Bado tunakukumbuka Regia Mtema....

Bado tunakukumbuka Regia Mtema....

Balantanda

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2008
Posts
12,484
Reaction score
4,824
RM2.jpg




Leo ni miaka miwili tangu umetutoka mpendwa wetu Regia....Uliondoka mapema wakati bado Tanzania inakuhitaji....

Pamoja na kwamba kimwili haupo nasi lakini tupo nawe kiroho na bado tupo nawe kupitia maandiko na kauli/misimamo yako....

Binafsi nakuombea na kukumbuka kila wakati mpendwa wetu...

Daima tutakukumbuka dada yetu, mwalimu wetu, mwakilishi wetu na mpigania haki za wanyonge....

Mungu azidi kuipa nguvu na uvumilivu familia ya mzee Estellatus Mtema katika siku hii ambayo mpendwa wetu Regia alitutoka.....

Uendelee kupumzika kwa amani mpendwa wetu....

Raha ya milele umpe ee bwana, na mwanga wa milele umuangazie, Apumzike kwa Amani
...Amina.
 
Nilikuwa NAMPENDA SANA REGIA MTEMA...Mungu aendelee kuwapa uvumilivu familia, rafiki, jamaa na wanachama, wapenzi wa CHADEMA.
 
We miss you Regia.

Bahati mbaya ile chadema uliyoiacha kipindi kile, sio hii iliyopo sasa.
mambo yamebadilika mno.
viongozi wanatimuana, wanatukanana, wanapelekana mahakamani.
Matamko kila kukicha, wasemaji wa chama wamekuwa wengi.
Mwenyekii alikiri kuwa alipewa pesa na Nimrod Mkono yule mbunge tajiri wa CCM.

Chadema ile sio hii Regia. Rest in peace mpiganaji.
 
Duh umenikumbusha mbali sana! Mungu aiweke roho ya marehemu mahali pema peponi, amina!
 
We miss you Regia.

Bahati mbaya ile chadema uliyoiacha kipindi kile, sio hii iliyopo sasa.
mambo yamebadilika mno.
viongozi wanatimuana, wanatukanana, wanapelekana mahakamani.
Matamko kila kukicha, wasemaji wa chama wamekuwa wengi.
Mwenyekii alikiri kuwa alipewa pesa na Nimrod Mkono yule mbunge tajiri wa CCM.

Chadema ile sio hii Regia. Rest in peace mpiganaji.
Si pandizi na wasaaliti karma weye wamekuwa wengi,
 
Si pandizi na wasaaliti karma weye wamekuwa wengi,

Naombeni tusichafue hewa kwenye hii thread tafadhali....

Hayo mambo ya usaliti n.k fungueni thread mahsusi....

Hapa tunamkumbuka Mpendwa wetu Regia ...

Pls..
 
We miss you Regia.

Bahati mbaya ile chadema uliyoiacha kipindi kile, sio hii iliyopo sasa.
mambo yamebadilika mno.
viongozi wanatimuana, wanatukanana, wanapelekana mahakamani.
Matamko kila kukicha, wasemaji wa chama wamekuwa wengi.
Mwenyekii alikiri kuwa alipewa pesa na Nimrod Mkono yule mbunge tajiri wa CCM.

Chadema ile sio hii Regia. Rest in peace mpiganaji.

Chadema ni ile ile. Chadema ni moja. Chadema imeimarika zaidi. Regia amefariki hakuacha mgogoro wa madiwani Arusha ulioratibiwa kwa karibu kabisa na Zitto Zubeir Kabwe.
Regia amefariki hakumwacha Zitto Zubeir Kabwe akitumiwa na usalama wa taifa kukiharibu chama ambacho Regia alijitoa kukijenga.
Regia amefariki hakumwacha Zitto Zubeir Kabwe akitukana viongozi wakuu wa chama. Regia alifariki aliacha nidhamu kwa viongozi wake.
Sasa chadema inarudisha misingi yake. Inajenga timu inayowaza mamoja kuelekea kutwaa dola 2015. Inasafisha makapi,makandokando na mapandikizi yote ya CCM.
Chadema ni moja, mwenye kutaka ukombozi wa pili wa Mtanzania na aje!
 
Chadema ni ile ile. Chadema ni moja. Chadema imeimarika zaidi. Regia amefariki hakuacha mgogoro wa madiwani Arusha ulioratibiwa kwa karibu kabisa na Zitto Zubeir Kabwe.
Regia amefariki hakumwacha Zitto Zubeir Kabwe akitumiwa na usalama wa taifa kukiharibu chama ambacho Regia alijitoa kukijenga.
Regia amefariki hakumwacha Zitto Zubeir Kabwe akitukana viongozi wakuu wa chama. Regia alifariki aliacha nidhamu kwa viongozi wake.
Sasa chadema inarudisha misingi yake. Inajenga timu inayowaza mamoja kuelekea kutwaa dola 2015. Inasafisha makapi,makandokando na mapandikizi yote ya CCM.
Chadema ni moja, mwenye kutaka ukombozi wa pili wa Mtanzania na aje!

