Bahima empire almost there...!!!

Bahima empire almost there...!!!

Pierre Nkurunziza ni mhutu ambayo ni Bantu group hana uhusiano na bahima empire ila kwa mbali nasikia ni mixed blood, mama mtutsi na baba mhutu ila kuhalalisha kukubaliwa ,anawachukia watutsi kuliko hata wenye damu ya pure wahutu . Lakini hoja ni udictator ambayo umeshamiri Africa. Haijalishi ni Bantu au bahima issue ni kuwa bara Afrika na Asia ndio tumebaki na element za chama kimoja/kabila moja /dini moja/ukoo mmoja nk, kutawala milele. Ina maana hata wazungu wameona tuwaache hawa watu wavurugane wakichoka wataheshimiana . Ni kiwango cha uduni Wa kuelewa mambo kwa mapana yake ndio unafanye tutawaliwe hivi. Siku wengi wakiwa na mwamko tutakataa. Kama katika jamii watu mafisadi wanaporomosha majumba ndani ya mitaa yetu tunawasifu unashangaaje MTU akibadili katiba, si muendelezo Wa uvumlivu wa jamii kukubali kukandamizwa . Lile tusi la mbaguzi trump ( shit hole countries) si alikuwa anashangaa waafrika ni watu wa ajabu wanashindwa kuziwajibsha serikali zao. Kuna Siku tutatoka katika madhila haya ,siku tutakapoamini kuwa afrika tunahitaji Taasisi imara imara na sio kiongozi imara (we need strong institutions not strong men) ili tupate maendeleo.Ila contradictions za maendeleo, mbona China anapiga maendeleo kuliko India wakati moja ni largest single party dictatorship na nyingine largest multiparty democracy in the world. Lee Khan Yew aliitoa S.Korea kutoka third world country na kuifanya iwe first world democracy ndani ya muda Wa kizazi kimoja, kwa gharama kubwa ya kuminya haki za binadamu. Wengine wanaamini binadamu hawezi kula democracy na wengine wanaamini kuendelea bila kuwa na Uhuru Wa kutoa mawazo ni ni kumdunisha binadamu. Furaha yako au huzuni yako inategemea uko kundi gani kwa yanayotokea Afrika. Nimamua Kuwa neutral . Lakini tukubaliane kuwa jamii hupata kiongozi ambaye ni stahili yake. Hata tujidanganye vipi lakini ndani ya mioyo yetu bado Africa tunahusudu udictator . iwe ni ngazi ya familia/ kitongoji/ kata/ wilaya hadi taifa tunapenda kutoa maagizo na walio chini yetu wafuate tu. Hivi hata ndani ya vyama pinzani hatuoni mwendo ni kuburuzana tu. ?
Mleta mada kapiga fix na hearsay za huku na kule.. Mara asema Pierre kawekwa kama cover, mara aseme Watutsi wamekosa Mtutsi wa kumpandikiza yaani ni full fix fix..

Malcom Lumumba
 
Nafikiri ndio mna shida huyo kawekwa alipo kupoteza lengo...
Kihistoria kamwe mhutu hawezi kuwa mtumwa wa watutsi,nkurunziza anachokifanya ni moja ya njia ya kuwajulisha watutsi kote duniani wasahau kuitawala burundi
 
Habari mbaya Taifa huru la Burundi linaloanza wiki nazo ni kwamba rais wa nchi hiyo Pierre Nkuruzinza amepitishwa rasmi kuwa rais wa kudumu kudumu na mwenyekiti wa milele wa chama tawala

Sitaki kuijadili Burundi kama taifa huru bali Burundi kama sehemu na mwanachama wa jumuiya ya Afrika mashariki...

Hii ni nchi mwanachama wa tatu katika nchi 6 zinazounda umoja huu (sijataja Sudan bado impact yake ni ndogo) Tayari Uganda chini ya Kaguta na Rwanda chini ya Kagame marais wake wamejirasmisha utawala wao kupitia chaguzi bandia..

Nani anafuatia!? Kenya? Kongo? Tanzania? Yeyote atakayefuatia kujiunga na huu udhalimu ile BAHIMA EMPIRE itakuwa imezaliwa rasmi....
Kongo iko Afrika Mashariki?
 
Huwa naona walioleta siasa ya vyama vingi walikuwa na lengo la kututofautisha lugha ili tukwame kama ilivyokuwa kwenye mnara wa Babeli sababu hata yule aliyeshindwa atabaki kuwa Rais wa wale walioshindwa na akiongea kitu wafuasi wake wanamtii kwahiyo automatic kunakuwa na marais wengi kwenye nchi. Inafika hatua Rais wa nchi anasema hivi na huyu mwingine anasema vile matokeo yake hamuendi popote.
Neno sana hili
 
Back
Top Bottom