viongozi wa serikali kulaani tabia za namna hii. hujasoma magazeti leo kwamba hata Rais Kikwete amesoneshwa na kilichotokea arusha na kuahidi kuwa hakitatokea tena? Hivi unadhani ni kwa nini serikali imefikia kuomba meza ya mazungumzo na wawakilishi wa wananchi-cdm kwa tukio la arusha? THINK THINK THINK kabla hujamwaga mawazo yako janvini
 
Usipoangalia unakaribia kupata ugonjwa unaowapata wengi wanaothamini dini kuliko haki unaoitwa fikramgandoosis. Unajua mission ya dini yoyote duniani? unapoona haki inakiukwa ni wajibu wa wapenda haki wote kukemea. kumbuka leo kwa mwenzio, kesho kwako. hakuna binadamu mwenye akili timamu awezaye kukaribisha hali hatarishi ya maisha ya viumbe wenye thamani kupita wote duniani-Binaadamu. Ni jukumu siyo la wapenda haki tu, bali la watanzania wote kulaani matumizi ya nguvu katika shughuli halali zenye haki za kikatiba ili kuilinda katiba yetu pamoja na mapungufu yake. Hapa natarajia hata viongozi wa serikali kulaani tabia za namna hii. hujasoma magazeti leo kwamba hata Rais Kikwete amesoneshwa na kilichotokea arusha na kuahidi kuwa hakitatokea tena? Hivi unadhani ni kwa nini serikali imefikia kuomba meza ya mazungumzo na wawakilishi wa wananchi-cdm kwa tukio la arusha? THINK THINK THINK kabla hujamwaga mawazo yako janvini

we b.w.e.g.e badala ya kumrekebisha mtuma post .
 
Habari ya mwembechai ilikuwa na maslahi kwa kundi moja katika jamii, habari ya Arusha ina maslahi kwa taifa zima

Mtu yoyote kuwawa sio kitu cha kufurahisha ispokua ni lazima tukubali mazingira aliyouwawa mtu yana mchango mkubwa ktk kufikia uamuzi kua aliuwawa kimakosa au hapana. Sidhani kua ni hekima kusema kua mauaji ya muembe chai yalikua ni halali kwa kua wale watu walipigania maslahi binafsi na maandamano ya juzi yalikua na maslahi kwa taifa zima.

Ni muhimu kua na utaratibu ktk ufanyaji wa mambo na ni lazima utaratibu ufuate, Ninafikiri kua maandamano yalizuiwa na serikali kwa sababu zinazohusiana na uslama, sasa kama kituo cha polisi kilitiwa moto na watu wengine walitaka kuwatoa watu ktk kituo cha polisi kwa nguvu. yoyote anaweza kuona kua hiyo haikukaa sawa.

Mpaka sasa tunapata sana information za upande mmoja ule unaolaumu kua umefanyiwa dhuluma, tusubiri serikali nayo itoe maelezo kua kwanini hali ilikua vile au mazingira gani yalipelekea ile hali kutokea.

Wengi hawaoni kua kuna change yoyote kubwa inayoweza kufanyika hasa ukizingatia ni juzi tu tumemaliza uchaguzi.
 
Mtu yoyote kuwawa sio kitu cha kufurahisha ispokua ni lazima tukubali mazingira aliyouwawa mtu yana mchango mkubwa ktk kufikia uamuzi kua aliuwawa kimakosa au hapana. Sidhani kua ni hekima kusema kua mauaji ya muembe chai yalikua ni halali kwa kua wale watu walipigania maslahi binafsi na maandamano ya juzi yalikua na maslahi kwa taifa zima.

Ni muhimu kua na utaratibu ktk ufanyaji wa mambo na ni lazima utaratibu ufuate, Ninafikiri kua maandamano yalizuiwa na serikali kwa sababu zinazohusiana na uslama, sasa kama kituo cha polisi kilitiwa moto na watu wengine walitaka kuwatoa watu ktk kituo cha polisi kwa nguvu. yoyote anaweza kuona kua hiyo haikukaa sawa.

