Baki njia kuu, epuka Michepuko!

Baki njia kuu, epuka Michepuko!

Mkumbuke huko kwenye vichochoro ndo kuna misumari na miba mikubwa mtatoboa tairi zenu hata mkija kwenye njia kuu mnatembelea viraka.
Na njia kuu ndo kuna misumari ya kutegeshewa kwenye mifuko ya nailoni na vipande vya mbao

 
Aisee! Ujumbe huu una mkanganyiko sana! Yani kuliko kumshauri mtu kuwa na mmoja tuu kitu ambacho kwa sasa kimeshindikana ni bora kumshauri kutumia kinga.
 
Mkumbuke huko kwenye vichochoro ndo kuna misumari na miba mikubwa mtatoboa tairi zenu hata mkija kwenye njia kuu mnatembelea viraka.

Vichochoroni hatupiti kwa fujo. Haraka ya nini wakati njia fupi?
 
Hakuna kitu kinachokera kwenye njia kuu kama ule ukarabati wa kila mwezi, njia inafungwa siku tatu au zaidi. Kero kwa watumiaji

!Nduka sasa huko uchochoroni ndo hakunaga hata kupalilia uchochoro au unataka kusemaje? Mbona mnatafuta visingizio vya kuchepuka? Baki njia kuu bwana
 
Aisee! Ujumbe huu una mkanganyiko sana! Yani kuliko kumshauri mtu kuwa na mmoja tuu kitu ambacho kwa sasa kimeshindikana ni bora kumshauri kutumia kinga.
Ruttashobolwa hii imetokana na kuwa watu hawana hofu ya MUNGU huku wengine wakiamini hakuna MUNGU.
 
Last edited by a moderator:
Asante kwa ujumbe. Hata mie nilishamwambiaga siku nyingi achague kwangu au kule, mambo ya kuchanganywa sipendagi. Namshukuru amenielewa. Hakuna kuchepuka, uko kwangu kaa kwangu, kule ushatoka achana na mambo ya kule yalopita yamepita.
 
Ila sasa toka nimeanza kusikiliza haya matangazo ya redioni ya Baki njia kuu mbona ni matuko ya kunaswa wanawake tu?, wao ndio wanaotumia vichochoro zaidi au?
 
!Nduka sasa huko uchochoroni ndo hakunaga hata kupalilia uchochoro au unataka kusemaje? Mbona mnatafuta visingizio vya kuchepuka? Baki njia kuu bwana

Uchochoro hauna ukarabati ni all weather, masika madimbwi kiangazi vumbi tunadunda tu.
 
Hahahahaa umekamatika loh si umejifanya mjuaji? Baki njia kuu Babu unaona? chochoo hizo!

lol chocho nyingine laanakum. hizo namwachia Fidel80 muzee ya tope. kidume kinataka kunipa uchochoro LMAO!!!!
 
Last edited by a moderator:
Asante kwa ujumbe. Hata mie nilishamwambiaga siku nyingi achague kwangu au kule, mambo ya kuchanganywa sipendagi. Namshukuru amenielewa. Hakuna kuchepuka, uko kwangu kaa kwangu, kule ushatoka achana na mambo ya kule yalopita yamepita.

Da Sofi bhana.
 
Back
Top Bottom