BAKWATA na Mauaji Arusha

BAKWATA na Mauaji Arusha

Udini ni kichaka cha kuficha udhaifu wote. Jk analaumiwa kutokana na kushindwa kuongoza nchi. Hachukiwi kwa sababu ya uislam wake.
tuko pamoja kwa hili mkuu, udini una letwa ili watuondoe kwenye hoja na watugawe..siku ya maandamano walikuwepo masheikh na maaskofu waliombea mkutano yote hiyo iliimanisha kulikuwa na dini zote..
 
This was bound to happen, Maaskofu walipoingilia siasa na kutoa such a statement it was totally wrong. This statement if it was made by a group of people wether affiliated with political parties or not, this would have been OK!

NOW ITS THE TIME TO STOP RELIGIOUS LEADERS TO MAKE POLITICAL STATEMENTS BEFORE ITS TOO LATE OR WE ARE BOUND TO START KILLING EACH OTHER !!!!

Mapambano,
I dare to call you Mapambano a.k.a. Makamba!
You seems to be one of those CCM hooligans who are still day dreaming about Single Party ruling which is now a history!
Please wake up now and witness the move of changes prevailing now in Tanzania.

Lazima ujue kuwa swala la mgogoro wa Umeya wa Arusha halina uhusiano wa kidini hata chembe. Wanaotaka kuingiza udini ni mambumbu na malimbukeni WALIOFILISIKA KISIASA na ambao kwao CCM kushindwa kwenye Uchaguzi ni kitu kisichowezakana!!! Huu ni upuuzi na upambaf ambao hatuwezi kuukubali.

Ujue tu kwamba Maaskofu kuzungumzia swala la MAUAJI YA ARUSHA ni haki yao kikatiba wakiwa ni sehemu ya jamii au umma wa Watanzania.
Hivi unataka kutuaminisha kuwa Askofu au Padre akizungumzia mstakabali wa Amani,Upendo na Mshikamano ndani ya Tanzania ni dhambi? CCM lazima mjue kuwa Viongozi wa kidini ni sehemu ya Jamii ya Watanzania ambao wana uhuru wa kutoa mawazo yao kuhusu mwelekeo wa Siasa za nchi hii. Wao ni viongozi wa kiroho wa haohao Wanasiasa wanaowabeza kwa sasa.

Acheni upuuzi wenu wa kupayuka na kuropoka kama vile mmekunywa denge au gongo. Kauli za Makamba na Mary Chatanda kuwa Uchaguzi wa Meya Arusha hautarudiwa na kwamba Maaskofu wanaotaka siasa WAVUE MAJOHO WAINGIA KWENYE SIASA NI MATUSI KWA VIONGOZI WA DINI.

Nimeshasema MAKAMBA ANA MTINDIO WA UBONGO,NI BORA CCM WAKAMPELEKA MIREMBE MENTAL HOSPITAL AKACHUNGUZWE AKILI ZAKE MAANA ANAONEKANA KUHATARISHA MSTAKABALI WA CCM. Kama Waziri wa Mambo ya Ndani amekubali kuna tatizo kwenye swala la Umeya kwanini MAKAMBA akatae kuwa hakuna tatizo na CHADEMA waende mahakamani? Hakika huyu Makamba ni HATARI, Makamba ni MNAFIKI,MWONGO,MPAYUKAJI,MZUSHI NA KIZABIZABINA! Ni UWENDAWAZIMU kusema kuwa Uchaguzi wa Meya Jiji la Arusha ulikuwa Huru na Haki ilhali MADIWANI WA CHADEMA hawakuwepo kwenye Uchaguzi huo ukizingatia kuwa CHADEMA ndiye MWAKILISHI WA WANANCHI WA JIJI LA ARUSHA kwenye Bunge la JMT.

Akili na Utashi wa kawaida kabisa kwa mtu mwenye AKILI TIMAMU ATAONA KUWA UCHAGUZI WA MEYA ARUSHA ULIKIUKA MISINGI NA TARATIBU MUHIMU KABISA ZILIZO WAZI. CCM WALITUMIA MAMLUKI KUTOKA TANGA KWA JINA LA MARY CHATANDA AKIJIFANYA NI DIWANI WA ARUSHA MJINI WAKTI SI KWELI. JE,HIVI CHADEMA NA WAO WANGEAMUA KULETA MADIWANI KUTOKA NJE YA ARUSHA WAKAIPIGIA KURA CHADEMA,CCM MNGEKUBALI????