Mpaka sasa tunapata sana information za upande mmoja ule unaolaumu kua umefanyiwa dhuluma, tusubiri serikali nayo itoe maelezo kua kwanini hali ilikua vile au mazingira gani yalipelekea ile hali kutokea.

Wengi hawaoni kua kuna change yoyote kubwa inayoweza kufanyika hasa ukizingatia ni juzi tu tumemaliza uchaguzi.

Sijasema mauaji ya Mwembechai yalikuwa halali. Nilikuwa namjibu mchangiaje anayeshangaa kwa nini maaskofu hawakulaani mauaji yale. Ndio maana nikasema, yale ya Mwembe yalihusu kundi moja ambalo linakinzana na maaskofu sasa wasingeweza kulitolea tamko. Kwanza waislamu walianza kuwakashifu hao maaskofu hivyo kuondoa uwezekano wa maaskofu 'ku-sympathise' nao. Hili la Arusha halina msingi wa dini yoyote na hivyo maaskofu ktk neutrality yao wametoa tamko kulaani, na hata Bakwata naamini wako njiani kutoa tamko kwa sababu kipenzi chao (Lipumba) ameshafanya hivyo.
 
BAKWATA ni chombo ya WAGALA ambao wako Serikalini

pia msisahau kuwa BAKWATA iliunda na Serikali

majority ya waislam hawaitambui

In otherwords Bakwata is just one of many organisations kama vile Baraza kuu, Shura ya Maimam, SUPTAM na wengineo sema BAKWATA wanaenjoy kupewa niceties na serikali

And dont get me started on Sheikh Mkuu wa BAKWATA wa DSM....


I means seriously Bakwata inaongozwa na mtu iliterate halafu mnataka muone Tamko lao?


Hivi mnawa rate so high hawa jamaa?

nani kakuongopea? "muislam ndugu yake muislam" kwa vyovyote tutaipinga bakwata lakini hatutoisaliti ni tofauti za kawaida si kwamba bakwata haitakiwi na waislam. alafu yalipofanyika mauwaji kule pemba hao wagala wa kwanza kupinga tamko waliongea nini?
au ndo mkuki kwa nguruwe?
 
Muda bado upo kwa bakwata kutoa msimamo wao. Pia ianwezekana walishatoa lakini kwakuwa hawana redio wala gazeti ndio maana hamjawasikia. Pia inawezekana wameona ni busara zaidi kukaa kimya kwa kuwa hawana taarifa ya kutosha kuhusiana na vurugu hizo. Kama kuna wengine walihojiwa na kutoa misimamo yao, yeyote kati yetu anaweza kufanya appointment na viongozi wa bakwata akaenda kumhoji kujua mtizamo wao katika suala hili.

Kusema kwamba bakwata wanajali oic tu ni kauli ambazo zinaweza kutonesha hisia za kidini na kuleta tofauti kati ya wanachama wa jamii forum na wanachi wengine bila sababu.
 
Mimi natowa tamko la kuwalaani wote walioanzisha na kushadidia maandamano yaliyozuiliwa na polisi kufanyika.

Walaaniwe wote waliolazimisha ya fanyike na damu za hawa waliofariki ziwasute maisha yao yote.


