Bado wapo wenye imani na CHADEMA?

Bado wapo wenye imani na CHADEMA?

Hawa CHADEMA ndo basi tena.

Naona wapo kwenye mwendokasi wa kuelekea kaburini.

Hii si mara yao ya kwanza kuwapandisha watu mzuka halafu wanaishia kubadili gia angani na kuwaacha watu wakining'inia.

Nani tena atawaamini hawa jamaa? Manake baada ya kuwaaminisha watu kwa miaka mingi kuwa Lowassa ni fisadi, matokeo yake ndo akaja kuwa mgombea wao. Mamlaka ya kimaadili ya kukemea ufisadi wakayapoteza.

Baada ya kuwapandisha watu mzuka wa UKUTA, leo wameufyata mbele ya Ngosha.

Sasa eti wametangaza hayo maandamano yatafanyika Oktoba mosi.

Watampata nani hiyo Oktoba mosi? Wake, waume, na watoto wao?

Wameishiwa kabisa. Hawana jipya tena. Hawana dira wala mwelekeo wowote ule.

Mtu afadhali unaweza kusema kuwa kabla ya ujio wa Lowassa kwamba watu walijua wanasimamia nini na wanasimama wapi.

Lakini leo hii nani anayejua wanachokisimamia? Nani anajua wanaposimama?

Walishindwa hata kuwashawishi wapinzani wenzao kuwaunga mkono ki hali na ki mali kwenye huo UKUTA wao. Wengine wakadiriki hadi kuwatakia kila la kheri na kuwaahidi kuchangia damu endapo wangehitaji baada ya kupokea kichapo cha vijana wa Ngosha.

Matokeo yake tingatinga limepita na kuusambaratishia mbali.

Wanahitaji uongozi mpya wenye maono mapya la sivyo wataenda bye bye for good.

Inashangaza kwamba bado Watanzania wenye uelewa kama wewe unapigia debe Siasa za Kishabiki badala ya Maendeleo. Hivi kama CHADEMA wangeandamana unadhani madhara yangetokea kwa Waandamanaji tu? je wananchi wanaowazunguka?

Kumbuka amani inapochafuka haingalii kwamba wewe uko chama gani bali inamwathiri kila mmoja wetu. Kumbuka hata hao CHADEMA pia ni WATANZANIA kama wewe na ukifuatilia kwa umakini unaweza ukakuta familia moja ina Wanachama wa CCM na wale wa CHADEMA kwahiyo usidhani kwamba ukosefu wa amani uko kwa wapinzani tu.

Bila shaka nia yako ilikuwa ni kuona leo watu wamepigwa risasi au kupigwa virungu na kujeruhiwa vibaya ama kufa. Huo ni uchochezi mbaya sana.

CHADEMA kama Chama kingine chochote cha SIASA wana haki ya kufanya maandamano ilimradi tu hawavunji Sheria na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Sasa unaposhabikia mabavu ya uonevu yanayofanywa na Serikali iliyoko madarakani usidhani kwamba ni sifa au inakusaidia chochote zaidi ya kuwa mwenye mawazo mgando.

Tukumbuke kuwa Nchi hii ilikubali kuanzishwa SIASA ya vyama vingi yenyewe mwaka 1992. Nakumbuka kipindi kile nikiwa mdogo ilipigwa kura ya maoni kama je Watanzania wanataka Siasa ya vyama vingi na 80% walitaka tubaki kwenye Siasa ya Chama Kimoja. Sasa Serikali yenyewe ama kwa shinikizo la IMF (Kupewa misaada) waliamua kuingia kwenye Siasa ya vyama vingi. Sasa kama tumekubali wenyewe kuingia kwenye Siasa hiyo, je ni kwanini tunawakandamiza wale raia walioamua kuwa vyama vya upinzani?

Nakumbuka Rais aliyepita Mhe. JK pamoja na mapungufu yake kama binadamu yeyote lakini aliweza kuongoza kwa kufuata Utawala wa Sheria/Katiba na aliweza kupambana na hawa wapinzani kwa kutumia hoja na si vitisho na kuwakandamiza. Kwa kutumia njia hii hii aliweza kuweka mkakati wa kutembea Nchi nzima (Kinana pamoja na Mhe. Nape) ili kukiimarisha Chama. Hii ndio njia inayopaswa kuigwa na Rais aliyeko madarakan.