Kuna watu wachache CCM wenye hekima angalao kidogo. Tumeona LOWASA akilonga mapema sana hata KABLA YA MAUAJI YA ARUSHA KUWA UMEYA ARUSHA NI TATIZO UNAWEZA KUPELEKEA IVORY COST NYINGINE NDANI YA TANZANIA HIVO CCM na CHADEMA WAKAE PAMOJA WATATUE MGOGORO HUO. KKY MAKAMBA NA NUNDU LAKE AKAPAYUKA AKABEZA NA KUKATAAA MAONI YA KADA MKUU LOWASA!

Tumemsikia MALECELA NA NAHODHA WAKIKIRI KUWA MGOGORO UPO NA LAZIMA CHADEMA NA CCM WAKAE PAMOJA WAMALIZA HILI TATIZO. BADO MAKAMBA AMEKOMAA KUWA CHADEMA WAENDE MAHAKAMANI!!!!!!!!!!!HUYU MZEE NI KICHAA PERCE!!!
 
Baada ya Makamba kuanza nukuu zake kutoka kwenye Biblia Takatifu; tayari nilijua ni nini mwelekeo wake kuhusu maandamano ya Arusha. Nilijua mwisho wake ni kwenye Udini ndo maana nikamsii Makamba aachane kabisa na nukuu zake zisizo na maana.

Hakuna udini Tanzania na atakayeuleta udini ni Makamba na Kikwete wake na hii ni kutokana na kufirisika kisera. Sijui kwanini CCM walimchagua Makamba kuwa Katibu Mkuu mtu ambaye mimi naona kama HAMNAZO. Uwezo wake wa kufikiri ni mdogo sana; hatofautiani na watu wa vijiweni kwa Mtogore. Hivi CCM haina watu wanaoweza kuwa Makatibu Wakuu? Huyu mzee anakiua chama bila wao kujua; au ndo sera yao kukiua chama?.

Makamba Sasa Yatosha, hatutaki huo upuuzi wako.
 
labda mie sielewi haya
1. Kwanini viongozi wa dini wakikosoa selikari ndipo hoja za kufanya mambo yasiyo wahusu huja? wakiipongeza hakuna maneno kabisa.
2.Kiongozi huwa na mipaka? yaani viongozi wa dini hawaruhusiwi kukosoa mfumo wa selikari yao? angalau viongozi hao wangekuwa wazungu na wanakosoa selikari ya tanzania hapo shida ingekuwepo, lakini nao ni watanzania na wanapiga na wanaweza kupigiwa kura.
3.Kwanini waislamu walaani kauli ya viongozi wenzao na sio tatizo? tatizo ni uchaguzi wa meya wa Arusha na sio kingine je waislaamu wanatuambia nini kwa mchakato wa kumpata meya ?Au kwakuwa ni wa CCM basi hapo hakuna shida?
4. Viongozi wa dini hawapaswi kuielimisha jamii?

No one said that viongozi wa dini don't have the right to voice their opinion, you are missing a bigger picture here. I've just highlighted some of your statements that show "us and them mentality"....a sick division we should avoid/fight. There is no argument when it comes to the good role of religion in any society, but again this is if we trade it right....otherwise the same viongozi could cause devastation
 
Kwa wakristo kutomtka Kikwete, nadhani lina ukweli ndani yake. Tazama hata humu JF, ni wakristo wangapi wanomponda Kikwete ingawa ni wazi kabisa kuwa Kikiwete ni kiongozi mzuri, mchapa kazi na ameifikisha mbali Tanzania katika miaka hii mitano.

Hiyo ni stetimenti ya jumla sana "wakristo kutomtaka Kikwete"! Kama ndivyo hivyo basi itabidi ukubaliane na madai ya wapinzani kwamba kaingia madarakani kwa hila maana haiwezekani kwamba kura milioni 5 alizopata ni za waislam. Na kama ndivyo basi kura zilizobaki (milioni 3) ndizo waligawana wagombea wa upinzani. Elimu ya idadi ya watu (demography) inakataa mtazamo huo.

Kila mtanzania anayeshadidia udini ni vema akafanya tathmini kujua
1) Hana ndugu ambao ni wa dini tofauti na yake
2) Hana watu wa dini nyingine waliochangia kwa yeye kufika alipo sasa
3) Atakuwa na raha timilifu ikiwa Tanzania itakuwa na watu wa dini yake tu (mfano kama ni mpira wananchi wote wawe mashabiki wa Yanga), hakuna diversity.