Wewe ni nani? Swali limeuza Bakwata! nadhani husitumie uhuru wa kutoa maoni humu kutoa ushabiki wa mpira katika mambo ya msingi; kwanza hata hujui mstakabali wa Tanzania ni bora ukae kimya kwa mambo husiyo yajua; tulipo sema katiba nyinyi ndio kunguru wa awali kuimba kwamba sio tatizo leo Dunia nzima inakiri ni tatizo kubwa sana, si kila matatizo katika jamii yanashugurikiwa na jamii nzima tunajua katika yoyote kuna watu wa aina tatu, MOJA Shujaa ambao wao kwa Tanzania wamekuwa mstari wa mbele kudai haki na maslahi sawa kwa Watanzania tokea enzi za Mkoloni, wanakufa na kuzaliwa wengine kila siku na wanaendele kudai haki za watanzania kila siku, katika kundi hilo wamo Watanzania wengi na kwa sasa wengi wamejiunga kudai haki hizo kupia CDM, PILI waoga ambao wanayajua matatizo hawayataki wanayachukia lakini ni waoga kushiriki katika vuguvugu la kudai haki kwa kuogopa kupoteza maisha, vyeo, na riziki wanayopewa kutoka kundi la wanyaji, katika kundi hili mfano mzuri ni Spika Sitta na wanyonge wengine wengi ambao wapo serikali na vijijini, najua wapo Majeshini na katika vyombo vya Usalama vyote na Rais wako anajua na chama chako kinajua, hili kundi ni kubwa kwa sasa ndio maana kikwete anapata taabu, kundi hili ni muhimu kwa maana hawa wanapokomaa na kuamua uwa kundi la kwanza la uendelea kuishi katika kundi hiliTATU Punguani ambao wao hawajui lolote wala chochote kinachoendele kila kitu kwao ni sawa, kundi hili hawana cha kulaumiwa bahati mabaya wamezaliwa hivyo na watakufa hivyo hivyo, sitaogopa hasilani kukwambia wewe ni hili kundi la tatu hamna tofauti yako na ombaomba walioko BibiTiti/Moromoro rd kama unabisha taja jina lako halisi naujitokeze hadharani tukakupime akili!
 
Hivi KKT nao walilaani maiuaji ya MWEMBECHAI?

Sijasema mauaji ya Mwembechai yalikuwa halali. Nilikuwa namjibu mchangiaje anayeshangaa kwa nini maaskofu hawakulaani mauaji yale. Ndio maana nikasema, yale ya Mwembe yalihusu kundi moja ambalo linakinzana na maaskofu sasa wasingeweza kulitolea tamko. Kwanza waislamu walianza kuwakashifu hao maaskofu hivyo kuondoa uwezekano wa maaskofu 'ku-sympathise' nao. Hili la Arusha halina msingi wa dini yoyote na hivyo maaskofu ktk neutrality yao wametoa tamko kulaani, na hata Bakwata naamini wako njiani kutoa tamko kwa sababu kipenzi chao (Lipumba) ameshafanya hivyo
 
Kanisa heri linyamaze na kufunga mdomo maana kila nikikumbuka mauaji ya kimbari Rwanda huwa nasikitika sana Kanisa linapoongelea juu ya haki! kila nikikumbuka mauaji ya Mwembechai Dar, na kauli alieitoa Padri Lwambano kuwa Serikali iwashugulikie Waislamu wa Msikiti wa Mwembechai na siku ya pili Polisi waliitikia wito huo na kuuwa wananchi wenzetu! nasikitika tena Kanisa kuhubiri haki!

Kila nikikumbuka mauaji ya raia huko visiwani na kauli ya Muadhama Kardinali Pengo kuwa waliouliwa na Polisi huko Zenji ndio wabebe lawama kwa kutokutii amri ya Serikali ya kutokuandamana!!

Sasa, leo Kanisa na Baraza la Maaskofu watakuwa na ubavu gani wa kujitokeza na kulaani mauaji ya Arusha?

Kuna watu wengine wapumbavu watakao fikiri kuwa mimi nafurahia mauaji ya Arusha lakini kwa hakika kila binaadamu mwenye hisia hatafurahia kitendo hicho cha Askari wetu kufyatua risasi za moto na kuua wananchi! ni tendo la kulaaniwa lakini sio Maaskofu wajitokeze leo ghafla na kutoa kilio cha kinafiki! kwanza waombe msamaha kwa maovu waliofanya huko nyuma kwa kuunga mkono maamuzi ya Serikali ya Benjamin Mkapa ya kuuwa raia wa nchi hii na ndipo wafungue ukurasa mpya wa kudai haki za wananchi kinyume chake itakuwa vigumu kuelewa lengo la Kanisa ni nini!