Fungua thread uelezee huu ujinga wako, hapo tuko kwenye kumbukumbu ya REGIA, sio mambo ya migogoro yenu!
 
Alale Pema Peponi Regia Mtema.

Nitakukumbuka daima.
 
Fungua thread uelezee huu ujinga wako, hapo tuko kwenye kumbukumbu ya REGIA, sio mambo ya migogoro yenu!

Mkuu CHOONI, Chadema ni moja. Chadema ni ya Watanzania. Chadema aliyoiacha Regia inazidi kuimarika. Regia hakuacha wahalifu wa kufifisha jitihada za kumkomboa Mtanzania.
Chadema ni njema, mwenye kutaka kuja Chadema na aje!
 
Nilimfahamia humu jf kupitia post fulani ya Mzee Mwanakijiji,
Nilipopandisha thread hii, Chadema Yakubali Yaishe! Yamtambua Rasmi JK!

Yeye alinishukia kwa thread hii, Pasco Tuombe radhi CHADEMA-

Hatimaye nikaomba rasmi msamaha! Nawaomba radhi wana CHADEMA,

From there tukawa marafiki
Na kwenye mazishi kule Kilombero, nilikuwa ni miongoni mwa jf team iliyomsindikiza hadi safari yake ya mwisho kwenye makao yake ya milele!.

RIP RM!.

Pasco

Safi sana Pasco....

Hakika Regia ni Hazina iliyotoweka wakati bado inahitajika na Taifa hili...

Ukisoma signature yangu utakumbana na maneno ambayo Regia aliwahi kuyazungumza wakati wa kutatua mojawapo ya migogoro ndani ya CHADEMA(I stand to be corrected)....Kutokana na maneno hayo mtu atatambua Regia ni mtu wa aina gani...

Regia alikuwa na moyo wa uthubutu...Alijitolea maisha yake na muda mwingi kupigania maslahi ya wasiojiweza/wanyonge....

Daima nitamkumbuka Gender Sensitive....Mungu azidi kumpa nguvu pacha wake Remija katika siku hii ya kifo cha mpendwa wetu...
 
Mkuu CHOONI, Chadema ni moja. Chadema ni ya Watanzania. Chadema aliyoiacha Regia inazidi kuimarika. Regia hakuacha wahalifu wa kufifisha jitihada za kumkomboa Mtanzania.
Chadema ni njema, mwenye kutaka kuja Chadema na aje!
Mkuu hapa tumzungumzie Regia zaidi na si mgawanyiko ndani ya CHADEMA....
 
Mkuu CHOONI, Chadema ni moja. Chadema ni ya Watanzania. Chadema aliyoiacha Regia inazidi kuimarika. Regia hakuacha wahalifu wa kufifisha jitihada za kumkomboa Mtanzania.
Chadema ni njema, mwenye kutaka kuja Chadema na aje!

Sawa Lakini huo ushabiki wako, hapa sio mahala pake!
 
Mkuu hapa tumzungumzie Regia zaidi na si mgawanyiko ndani ya CHADEMA....
Mkuu mimi nilikuwa namjibu huyu hapa chini. Aau yeye hamjamwona?

Ndibalema said:
We miss you Regia.

Bahati mbaya ile chadema uliyoiacha kipindi kile, sio hii iliyopo sasa.
mambo yamebadilika mno.
viongozi wanatimuana, wanatukanana, wanapelekana mahakamani.
Matamko kila kukicha, wasemaji wa chama wamekuwa wengi.
Mwenyekii alikiri kuwa alipewa pesa na Nimrod Mkono yule mbunge tajiri wa CCM.

Chadema ile sio hii Regia. Rest in peace mpiganaji
 
Can we please have a moment of silence?
As day comes and night falls
For the rest of our life we'll miss her
And even though life must go on, we'll still mourn.

can we have another moment of
silence?

For Pac, Biggie and Pun 'cause through us they live on Jam Master Jay, Freaky Tah and Aaliyah Big L and Left Eye.
 
Sawa Lakini huo ushabiki wako, hapa sio mahala pake!

Hakuna ushabiki, tafsiri ya ushabiki hutegemea mtu na mtu. Namwelezea Regia na Chadema yake. Sio rahisi kumtaja Mh. Regia bila kukitaja CDM. Alikitumikia chama kwa Mwili, akili na Roho yake. Kupitia Regia Watanzania wengi walinufaika. Ni bahati mbaya vizuri havidumu. Regia aliipenda CDM na CDM ilimpenda. Nina hakika Regia angekuwa hai leo angekuwa mstari wa mbele kufukuza wahuni waliotaka kuharibu chama. Asante Mungu amewafunua wahuni mapema kabla hawajatekeleza Ubaradhuli wao

Chadema ni njema, mwenye kutaka kuja na aje!
 
Kweli tumekumiss sana dada yetu ulikuwa ni kioo kwetu.
 
Back
Top Bottom