Ni vema sisi watanzania wa kawaida tukatazama nje ya kile wanasiasa wanakisema, wao kula yao inatokana na siasa na wako tayari kutumia chochote ili mradi masilahi yao yanalindwa. Leo hii CCM watatumia kete ya udini kwa ku-side na waislamu lakini mkiwaomba mahakama ya kadhi hawawezi kuwapa maana wanajua kesho watawahitaji wakristo na wapagani.

Mamlaka ya baba kwenye familia hayatokani na dini anayosali bali uwezo wake wa kukabili changamoto za familia yake. Kikwete atende yale yatakayotoa majibu ya kero za watanzania. Hii habari ameifikisha mbali nchi inategemea hiyo mbali kwa kuelekea wapi.

Mbona wapinzani wanapowashambulia kina EL, AC, Mzee wa Kikofia, Gavana n.k hamsemi kama ni udini???
Wengi wetu hapa hatutakuwepo miaka 50 ijayo, je ni Tanzania ya kuchinjana ndio tunataka kuwaachia watoto wetu???

Tafakari!!!!!!!! chukua hatua.
 
Yaani hata yale majinamizi makuu (Ujinga, Umasikini na Maradhi) hayajamalizwa tayari watanzania wanakaribisha jinamizi jingine.
 
Mimi ni Muislamu na nimemuona Sheikh akisoma taarifa yake,ni kwamba haya matamshi wemepikiwa.
Hivi ni kweli Wakristo hawamtaki Kikwete,kuna ushahidi wa kutosha?Mbona 2005 wakiristo walitamka ya kuwa Kikwete ni Chaguo la Mungu?

CCM inatupeleka pabaya, hakuna udini Tanzania ila CCM kwa kutaka madaraka wako tayari kufanya lolote. CUF wameshindwa kujinasua katika hilo.
 
Amani Katoshi: Labda nimesahau. Hivi kanisa lilitoa tamko baada ya mauaji ya wana CUF? Hivi kulisema kanisa ni Udini? Nikisema kanisa lilishiriki katika mauaji ya kimbari Rwanda(Vatican wamekiri na kuomba msamaha) nitaitwa pia mdini? Na wapi nimeshindwa kuoanisha mambo? Je CUF hawakuuawa kwa sababu ya maandamano ya kupinga matokeo ya uchaguzi kama CDM walivyouawa Arusha?

I wanna know whether you are happy with the current political situation in Tanzania. You might have been not going to school that's why you have encountered such a myopic problem. Hivi wewe na hao mashee mlionunuliwa hamkuona kuwa kuna ukweli kuwa Meya alichaguliwa kibadhirifu? Mbona naibu wake amestep down kwakukiri kulikua na tatizo? Ninyi mnatatizo kwanza la unafiki na kisasi kingi.

EPA, KAGODA, DOWANS ambayo zinawaathiri hata familia zenu ila ninyi hamuezi jua gharama kwasababu madrasa hata chini ta mti mnaweza kusoma wala hamna haja ya kutumia computer hivyo hayawaathiri, ninyi ni watu wa giza tu.
 
Kwa wakristo kutomtka Kikwete, nadhani lina ukweli ndani yake. Tazama hata humu JF, ni wakristo wangapi wanomponda Kikwete ingawa ni wazi kabisa kuwa Kikiwete ni kiongozi mzuri, mchapa kazi na ameifikisha mbali Tanzania katika miaka hii mitano.
Wewe kweli unatumia makalio kufikiri,Hapa JF unamjua nani kuwa ni mkristo au mwislamu? au unakutana nao kwenye kuswali au kusali? acheni ujinga basi! dini inawafanya hata kufikiri mnashindwa? mmeng'ang'ania kubishana ukristo na uislamu, mbona kuna dini nyingi tuu, Budha,hindu nk na hawana kelele? Kama kiongozi mbovu asiambiwe kwa vile ataonekana anaambiwa kwa vile dini ni tofauti? mawazo ya kipumbavu ya aina hiyo sijui yametoka wapi! mbona awamu hii ujinga umezidi sana? hivi ujinga huu ni asili yenu au umepandikizwa kwa maslahi fulani?
 
Hivi labda sielewi kwani maaskofu wamesema hawamtambui Kikwete au hawamtambui Meya? I think they said Meya so why is it a religion issue wakati meya mwenyewe mkristo. Duuh! I am failing to understand kama ni uwezo, uvivu, au uzembe wakuchambua mambo tunaishia kukurupuka. Sometimes the way one sees the problem is also a problem.
 