Kutumia ubabe na mambo mengine ambayo sio ya msingi yanaturudisha nyuma kwa enzi za Chama kimoja ambazo kamwe hazitaweza kufanikiwa maana hizi ni dhama nyingine na karne tofauti kabisa. Pia namshauri Mheshimiwa Rais asitumia nguvu nyingi sana kuwabana wapinzani kwani wanampotezea sana muda wa kufanya shughuli za maendeleo na kutekeleza ilani ya CCM.
 
Ogopa sana lidude fulani linaitwa mfumo. Linapoingia kazini, jiandae kwa maumivu, na huo mfano wako unakuwa umesahaulika kwani hautaweza kukusaidia.

Wewe huelewi. Unataka kuwaminisha watu kuwa Mbowe na wanaCDM walikuwa hawajui hatua zitakazo chukuliwa na Mfumo/Serikali/CCM?.
Amini hivyo maana hata Makaburu waliamini Mandela atafia Jela na wao watakuwa Watawala wa SA milele.Kinachopiganiwa na CDM ni kwa faida ya wajukuu zako maana wengine wenu ni wanufaika wa Mfumo hivyo kuparaganyika kwa mfumo ni hatari kwa masilahi yenu..
 
Kila mtu ana imani yake,mi naamini hadi sasa wamefanikiwa kupata walichotaka.
 
Wewe huelewi. Unataka kuwaminisha watu kuwa Mbowe na wanaCDM walikuwa hawajui hatua zitakazo chukuliwa na Mfumo/Serikali/CCM?.
Amini hivyo maana hata Makaburu waliamini Mandela atafia Jela na wao watakuwa Watawala wa SA milele.Kinachopiganiwa na CDM ni kwa faida ya wajukuu zako maana wengine wenu ni wanufaika wa Mfumo hivyo kuparaganyika kwa mfumo ni hatari kwa masilahi yenu..
Hakuna cha maana wanachopinga CDM, ni wapigaji tu kama wapigaji wowote unaowafahamu kwenye ubongo wako. Ondoa kichwani dhana potofu kwamba kila kinachofanywa na serikali ya CCM kimejaa uonevu na kile ambacho kingeweza kufanywa na serikali ya CDM kama ingeingia ikulu ni chema na kina kila aina ya baraka. Stop being delusional, came back to the real world.
 
shetani akiamua kuwateka watu haoni nyuma loh hata we we ngabu? sijawahi kupita uzi wako bila kuusoma ila kwa hili bye ngabu!
 
Mimi naona Mbowe akae pembeni sasa maana akili yake imechoka labda kutokana na kuongoza kwa muda mrefu bila kupumzika...
 
Hawa CHADEMA ndo basi tena.

Naona wapo kwenye mwendokasi wa kuelekea kaburini.

Hii si mara yao ya kwanza kuwapandisha watu mzuka halafu wanaishia kubadili gia angani na kuwaacha watu wakining'inia.

Nani tena atawaamini hawa jamaa? Manake baada ya kuwaaminisha watu kwa miaka mingi kuwa Lowassa ni fisadi, matokeo yake ndo akaja kuwa mgombea wao. Mamlaka ya kimaadili ya kukemea ufisadi wakayapoteza.

Baada ya kuwapandisha watu mzuka wa UKUTA, leo wameufyata mbele ya Ngosha.

Sasa eti wametangaza hayo maandamano yatafanyika Oktoba mosi.

Watampata nani hiyo Oktoba mosi? Wake, waume, na watoto wao?

Wameishiwa kabisa. Hawana jipya tena. Hawana dira wala mwelekeo wowote ule.

Mtu afadhali unaweza kusema kuwa kabla ya ujio wa Lowassa kwamba watu walijua wanasimamia nini na wanasimama wapi.

Lakini leo hii nani anayejua wanachokisimamia? Nani anajua wanaposimama?

Walishindwa hata kuwashawishi wapinzani wenzao kuwaunga mkono ki hali na ki mali kwenye huo UKUTA wao. Wengine wakadiriki hadi kuwatakia kila la kheri na kuwaahidi kuchangia damu endapo wangehitaji baada ya kupokea kichapo cha vijana wa Ngosha.

Matokeo yake tingatinga limepita na kuusambaratishia mbali.

Wanahitaji uongozi mpya wenye maono mapya la sivyo wataenda bye bye for good.

