Bado wapo wenye imani na CHADEMA?

Bado wapo wenye imani na CHADEMA?

Hawa CHADEMA ndo basi tena.

Naona wapo kwenye mwendokasi wa kuelekea kaburini.

Hii si mara yao ya kwanza kuwapandisha watu mzuka halafu wanaishia kubadili gia angani na kuwaacha watu wakining'inia.

Nani tena atawaamini hawa jamaa? Manake baada ya kuwaaminisha watu kwa miaka mingi kuwa Lowassa ni fisadi, matokeo yake ndo akaja kuwa mgombea wao. Mamlaka ya kimaadili ya kukemea ufisadi wakayapoteza.

Baada ya kuwapandisha watu mzuka wa UKUTA, leo wameufyata mbele ya Ngosha.

Sasa eti wametangaza hayo maandamano yatafanyika Oktoba mosi.

Watampata nani hiyo Oktoba mosi? Wake, waume, na watoto wao?

Wameishiwa kabisa. Hawana jipya tena. Hawana dira wala mwelekeo wowote ule.

Mtu afadhali unaweza kusema kuwa kabla ya ujio wa Lowassa kwamba watu walijua wanasimamia nini na wanasimama wapi.

Lakini leo hii nani anayejua wanachokisimamia? Nani anajua wanaposimama?

Walishindwa hata kuwashawishi wapinzani wenzao kuwaunga mkono ki hali na ki mali kwenye huo UKUTA wao. Wengine wakadiriki hadi kuwatakia kila la kheri na kuwaahidi kuchangia damu endapo wangehitaji baada ya kupokea kichapo cha vijana wa Ngosha.

Matokeo yake tingatinga limepita na kuusambaratishia mbali.

Wanahitaji uongozi mpya wenye maono mapya la sivyo wataenda bye bye for good.
Usikae nyuma ya keyboard ukapiga kelele mbaya zaidi tena nje ya nchi njoo fild
 
Naiamini mbinu wanayoitumia chadema kupinga uvunjaji wa katiba na sheria za nchi. Wangeandamana kesho wangeambiwa wamewaingilia JWTZ ambao ni serikali pengine wangekamatwa wananchi wengi wasio na hatia . Tukutane 1st October.
Chadema Mimi ni CCM niliyeamuwa kuwaunga mkono kwenye maandamano.
 
Tatizo kubwa la CDM ni kwamba ukiwaambia walifanya makosa kumsimamisha Lowasa Kama mgombea Wao wanakuita CCM, lakini ukweli unabaki pale pale kuwa like lilikuwa ni kosa kubwa, migogoro iliyopo CUF, NCCR na CDM yenyewe chanzo chake kikuu ni Hilo kosa.
CHADEMA Walitaka Publicity,na Wameipata!na Hata Kusema Kuwa Watumishi wa Mungu Kuwaomba Watulie Bado ni Kick Nzuri!
Na Mpaka Oktoba Mosi CHADEMA Haita Kauka Vinywani Mwenu!
Hivi Usafi Kesho Unaendelea,ahahaha!
CHADEMA Wametanguliza,wao Wamepiga Kona Fasta!
 
Imani ya chama huja kwenye maandamano migogoro mifarakano maridhiano sio mazur ktk vyama sisi tunataka minyukano hiyo ndo sifa ya upinzani amani haifai pakitokea maridhiano.
 
Usikae nyuma ya keyboard ukapiga kelele mbaya zaidi tena nje ya nchi njoo fild

Mbona nyie mlikuwa mnapiga kelele kwenye Instagram huko na siku moja kabla ya siku ya siku ujumbe umepenyeza.

Ona hawa wenzio....hivi kweli wamekaa hata mkao wa ku rumble hawa?

 
Hawa CHADEMA ndo basi tena.

Naona wapo kwenye mwendokasi wa kuelekea kaburini.

Hii si mara yao ya kwanza kuwapandisha watu mzuka halafu wanaishia kubadili gia angani na kuwaacha watu wakining'inia.

Nani tena atawaamini hawa jamaa? Manake baada ya kuwaaminisha watu kwa miaka mingi kuwa Lowassa ni fisadi, matokeo yake ndo akaja kuwa mgombea wao. Mamlaka ya kimaadili ya kukemea ufisadi wakayapoteza.

Baada ya kuwapandisha watu mzuka wa UKUTA, leo wameufyata mbele ya Ngosha.

Sasa eti wametangaza hayo maandamano yatafanyika Oktoba mosi.

Watampata nani hiyo Oktoba mosi? Wake, waume, na watoto wao?

Wameishiwa kabisa. Hawana jipya tena. Hawana dira wala mwelekeo wowote ule.