Ndugu yangu UNSTPPABLE hawa jamaa wanaanzisha thread ambazo hawana nguvu ya kuzijengea hoja, kila kitu wanaonewa. Sasa wajinga kama hawa tusipowajibu kwa hoja itaonekana tumepwaya, hata sisi hatupendi kuzungumzia udini, nikwasababu hiyo. Ila wazo lako ni zuri na tutalifanyia kazi.
 
Kwanza kabisa katika hili hakuna udini kulifumbia macho ni kuendekeza wauwaji na hatutabaki kuwa na amani hii tulionayo.. Hawa jamaa huwa wanatafuta point ndogo sana kisha kuikuza ili ionekane ni udini.

Popote ulimwenguni nchi ikiwa legelege hawa jamaa huibuka kama uyoga na kuanza kudai wanaonewa. Je mwayajua yatokeayo Zanzibar makanisa na waumini kufanyiwa vurugu ni kawaida. Sipendi kusoma kitabu chao ila nasikia kinaruhusu mtu ambaye si wa kambi yao kukatishwa uhai halafu aliyehusika kupata thawabu. Kwa hiyo wanataka sana kuleta vurugu ili watuuwe wakidhani wanapate thawabu.

Anyway Almighty God be on our side epusha vita Tanzania make tz sea of peace waelimishe na kuwaondoa wale wote wanaofurahia mauaji ili tubakiwe na amani. Tuheshimiane na tusipende kila Maaskofu wakiongea kuwapinga mana ndo kuimarisha udini huko. Na pia Maaskofu nawaomba Mashehe wakitoa tamko tusiwapinge kwa minajiri ya kidini bali tuwapongeze kama wameongea jambo jema.

Napenda Amani, naipenda Tanzania.
 
CCM wangeanza kwanza kuonyesha mfano kwa kumvua Mch. Lwakatare majoho ili awe mbunge tu. Halafu hivi wanaokatazwa kushiriki kwenye siasa ni viongozi wa dini tu? Na polisi Je? Na mahakama Je?
 
Ni lini WATANZANIA tutajadili hoja badala ya kumjadili mtoa hoja?
 
Nilijua watatoka kihivi, achaneni nao, waendelee kutafuta mahakama ya Kadhi!
 
Amani Katoshi: Labda nimesahau. Hivi kanisa lilitoa tamko baada ya mauaji ya wana CUF? Hivi kulisema kanisa ni Udini? Nikisema kanisa lilishiriki katika mauaji ya kimbari Rwanda(Vatican wamekiri na kuomba msamaha) nitaitwa pia mdini? Na wapi nimeshindwa kuoanisha mambo? Je CUF hawakuuawa kwa sababu ya maandamano ya kupinga matokeo ya uchaguzi kama CDM walivyouawa Arusha?

Vatican imekiri wapi kuhusika na mauaji ya Rwanda? Tuwekee japo link au source ya maneno yako?
The pope has apologised for abuses in Ireland but not yet for reported abuses in Germany, Italy and recently in Wisconsin. And no-one in the Vatican has apologised for the actions of priests in the genocide in Rwanda. Not that apologies are enough - action is needed. Strip guilty priests of their priesthood - if they object, excommunicate them as well. Make it clear that action is taken immediately and that no cover up will ever be done again. If you try to research Catholics and Rwanda, you don't get much - but a recent report in the UK Guardian by Martin Kimani spells out some of what is known. And it's not pretty. In many ways it's worse than abuse of defenceless children.


Nimeitoa hapa:
Pope must acknowledge role in Rwanda genocide

Sasa mwenzetu hizo apologies umezisikia wapi?

Kwani kuna mtu anabisha kuwa kuna raia waliuawa Pemba, Unguja na Dar es Salaam kama ilivyotokea Arusha?

Amandla....
 
Huyu fundi mchundo hawezi kukubali ukweli asilani, bcz ubongo wake ni wa kifuu,jaribu kusoma kwa makini post zake utaona, shortly wa kupuuzwa!

Huwa nakubali michango yako mingi ambayo huwa inajikita kwenye fact-lakini hii leo ni zero tena beyond pumba za mtama. Mkuu why unataka kupingana na facts?

Kwanza unanisifu kuwa kabla ya hii ishu ulikuwa unaniaminia, halafu unadai kuwa ubongo wangu ni wa kifuu! Kweli umesinyaa siku moja tuu? Sikukuomba usome posting zangu na utakuwa unanifanyia favour kama utaacha kuzisoma.

Amandla....
 
Back
Top Bottom