Tupo wengi wa kutosha tunaoiamini Chadema.

Je,wewe uko Bongo au Ughaibuni?Kama uko Bongo sawa lakini kama upo ughaibuni basi hukupaswa kuongea unachoongea.Kwanini mlioko Ughaibuni hamkuandamana mpaka balozi wa Tanzania?Mliogopa nini wakati hata Trafiki hakuna?
 
Mimi hapa naipenda Chadema mpaka kufa na hata vyama vyote vya upinzani vikifutwa kamwe cntokaa niipende ccm!
Ongea kingine...!
 
Kiongozi mwepesi kutengeneza maadui zaidi ya marafiki hawezi kufanikiwa na ni hatari kwa taifa"
 
Sijui kwa nini tu watu huwa hawajibu maswali.

Unamuuliza hiki yeye halafu yeye anakuja na ngonjera nyingine kabisa!

Ndo maana tuna mambo kama hayo ya UKUTA.

Bado wapo na ni wengi sana. Ukitaka kujua kila kiongozi aliacha shughuli zote kazi ikawa ni Ukuta tu.
 
Inashangaza kwamba bado Watanzania wenye uelewa kama wewe unapigia debe Siasa za Kishabiki badala ya Maendeleo. Hivi kama CHADEMA wangeandamana unadhani madhara yangetokea kwa Waandamanaji tu? je wananchi wanaowazunguka?

Kumbuka amani inapochafuka haingalii kwamba wewe uko chama gani bali inamwathiri kila mmoja wetu. Kumbuka hata hao CHADEMA pia ni WATANZANIA kama wewe na ukifuatilia kwa umakini unaweza ukakuta familia moja ina Wanachama wa CCM na wale wa CHADEMA kwahiyo usidhani kwamba ukosefu wa amani uko kwa wapinzani tu.

Bila shaka nia yako ilikuwa ni kuona leo watu wamepigwa risasi au kupigwa virungu na kujeruhiwa vibaya ama kufa. Huo ni uchochezi mbaya sana.

CHADEMA kama Chama kingine chochote cha SIASA wana haki ya kufanya maandamano ilimradi tu hawavunji Sheria na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Sasa unaposhabikia mabavu ya uonevu yanayofanywa na Serikali iliyoko madarakani usidhani kwamba ni sifa au inakusaidia chochote zaidi ya kuwa mwenye mawazo mgando.

Tukumbuke kuwa Nchi hii ilikubali kuanzishwa SIASA ya vyama vingi yenyewe mwaka 1992. Nakumbuka kipindi kile nikiwa mdogo ilipigwa kura ya maoni kama je Watanzania wanataka Siasa ya vyama vingi na 80% walitaka tubaki kwenye Siasa ya Chama Kimoja. Sasa Serikali yenyewe ama kwa shinikizo la IMF (Kupewa misaada) waliamua kuingia kwenye Siasa ya vyama vingi. Sasa kama tumekubali wenyewe kuingia kwenye Siasa hiyo, je ni kwanini tunawakandamiza wale raia walioamua kuwa vyama vya upinzani?

Nakumbuka Rais aliyepita Mhe. JK pamoja na mapungufu yake kama binadamu yeyote lakini aliweza kuongoza kwa kufuata Utawala wa Sheria/Katiba na aliweza kupambana na hawa wapinzani kwa kutumia hoja na si vitisho na kuwakandamiza. Kwa kutumia njia hii hii aliweza kuweka mkakati wa kutembea Nchi nzima (Kinana pamoja na Mhe. Nape) ili kukiimarisha Chama. Hii ndio njia inayopaswa kuigwa na Rais aliyeko madarakan.

Kutumia ubabe na mambo mengine ambayo sio ya msingi yanaturudisha nyuma kwa enzi za Chama kimoja ambazo kamwe hazitaweza kufanikiwa maana hizi ni dhama nyingine na karne tofauti kabisa. Pia namshauri Mheshimiwa Rais asitumia nguvu nyingi sana kuwabana wapinzani kwani wanampotezea sana muda wa kufanya shughuli za maendeleo na kutekeleza ilani ya CCM.
Mode mgepadisha hii note uko juu. Asante
 
Chenga za chadema uwanja wa siasa zimewaacha majerui na wengine kufa. Endeleeni na mazoezi/usafi. Tukutane Oct 1st.
 
Back
Top Bottom