Bajaj ya wajawazito - Ahadi imetimia!

Bajaj ya wajawazito - Ahadi imetimia!

Hivi hizo bajaj zina uwezo wa kuhimili mikiki na mihangaiko ya uchungu wa mama anapotaka kujifungua???

......................................................

yaani hao walioapprove huu mradi utadhani hawajawahi kumuona mjamzito mwenye utungu anavyhangaika............. ina maana hao waliokubali zinunuliwe hawakuwa na mwnaamke japo mmoja anayeijua vizuri shughuli ya kujifungua ilivyo?........ si wangewauliza wakina mama wenyewe watoe maoni kwanza kabla hawajakurupuka?......... jamani nina hasira hapa, nyie acheni tu!............... naungana na aliyesema kuwa tanzania tunalo janga fulani la kitaifa la uongozi ........... khaaaaaaaaaaa.................
 
Hivi hizo bajaj zina uwezo wa kuhimili mikiki na mihangaiko ya uchungu wa mama anapotaka kujifungua???

......................................................
JS,
Nimejiuliza maswali kadhaa nikakosa majibu!
Katibu Mkuu Bibi Blandina Nyoni si ni mwanamke na amezaa?
Niachie hapa nisije kuropoka maneno yakunivunjia heshima yangu!
 
Inanisikitisha sana hali hii kiasi kwamba najiuliza hivi hao wabunge tunaowaita VITI MAALUMU wanafanya nini bungeni km hawawezi kuelezea hali halisi ya mwanamama anapokua mjamzito na wao ni wanawake na wengi wao wana hadi vitukuu.......sioni sababu ya kuwepo viti hivyo kama wanashindwa hata kutetea vitu muhimu namna hii na hali wao wananengua tu kwenye mavx.
Mara elfu kumi kila wilaya ingepewa town ice hata 1 kulikoni hizo pikipiki. Na hapa wataongeza sn maternal death
 
Samdala are you serious? Kwenye mshahara wako unakatwa shilingi ngapi kama kodi ili kuchangia maendeleo ya taifa hili? sasa iweje tukanunuliwe bajaj za kubebea wajawazito,hii ni kejeli kwa wadanganyika! Something has to be done,ikibidi tujiunge na nchi za kiarabu na tufanye kama Libya ili waelewe kuwa tumechoshwa na hizi kebehi na hatudanganyiki tena!
 
JS,
Nimejiuliza maswali kadhaa nikakosa majibu!
Katibu Mkuu Bibi Blandina Nyoni si ni mwanamke na amezaa?
Niachie hapa nisije kuropoka maneno yakunivunjia heshima yangu!

yaani mpendwa ....................... aah, ngoja na mimi niishie hapa........... ila imenibore sana sio siri............
 
Inanisikitisha sana hali hii kiasi kwamba najiuliza hivi hao wabunge tunaowaita VITI MAALUMU wanafanya nini bungeni km hawawezi kuelezea hali halisi ya mwanamama anapokua mjamzito na wao ni wanawake na wengi wao wana hadi vitukuu.......sioni sababu ya kuwepo viti hivyo kama wanashindwa hata kutetea vitu muhimu namna hii na hali wao wananengua tu kwenye mavx.
Mara elfu kumi kila wilaya ingepewa town ice hata 1 kulikoni hizo pikipiki sitaki ht kuziona....mvyuuu

hali za wanawake wanapojifungua wala si ya wananwake pekee wala si ya hao wa viti maalum................ hata wanaume tunajua vizuri sana,................. si sisi ndio tunaowapeleka hospitali na siku hizi tunaruhusiwa hata kuingia labor na kumpa tafu mamam hadi dakika ya mwisho?............. sasa mtanange ule na vibajaji vya miguu miwili wapi na wapi!............ akijigeuza tu si kanapinduka? kule kwetu kimara na vichuguu vile kitapandaje na kitashukaje na mjamzito akijigeuza kwa utungu? kijijini je, katamudu nini hata bila mafuriko/mvua............... aaagh, hawa watu jamani, janga gani hili?....................
 
