Zimmermann
JF-Expert Member
- Sep 28, 2010
- 2,765
- 1,208
Hivi bakwata inawafanyia nini Waisilamu kama siyo kutumiwa tu na CCM?
Mimi ni Muisilamu lakini nakerwa sana na chombo hiki kinachodaiwa ni mwavuli wa Waisilamu wote nchini.
Hakina faida yoyote kwa Waisilamu na sasa hivi viongozi wake wanatia aibu kwa kukubali kutumiwa na wanasiasa na viongozi wa serikali ya CCM, tena bila hata ya faida yoyote kwao, achilia mbali shukurani.
Na kinachosikitisha zaidi ni kwamba haya ‘mateke ya punda' wanayapata chini ya uongozi mkuu wa nchi aliye madarakani ambaye ni Muisilamu.
Hivyo kinachoonekana ni kwamba baadhi ya viongozi hawa wa bakwata huhongwa kwa hela za muda mfupi tu.
Hapa nitatoa vielelezo vya kuonyesha kile ninachokisema:
Pamoja na kwamba ni juzijuzi tu JK alipigilia msumari wa mwisho kuhusu mahakama ya kadhi, Bakwata si tu imeufyata kabisa, bali pia inakubali kutumiwa na hiyo hiyo CCM kufanya ‘cheap' campaign kwa niaba yao kule Igunga.
Suala la DC wa igunga na Bakwata kukurupuka kumtetea ni mojawapo ya mambo yanayoonyesha ‘ukibaraka' wa viongozi wake, sijui kwa sababu ya umasikini? Suala la DC lilikuwa la kisiasa, lakini Bakwata wakaingilia kulifanya la kidini, na kama vile nilivyosema hawatapata shukurani yoyote kutoka CCM, bali mateke ya punda tu katika madai yao yote halali.
Kuna suala la OIC kadhalika – Bakwata ilishafungwa mdomo tangu zamani, lakini wanaume bado wamo tu na CCM!
JK aliwakera sana Waisilamu kwa kumleta Rais George W Bush wa Marekani, aliyesababisha vita Iraq na Afghanistan ambapo maelefu ya Waisilamu wamekufa na kuendelea kufa.
Kwanza wakati wa ujio wa Bush serikali ilipiga marufuku maandamano yoyote ya Waisilamu kuupinga ujio huo, lakini baadaye akina Kundecha walisimama kidete na yakaruhusiwa.
Mwaka 2007 JK alikwenda Vatikan kuonana na Papa Benedict, kuna picha ikimuonyesha akipiga magoti na kuubusu mkono wa Papa. Jee ilikuwa lazima aende huko? Mkapa, Mkatoliki, katika miaka yake 10 ya uongozi hakufikiria kufanya ziara ya namna hiyo.
Tukienda nyuma zaidi wakati wa Mzee Ruksa, Rais wa kwanza Muisilamu wa nchi hii. Serikali yake nayo ilikuwa na maudhi yake mengi dhidi ya Waisilamu:
Alimleta papa John Paul II mwaka 1990, kitu ambacho hata Nyerere mwenyewe Mkatoliki hakufikiria kukifanya.
Mwaka 1993 wakati serikali hiyo ya Mwinyi iliporekebisha siku za kazi kwa watumishi wa serikali kuwa siku 5 kwa wiki (yaani kuondoa Jumamosi kama siku ya kazi) pia alirudisha Sikukuu ya Boxing Day (December 26) hivyo Wakristu kuwa na jumla ya sikukuu nne za kidini kwa mwaka (e.g. Pasaka siku 2, Christmas na Boxing Day) – hivyo kwenda sambamba na Waisilamu ambao tangu zamani za Nyerere walikuwa na sikuu 4 za kidini kila mwaka (yaani Id el Fitr siku 2, id el-Hajj na Maulidi).
Lakini hapo hapo Mwinyi pia alirudisha Januari mosi kama sikukuu ambayo ilikuwa haipo tangu enzi hizo za Nyerere. Swali hapa: Kama aliweka Januari mosi kuwa siku ya mapumziko, siku ambayo ni mapumziko katika ulimwengu wa nchi za Kikristo, kwa nini, pia asiweke siku ya mwanzo wa mwaka wa Kiisilamu (tarehe mosi Muharram - Mfungo Nne) kuwa pia ni sikukuu ya kupumzika? Mwaka jana Waisilamu walisikika wakiiomba serikali nayo pia iiweke siku hiyo iwe ya mapumziko.
Tukiacha hilo kuna suala lile lenye mgogoro la Memorandum of Understanding (MoU) kati ya serikali na Makanisa. Waisilamu hawakuona ajabu kwamba hili lilianza chini ya utawala wa Rais Ali Hassan Mwinyi Muisilamu? Wangemuuliza kwa nini aliwasahau Waisilamu katika MoU?
Kwa ujumla pamoja na mambo yote haya yote hasi (negative) dhidi ya Waisilamu niliyotaja – bado Waisilamu wanaing'ang'ania CCM na kuitetea hata katika mambo cheap kabisa.
Wako wap akina Mponda, Kundecha na Sheikh Khalifa, viongozi machachari wa Kiisilamu waliokuwa wakiihenyesha serikali huko nyuma (eg katika sakata la mauaji ya Mwembe Chai)? Au tayari kwisha nunuliwa na CCM?
mkuu hapo kwenye wekundu una hiyo picha?