BAKWATA si chombo halali cha waislamu wala chombo hiki hakina ridhaa ya Waislamu bali Serikali inaibeba kwa amri ya Mwalimu Nyerere ambae kwa hakika ndie alie asisi mwaka 1968 huko Iringa baada ya kuvunja jumuiya ya Waislamu ya EAMWAS! ambayo iliwaletea Waislamu maendeleo makubwa na kutaka kujenga chuo kikuu cha kiislamu cha Afrika Mashariki ndipo Nyerere akafikia uamuzi huo wa kuivunjilia mbali! soma: Mwembechai Killings

Hivyo BAKWATA walaani au wasilaani hiyo sio issue kwa Waislamu bali Waislamu wanajumuiya zao zinazowakilisha maslahi yao na kama kutoa kauli basi ni viongozi wao ndio watatoa lakini sio BAKWATA!

nadhani kuna mantiki kubwa katika uliyoyasema kaka. Niko pamoja nawe.
Pengine tujiulize; MBONA MAASKOFU HAWAKUTOA MATAMKO JUU YA WANACHADEMA WALIPOUA PALE MASWA?? AU ILE DAMU ILIKUWA MAJI?? NAONA DAMU ILE YA YULE JAMAA ALIYEUAWA PALE MASWA NDIYO IMEWAFUATA CHADEMA. MTENDA HUTENDWA!
naliyasema haya ndani ya JF ila kwa sababu ya mihemuko watu wakaniona mpuuzi. Kuna mtu mmoja anajiita "Josephine" akanitukana sana nikasema haya. ukisema nasapoti juu yako lakini ukweli umetimia. asiyesikia la mkuu kichwa hupigwa ngeu.

 
Cityboy hebu rudi tena.....Maaskofu wana ubia na CDM au wana 'memorandum of understanding' na serikali kama mlivyokuwa mnadai hapo awali?

Ndio serikali ina MOU na kanisa.MOU uliingiwa wakati wa mkapa na kanisa lilikua na sauti kuu juu ya serikali.Soma fact za Kadogoo hapo juu.Wakati huu wakristo na matamko ya kilaleo ili tu nafasi irudi huku wakitafuta mbadala ambao ni kupitia cdm.Tazama humo cdm kulivyo na udini,tena ukatoliki ukiwa zaidi ya waunga mkono wengine.Kanisa lina hangaikia nguvu za kuuangamiza uislam na JK amewasoma ndo maana mwaka2010 hakua chaguo la Mungu tena kwani mlivyoni ni wa kuburuza tu sivyo!Kampeni zenu tunazijua A to Z upo hapo?
 
Ndio serikali ina MOU na kanisa.MOU uliingiwa wakati wa mkapa na kanisa lilikua na sauti kuu juu ya serikali.Soma fact za Kadogoo hapo juu.Wakati huu wakristo na matamko ya kilaleo ili tu nafasi irudi huku wakitafuta mbadala ambao ni kupitia cdm.Tazama humo cdm kulivyo na udini,tena ukatoliki ukiwa zaidi ya waunga mkono wengine.Kanisa lina hangaikia nguvu za kuuangamiza uislam na JK amewasoma ndo maana mwaka2010 hakua chaguo la Mungu tena kwani mlivyoni ni wa kuburuza tu sivyo!Kampeni zenu tunazijua A to Z upo hapo?

Kwa hiyo MoU ukomo wake ilikuwa ni 2010?
 
Unataka kuniambia kuwa viongozi wa dini hawaruhusiwi kukemea uovu uliofanywa na vyombo vya Serikali, km Jeshi la Polisi, eti kwa hofu ya kuogopa kuchanganya dini vs siasa?

Rejea tamko la kanisa juu ya mauaji ya Zanzibar.Kama unakumbukumbu naomba unijibu. Zanzibar walokufa ni waislam.Kanisa na cdm lao moja! Upo?
 
Back
Top Bottom