Fadeless haimaanish pesa ninayokatwa ni kwa jili ya bajaji tu,,..ni kwa maendeleo ya nch kwa ujumla,,..na sina uakika kwamba serikal yet ina uwezo wakununua magar ya wagonjwa ya kumfikia kila mtanzania kwenye kila kona ya nchi hi...,.so kama tunauwezo wa pikipik kwa sasa kwa nini tusizinunue zipunguze makali ya tatizo wakati tukitafuta uwezo wa magari ya wagonjwa.........and kweny hili usijifikirie wewe ambaye kwenye mtaa wako angalau kuna hsptl moja au mbili zenye ambulance..mfikirie yule mtanzania ambaye hajawai kuisikia ambulance hali ya maisha kwake is almost zero.....hiz pikipik zitamgusa yeye kwa kiasi kikubwa....wewe angalau una uwezo wa kuagiza hata tax....
 
Mwenzenu hapa ninapoishi nina shemeji yangu mjamzito wa miezi tisa, tumbo ni kubwa saana na hawezi kulala kifudi fudi kama walivoonyesha kwenye hilo Guta/bajaji.

Sasa wanamsaidiaje mama mwenye tumbo kubwa na uchungu huku akitapa tapa kwenye hilo guta? maana hiyo chemba ni ndogo sana na lazima ulale kifudi fudi.


shemeji yangu hilo guta simpandishi hata kwa mtutu, bora nimsukume kwa baiskeli taratibu.
 
......hii serikali ina utani sana, hivyo hapo huyo mama mjamzito atawekwa wapi? Hivyo wizara ya afya akili zao zina akili kweli? Yaani hapo ndio upeo wao wa akili ulipofikia kuamua kuishauri serikali kununua kitu kama hicho.........utafikiri hakuna wanawake vile huko wizara ya afya.
 
Kwanza kabajaj kalivyo kadogo haiwezekani kumuweka mama mjamzito akapita kwenye kamlango kaka!
 
Kama nakumbuka vema ziliahidiwa bajaji zaidi ya mia nne kwa wilaya ya chunya achilia mbali sehemu nyingine!!!Ni mradi wa kutosha tu!!!
 
Huyu raisi ni mmbabaishaji tu hii miradi ni ya wapambe wake wanajaribu kurudisha pesa zao walizotumia wakati wa uchaguzi
 
......hii serikali ina utani sana, hivyo hapo huyo mama mjamzito atawekwa wapi? Hivyo wizara ya afya akili zao zina akili kweli? Yaani hapo ndio upeo wao wa akili ulipofikia kuamua kuishauri serikali kununua kitu kama hicho.........utafikiri hakuna wanawake vile huko wizara ya afya.

hata mie nashangaa sana mpendwa!!!!!!!!!!!............. yaani....................
 
JS,
Nimejiuliza maswali kadhaa nikakosa majibu!
Katibu Mkuu Bibi Blandina Nyoni si ni mwanamke na amezaa?
Niachie hapa nisije kuropoka maneno yakunivunjia heshima yangu!



Sijui kama nitaiponyaka BAN, .....PID!
 
Barabara ya Makongo Juu ilivyo na mashimo hapo mjamzito lazima ajifungue njiani! ....Sasa imagine barabara za vijijini itakuaje ukizingatia na umbali wa vituo vya afya ?
 
......hii serikali ina utani sana, hivyo hapo huyo mama mjamzito atawekwa wapi? Hivyo wizara ya afya akili zao zina akili kweli? Yaani hapo ndio upeo wao wa akili ulipofikia kuamua kuishauri serikali kununua kitu kama hicho.........utafikiri hakuna wanawake vile huko wizara ya afya.

kwa kweli bado tuna safari ndefu kufikia hicho kinachoitwa busara!
 
Hapo ndipo kikomo cha uwezo wao wa kufikiria na kutatua matatizo ya jamii na wapiga kura wao. Cha kufurahisha ni kuwa utaona wanatinga katika vyombo vya habari kuelezea hilo nalo kuwa ni hatua kubwa ya mafanikio katika sekta ya afya. Sujui wanasafiri kwenga Nchi za wenzetu kufuata nini kama hawawezi hata kuiga yanayofanyika humo kama ubunifu umewashinda.
Masknini mwanamke wa TZ. hathaminiwi kabisa.
 
Back
Top Bottom