Babu wa loliondo amaliza watu Visiga

Babu wa loliondo amaliza watu Visiga

Jamani mniwie radhi.Hili siwezi kulinyamazia.Babu wa Loliondo 'ameshaua' watu wanne waliotoka kwake kupata kikombe katika Mtaa wa Visiga Kati,Kibaha Pwani.Watu hao ambao wote walikwenda kwa Babu wakiwa na afya ya kawaida,wamefariki kwa kufuatana.Majina ya Marehemu wote ninayo.Arobaini ya mmoja wao ni leo.Naiomba Serikali itamke tena kuhusu tiba hii ya Babu kuwa au kutokuwa na uwezo wa kuponya magonjwa yanayopigiwa upatu kuponywa:UKIMWI,Kisukari na Kansa.Wapo wengine wawili hapohapo ni taabani.Muda ukipita hivi,Serikali itawajibika.Kweli tena...

DUH! POLE MDAU KWA KILIO CHAKO
>>> ILA NASIKITIKA KUKUAMBIA KWA TAARIFA YAKO HIYO SERIKALI UNAYOSHTAKIA VIONGOZI WAKE WOTE WASHAENDA KWA BABU!!!!!!!!!!!!!!! :mod: SASA SIJUI NANI UTAMHUKUMU BABU WAKATI ALISHATIBIWA NA YEYE!!!
 
Dawa ya babu haitibu wala haiponyi, ukweli ni kwamba , wabunge, mawaziri , wanaamini sana ushirikina ndiyo maana wamepotosha serikali.
Babu amefanikiwa kuifanya serikali iamini ushirikina lakini sasa ukweli umeanza kudhihirika. Babu amefanikiwa kuhamisha hoja za maandamano ya kuondoa serikali madarakani.
Hakuna asiyejua kuwa babu ni mganga wa kienyeji na tapeli , hatuhitaji tamko la serikali.
Serikali ilikataa kwamba rostam siyo fisadi lakini leo wanajivua gamba.
 
Wapo wengine wengi wamekunywa wapo fit majina tunayo mfano Mrema wa TLP.Pole kwa wafiwa na mungu awapumzishe kwa amani waliotangulia.Sote tusafari moja!
umemwona kama yuko fiti au unajibu 2. uliza sasa uambiwe kisugar chake kinavyopanda sasa!
 
hizi Like zime jam nini nawagongea like @ PakaJimmy, Mlachake naSaid Bagile
 
Kwanza natoa pole zangu kwa wafiwa wote, wametangulia nasi tupo nyuma yao. swala zima la kujua ni kipi kilichosababisha kifo bado lipo
wazi, Tusemee swala na utamaduni wa kujua sababu iliyosababisha kifo kisayansi bado hatunalo kwa nchi yetu na africa kwa ujumla.
Kwani ccm wameweka mbele ufisadi na siasa zao uchwara. Na bila kujali afya za wananchi. na katika muono wangu vifo vya namna hiyo
vitakuwa vinaingiliana na magonjwa ya kuambukiza na haswa Kipindupindu. Na ukiangalia watu hao wametoka katika sehemu ya
mkusanyiko wa watu na njiani walimopita kuna vyakula walivyonunua vinaweza kusababisha magonjwa ya mlipuko, kwa sababu vifo
vya namna hiyo si vya kawaida, miili yao inafaa ichunguzwe ni kitu gani kilichosababisha kabla haijazikwa. Na kuweza kutoa tahadhali
kwa wengine.
 
Waliokwenda kwa ujumla ni watu nane kwa safari ya kwanza.Wakakaa karibu miezi mitatu ndipo walipoanza kufa mmoja baada ya mwingine.Waliosalia kwa safari ya kwanza ni wanne,nao ni wagonjwa sana.Wako wengine walikwenda kwa safari ya pili.Sasa wamejaa mashaka mno.Ni kweli kufa hakuzuiwi na Tiba ya Babu.Lakini,ndio wafe waliokwenda huko tu?! Hivi Mrema ndio yuko fit kweli? Ndio kipimo cha wote kweli? Hilisi jambo la mzaha hata kidogo....it is a serious issue than you can cheaply imagine.

Sorry for those who died..but the way you put it in the first place is as if you are condemning BABU and his medication. For your information, that does not only happen at your place , it is a problem to most people who went there, even in my home place. ButI I tell you, my simple research found that, all those who went to BABU and died were at a critical stage of infirmity. So, it is not that whoever goes to BABU dies at the end, it is that they either do not comply with the previously prescribed medication or they don't have faith at all.

Thank you
 
heheheee, naona babu aligundua style ya kuamua kuwamaliza wagonjwa wa UKIMWI ili maambukizi yapungue. Pole yao waliokwenda.
 
