Babu wa loliondo amaliza watu Visiga

Babu wa loliondo amaliza watu Visiga

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,006
Jamani mniwie radhi.Hili siwezi kulinyamazia.Babu wa Loliondo 'ameshaua' watu wanne waliotoka kwake kupata kikombe katika Mtaa wa Visiga Kati,Kibaha Pwani.Watu hao ambao wote walikwenda kwa Babu wakiwa na afya ya kawaida,wamefariki kwa kufuatana.Majina ya Marehemu wote ninayo.Arobaini ya mmoja wao ni leo.Naiomba Serikali itamke tena kuhusu tiba hii ya Babu kuwa au kutokuwa na uwezo wa kuponya magonjwa yanayopigiwa upatu kuponywa:UKIMWI,Kisukari na Kansa.Wapo wengine wawili hapohapo ni taabani.Muda ukipita hivi,Serikali itawajibika.Kweli tena...
 
Jamani mniwie radhi.Hili siwezi kulinyamazia.Babu wa Loliondo 'ameshaua' watu wanne waliotoka kwake kupata kikombe katika Mtaa wa Visiga Kati,Kibaha Pwani.Watu hao ambao wote walikwenda kwa Babu wakiwa na afya ya kawaida,wamefariki kwa kufuatana.Majina ya Marehemu wote ninayo.Arobaini ya mmoja wao ni leo.Naiomba Serikali itamke tena kuhusu tiba hii ya Babu kuwa au kutokuwa na uwezo wa kuponya magonjwa yanayopigiwa upatu kuponywa:UKIMWI,Kisukari na Kansa.Wapo wengine wawili hapohapo ni taabani.Muda ukipita hivi,Serikali itawajibika.Kweli tena...

Wapo wengine wengi wamekunywa wapo fit majina tunayo mfano Mrema wa TLP.
Pole kwa wafiwa na mungu awapumzishe kwa amani waliotangulia.
Sote tusafari moja!
 
tueleze pia jumla wameenda watu wangapi kutoka hapo visga?
Wanagapi kati yao wamekufa baada ya kupata kikombe na wamekufa muda gani baada ya kupata kikombe?
Wangapi hawajafa na hali zao zikoje kiafya?
 
Jamani mniwie radhi.Hili siwezi kulinyamazia.Babu wa Loliondo 'ameshaua' watu wanne waliotoka kwake kupata kikombe katika Mtaa wa Visiga Kati,Kibaha Pwani.Watu hao ambao wote walikwenda kwa Babu wakiwa na afya ya kawaida,wamefariki kwa kufuatana.Majina ya Marehemu wote ninayo.Arobaini ya mmoja wao ni leo.Naiomba Serikali itamke tena kuhusu tiba hii ya Babu kuwa au kutokuwa na uwezo wa kuponya magonjwa yanayopigiwa upatu kuponywa:UKIMWI,Kisukari na Kansa.Wapo wengine wawili hapohapo ni taabani.Muda ukipita hivi,Serikali itawajibika.Kweli tena...
Tiba ya babu si ya kuzuwia kufa...ni tiba ya magonjwa!
Mtu wa kufa atakufa tu...tusikanganye watu kwa maneno yenye hisia zaidi kuliko utafiti!
 
Ninaachoona hapa ni fitina tu kwani kumuita babau wa loliondo ndiye kawaua hao watu si kweli. Inawezekana hata wasingekwenda kwa babu wangekufa na si kwamba kwa babu walikunywa sumu ndio maana wamekufa. Kijijini kwangu watu wote waliokwenda wamepona na kama unavyojua ukienda kwa babu na imani mbili huponi kwani lazima uende ukiamini kwamba ukinywa kile kikombe mambo yako yatakuwa safi. We fikiria unampeleka mtu yuko mahututi na aelewi yuko wapi ni vigumu kupona kwa sababu mtu huyo hana fahamu za ku-exercise faith. Hafikiri wengi waliokufa ni watu ambao ufahamu wao ku-exercise faith ulikuwa umepotea au mtu aliekwenda tayari amekata tamaa na pale akaenda kama formality basi huyo ni vigumu kupona. Hivyo ndivyo ninavyo amini na correct me if I'm wrong.
 
Waliokwenda kwa ujumla ni watu nane kwa safari ya kwanza.Wakakaa karibu miezi mitatu ndipo walipoanza kufa mmoja baada ya mwingine.Waliosalia kwa safari ya kwanza ni wanne,nao ni wagonjwa sana.Wako wengine walikwenda kwa safari ya pili.Sasa wamejaa mashaka mno.Ni kweli kufa hakuzuiwi na Tiba ya Babu.Lakini,ndio wafe waliokwenda huko tu?! Hivi Mrema ndio yuko fit kweli? Ndio kipimo cha wote kweli? Hilisi jambo la mzaha hata kidogo....it is a serious issue than you can cheaply imagine.
 
Waliokwenda kwa ujumla ni watu nane kwa safari ya kwanza.Wakakaa karibu miezi mitatu ndipo walipoanza kufa mmoja baada ya mwingine.Waliosalia kwa safari ya kwanza ni wanne,nao ni wagonjwa sana.Wako wengine walikwenda kwa safari ya pili.Sasa wamejaa mashaka mno.Ni kweli kufa hakuzuiwi na Tiba ya Babu.Lakini,ndio wafe waliokwenda huko tu?! Hivi Mrema ndio yuko fit kweli? Ndio kipimo cha wote kweli? Hilisi jambo la mzaha hata kidogo....it is a serious issue than you can cheaply imagine.

