mwengeso
JF-Expert Member
- Nov 27, 2014
- 9,286
- 6,727
Chadema hawajakurupuka.
Wamefanya kile kile walichokuwa wamedhamiria.
Kukoki watu kwa kuwahadaa na matamko ya operesheni hewa.
Ni hewa kwa sababu hakuna aliyekuwa na nia ya dhati ya kuandamana tangia mwanzo.
"A publicity stunt".
Ni kweli hawajakurupuka.
CHADEMA wamefanya kile kile walichokusudia, umenena wewe Jozi 1, nikiamini unaujua undani wa UKUTA.
Je, ni mafanikio gani ya "M4C"; "SANGARA"; Peoples Power!"; "mabadiliko lowasa - lowasa mabadiliko"; "UKUTA" na mengineyo ambazo ni baadhi ya kaulimbiu na operesheni za CHADEMA.
Kumbe huwa ni matamko, kaulimbiu na operesheni hewa. Tunashukuru wewe na wafuasi wa CHADEMA mnatambua hivyo. Basi CHADEMA ni chama cha siasa hewa, au viongozi ndiyo hewa, la wafuasi ni hewa.
Ni kweli hawakurupuka, ila kwa jamii iliyozungukwa na umaskini, katika nchi tajiri, uhewahewa wa aina hiyo unadhihirisha uwezo mdogo wa viongozi wa kisasa kuwatumikia.
Viongozi wa CHADEMA wajipange upya