Bado nani sijamu UNFOLLOW Yanga?

Bado nani sijamu UNFOLLOW Yanga?

Hta kama mtu atarudi kuishabikia Yanga au kuendelea kuisapoti kwa namna yoyote ile, kuna sehemu ya funzo ambayo viongozi wa klabu watakuwa wamelipata.

Na hilo ndilo jambo la msingi mashabiki wanapolalamika, si kwa lengo la kuiacha timu kabisa, bali kuonyesha kuwa kuna mipaka ya kuvumilia maamuzi yasiyo na heshima kwao.

Kwa mfano, tupo kwenye kipindi cha kuelekea msimu mpya. Hiki ni kipindi ambacho klabu humtegemea sana shabiki kwa mambo kama:

  • Ununuzi wa jezi mpya
  • Tamasha la Siku ya Wananchi (kutambulisha wachezaji wapya)
  • Kujenga morali na hamasa ya msimu mpya
Sasa fikiria mashabiki wakisema: “Hatununui jezi, hatuhudhurii tamasha.” Halafu siku ya tukio inafika, uwanja uko nusu, jezi hazijauzwa, na hamasa iko chini unadhani viongozi hawatapokea ujumbe?
Mkuu wewe unaelewa ambacho sisi tunakipigania. Heshima taasisi na mipaka izingatiwe pia
 
Binafsi nilikua muwazi mapema sana kua Kwa hili la kuchangia chama viongozi wa yanga wamezingua pakubwa.

Lakini pia ndio tafsiri ya binadamu hatujakamilika tukiweka hilo pembeni viongozi hao hao wamefanya mengi mazuri tukafurahi na kushangilia pamoja

Narudia Tena sijaunga mkono Wala sijafurahishwa na hiki walichokifanya... Lakini kabla ya kutoa Kila aina ya povu tujiulize kwanza hakuna sehemu tuliwahi kukosea kama binadamu? Uongozi una Siri kubwa sana amazo huwezi kuweka zote hadharani tunapaswa kutazama Yale mazuri kutoka Kwa mtu tusitafute ukamilifu kwa binadamu.
 
Lakini pia ndio tafsiri ya binadamu hatujakamilika tukiweka hilo pembeni viongozi hao hao wamefanya mengi mazuri tukafurahi na kushangilia pamoja
Kukosea kupo ndio ila unapogundua umekosea inatakiwa urudi kuchutama na kuomba radhi. Hiyo ni ishara ya hekima na kutambua nini ulichokifanya na wapi ulipokosea
 
Nikiri wazi mimi ni shabiki wa Yanga kindakindaki kutoka moyoni. Lakini kwa hiki kilichofanyika imekua chukizo kwangu na kwa wengine wengi kama mimi. Najua wengine watabeza ila tayari nime unfollow kuanzia page ya Instagram mpaka viongozi wote wa Yanga.

Katika wakati kama huu hawakupaswa kutugawa hivi. Nakiri wazi nitabaki kuwa shabiki wa mpira kwa kuangalizia mabanda umiza tu, hata jezi sinunui mmetukera sana viongozi.
Shame Shame Shame.
Oko sahihi,ila wasamehe nadhani wamejifunza hawatarudia siyo Kila kitu kutafuta kiki,ingekuwa heri kama wangeenda viongozi na kutoa michango binafsi na siyo taasisi.piga moyo konde wasamehe huko huwenda na ccm wakaja kutuchangia kujenga uwanja wetu.
 
Back
Top Bottom