Jamani mniwie radhi.Hili siwezi kulinyamazia.Babu wa Loliondo 'ameshaua' watu wanne waliotoka kwake kupata kikombe katika Mtaa wa Visiga Kati,Kibaha Pwani.Watu hao ambao wote walikwenda kwa Babu wakiwa na afya ya kawaida,wamefariki kwa kufuatana.Majina ya Marehemu wote ninayo.Arobaini ya mmoja wao ni leo.Naiomba Serikali itamke tena kuhusu tiba hii ya Babu kuwa au kutokuwa na uwezo wa kuponya magonjwa yanayopigiwa upatu kuponywa:UKIMWI,Kisukari na Kansa.Wapo wengine wawili hapohapo ni taabani.Muda ukipita hivi,Serikali itawajibika.Kweli tena...
Hao jirani zako walikuwa "terminally ill" yaani walikwisha fikia ukomo wa maisha.
Inaelekea ndio hao ambao bila kikombe wangekuwa wamekufa kitambo!!
 
Kama ulikuwa mwizi,mchawai au ushawai kuua ukinywa kikombe ni kifo.Nina ushaidi wa watu watatu ninaowafahamum
Mzee alikuwa na sukari yuko fit mpaka leo mwezi wa tatu sasa
 
sikweli kuwa wanaokwenda kwa babu wakafa ati wanakasoro za kiimani. nachojua ni kwamba, walifuata matatizo wao wenyewe. Ninaushahidi wa mfanyakazi mmoja wa benk yetu aliyeaga dunia ghafla baada ya wiki chache za kutoka kwa babu. Na alikuwa na afya yake nzuri tu. Kwa kweli babu atamaliza wengi.
 
Pole sana ndugu yangu huyu mzee wa Loliondo ni Mwizi sana! Dawa zake zinazidi kumaliza watu
 
Sorry for those who died..but the way you put it in the first place is as if you are condemning BABU and his medication. For your information, that does not only happen at your place , it is a problem to most people who went there, even in my home place. ButI I tell you, my simple research found that, all those who went to BABU and died were at a critical stage of infirmity. So, it is not that whoever goes to BABU dies at the end, it is that they either do not comply with the previously prescribed medication or they don't have faith at all.Thank you
Faith, ooh! faith in what ? in magic ?
 
Kama ulikuwa mwizi,mchawai au ushawai kuua ukinywa kikombe ni kifo.Nina ushaidi wa watu watatu ninaowafahamumMzee alikuwa na sukari yuko fit mpaka leo mwezi wa tatu sasa
Sio kweli, mbona MAFISADI wamekunywa 'mbozyo' kwa babu wala hawana imani lakini bado wapo wanafisidi nchi.
 
"AMELAANIWA MTU YULE AMTEGEMEAE MWANADAMU" HOSEA 4:6 "watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa".
 
Nawapa pole wafiwa, ila mtoa hoja, unafahamu kuwa maralia ina dawa? Lakini bado inaongoza kwa kuuwa! Babu sio ndio kaja kuondoa kifo, kifo kitaendelea kuwepo tuuuuuu
 
Kuna watu wanafanyiwa upasuaji wa kisayansi na bado wanakufa. Cha msingi hapa, ni kwamba kikombe akizuii kifo na magonjwa huweza kuleta kifo pia. Kama ambavyo mtu anaweza kuwa mgonjwa kiasi upasuaji usifanikiwe ndio hivo hivo kikombe kinaweza kuwa na kiasi kisichotosha kuponesha.

Tafiti kadhaa zinaonesha kikombe kinaweza kuwa na kiasi pungufu, sahihi au kilichozidi kulingana na stage ya ugonjwa husika. Ni katika hili mtu hupona, huendelea kuumwa au hufa. Na ukweli wengi wa wanaokufa ni wale waliofikia hali mbaya sana ktk magonjwa yao. Je wanywe vikombe viwili au vitatu?? Hili ndilo linapswa kuzungumziwa. Sio kusema dawa wa babu inaua!!
 
Kama ulikuwa mwizi,mchawai au ushawai kuua ukinywa kikombe ni kifo.Nina ushaidi wa watu watatu ninaowafahamum
Mzee alikuwa na sukari yuko fit mpaka leo mwezi wa tatu sasa

Duh! Kwa hiyo hata magamba waliopiga kikombe wako fit kiroho? Basi nadhani ni kwa viwango vya babu na si MUNGU nimuabuduye mimi. Yeye huwafunika kwa neema watu wake kwani wote tumetenda dhambi. Yeye alikuja ili wawe na uzima, si vinginevyo. POleni na mungu wenu babu
 
Back
Top Bottom