Mtu afadhali unaweza kusema kuwa kabla ya ujio wa Lowassa kwamba watu walijua wanasimamia nini na wanasimama wapi.

Lakini leo hii nani anayejua wanachokisimamia? Nani anajua wanaposimama?

Walishindwa hata kuwashawishi wapinzani wenzao kuwaunga mkono ki hali na ki mali kwenye huo UKUTA wao. Wengine wakadiriki hadi kuwatakia kila la kheri na kuwaahidi kuchangia damu endapo wangehitaji baada ya kupokea kichapo cha vijana wa Ngosha.

Matokeo yake tingatinga limepita na kuusambaratishia mbali.

Wanahitaji uongozi mpya wenye maono mapya la sivyo wataenda bye bye for good.
Logical deduction from this move ni kuwa hao wanaokutaka usitishe maandamano wanakuunga mkono! Ungelikuwa unafanya uhalifu wasingelikubembeleza usitishe, wangeliungana na serikali kukupiga mabomu!
 
Mtampiga vita NN
Lakini kawapa ushauri huu upinzani wa sasa umekatisha tamaa wengi

Hakuna agenda za kitaifa na nyeti za kuukuza upinzani na mkichelewa , JPM akianza kutekeleza ahadi zake moja baada ya nyingine mtapotea kabisa

Mnachotakiwa cdm , badilikeni

Zama zimebadilika
 
Naiamini mbinu wanayoitumia chadema kupinga uvunjaji wa katiba na sheria za nchi. Wangeandamana kesho wangeambiwa wamewaingilia JWTZ ambao ni serikali pengine wangekamatwa wananchi wengi wasio na hatia . Tukutane 1st October.
Chadema Mimi ni CCM niliyeamuwa kuwaunga mkono kwenye maandamano.
Nimepita Kwenda Social Networks Nyingi Nimegundua Haya:
a)Wana CCM Wameumia Sana Baada ya CHADEMA Kuhairisha UKUTA
b)Baadhi ya Wana CHADEMA Analojia Wamekasirishwa Na Uhairishwaji wa UKUTA!
c)Ila Wana CHADEMA Digitali Wengi Tunaopenda Siasa za Hoja Tumeipenda Hii Kete!
d)JWTZ Na Polisi Wataendelea na Usafi na Operesheni ya VIKINDU!
 
Hawa CHADEMA ndo basi tena.

Naona wapo kwenye mwendokasi wa kuelekea kaburini.

Hii si mara yao ya kwanza kuwapandisha watu mzuka halafu wanaishia kubadili gia angani na kuwaacha watu wakining'inia.

Nani tena atawaamini hawa jamaa? Manake baada ya kuwaaminisha watu kwa miaka mingi kuwa Lowassa ni fisadi, matokeo yake ndo akaja kuwa mgombea wao. Mamlaka ya kimaadili ya kukemea ufisadi wakayapoteza.

Baada ya kuwapandisha watu mzuka wa UKUTA, leo wameufyata mbele ya Ngosha.

Sasa eti wametangaza hayo maandamano yatafanyika Oktoba mosi.

Watampata nani hiyo Oktoba mosi? Wake, waume, na watoto wao?

Wameishiwa kabisa. Hawana jipya tena. Hawana dira wala mwelekeo wowote ule.

Mtu afadhali unaweza kusema kuwa kabla ya ujio wa Lowassa kwamba watu walijua wanasimamia nini na wanasimama wapi.

Lakini leo hii nani anayejua wanachokisimamia? Nani anajua wanaposimama?

Walishindwa hata kuwashawishi wapinzani wenzao kuwaunga mkono ki hali na ki mali kwenye huo UKUTA wao. Wengine wakadiriki hadi kuwatakia kila la kheri na kuwaahidi kuchangia damu endapo wangehitaji baada ya kupokea kichapo cha vijana wa Ngosha.

Matokeo yake tingatinga limepita na kuusambaratishia mbali.

Wanahitaji uongozi mpya wenye maono mapya la sivyo wataenda bye bye for good.
Vijana wamekula elfu arobaini bure
 
Kijana kukaa ukishabikia CDM ni kupoteza mda wako bure.
Japo tunaona serikali imekuwa ikivunja katiba hadharani lakini bado dioni haja ya kushabikia CDM, bora kukaa bila kusapoti upande wowote, kama wameshindwa kwenda kumtoa kiongozi mwenzao Salum Mwalimu hadi leo anasota lupango wakati viongozi kina mbowe ndio waliompa hio kazi na walaaniwe viongozi wote wa CDM.
Tazama leo tena wameufyata na UKUTA wao, kazi kupiga kelele tu wachumia tumbo wakubwa.
 
Back
Top Bottom