Si Mrema tu wapo wengine hapa ofisini kwetu kuna watu zaidi ya kumi wamenda na wapo fit.
Sio mzaa nimetoa mfano wa MREMA kwa sababu alikuwa haishi kulazwa KCMC sasa hivi anadunda kutwa yupo bungeni
 
Wapo wengine wengi wamekunywa wapo fit majina tunayo mfano Mrema wa TLP.
Pole kwa wafiwa na mungu awapumzishe kwa amani waliotangulia.
Sote tusafari moja!

wengine wajanja kaka hawaachi dawa zao walizoandikiwa na dkr
 
Haiwezekani wapone watanzania wote!wengine hao wlikuwa wakufa tu!Dawa ya Malaria SP ilivyoingia watu walikufa wengi kuliko hao uliowasema,na bado inatumika mpaka leo!wenye alergy za ajabu ajabu walitakiwa kujiepusha!sie watafit tunasema mtaukio uliyoripoti ARE NOT STATISTICALLY SIGNIFICANT (p
 
Si Mrema tu wapo wengine hapa ofisini kwetu kuna watu zaidi ya kumi wamenda na wapo fit.
Sio mzaa nimetoa mfano wa MREMA kwa sababu alikuwa haishi kulazwa KCMC sasa hivi anadunda kutwa yupo bungeni

Kwa babu wajinga ndiyo waliwao hakuna cha kupona kwani wamejazwa maroho machafu na ndiyo yanayowaua, hao unaosema wako fit inawezekana unaona wako fit kimwili lakini kiroho ni marehemu. Kwani maisha ni hapa duniani tu? Ni vizuri kupona mwili lakini mtu apone katika msingi ya kisayansi au kuombewa kwa jina la Yesu ili abaki katika mpango wa Mungu ili akifa aende mbinguni. Lakini kwa watu wa ndoto na maono hao ni fungu moja na wachawi,na waganga na Mungu wao ni shetani ambaye kwake ahkuna msamiati wa uponyaji
 
wengine wajanja kaka hawaachi dawa zao walizoandikiwa na dkr

Kama ndiyo hivyo kwa babu walikwenda kufanya nini si wangeendelea na dawa zao tu. Kuendelea kupigia debe ndoto za babu wa Loliondo ni kujidhalilisha na kuwadhalilisha watanzania kwamba sisi ni watu wa njozi na by the way a great thinker really thinks greatly and can never be swayed by unsubstantiated illusions
 
Hivi?
Kama ile dawa ya yule mzee inauwa, Leo si tungekua tuna janga la kitaifa?

Ukiniuliza kama ile dawa inaponya nitakwambia sijui! Lakini ukiniuliza kama inaua nitakwambia hapana, Kwasababu watu wato ninaowajua wamekunywa bado wako hai, ila kupona sijui kwasababu mimi sio daktari.
 
Jamani mniwie radhi.Hili siwezi kulinyamazia.Babu wa Loliondo 'ameshaua' watu wanne waliotoka kwake kupata kikombe katika Mtaa wa Visiga Kati,Kibaha Pwani.Watu hao ambao wote walikwenda kwa Babu wakiwa na afya ya kawaida,wamefariki kwa kufuatana.Majina ya Marehemu wote ninayo.Arobaini ya mmoja wao ni leo.Naiomba Serikali itamke tena kuhusu tiba hii ya Babu kuwa au kutokuwa na uwezo wa kuponya magonjwa yanayopigiwa upatu kuponywa:UKIMWI,Kisukari na Kansa.Wapo wengine wawili hapohapo ni taabani.Muda ukipita hivi,Serikali itawajibika.Kweli tena...

Kuhusu Dawa ya Babu kama inatibu au haitibu sina maelezo, ila ieleweke kuwa Babu ameshasema hana uwezo wa kuzuia ''KIFO'' hili ni lamsingi sana kujulikana kwa wale wote wanaokwenda kwa Babu. Maana kuna watu wapo mahututi au magojwa yao yamefikia hatua mbaya lakini wanaona BABU ndiye anayeweza kuwafanya waepuke kifo. Mimi binafsi nina ndugu wakaribu ambao walikwenda wakisumbuliwa na Kisukari lakini baada ya kurudi hali zao ziliimalika japo pia kuna waliokwenda waliporudi hawakukaa sana wakaaga dunia, sasa kinachotakiwa kueleweka kwa jamii hii ni kuwa, Dawa ya Babu haina nguvu ya kimiujiza ni dawa kama dawa za HOSPITALINI ambazo hata zenyewe pamoja na utafiti na uhakika wa kuponyesha magonjwa lakini hazijawahi kuzuia kifo zaidi ya kusogeza muda wa kufa. Hivyo watu wajue kufa kwa mwanadamu ni lazima.
 
Jamani mniwie radhi.Hili siwezi kulinyamazia.Babu wa Loliondo 'ameshaua' watu wanne waliotoka kwake kupata kikombe katika Mtaa wa Visiga Kati,Kibaha Pwani.Watu hao ambao wote walikwenda kwa Babu wakiwa na afya ya kawaida,wamefariki kwa kufuatana.Majina ya Marehemu wote ninayo.Arobaini ya mmoja wao ni leo.Naiomba Serikali itamke tena kuhusu tiba hii ya Babu kuwa au kutokuwa na uwezo wa kuponya magonjwa yanayopigiwa upatu kuponywa:UKIMWI,Kisukari na Kansa.Wapo wengine wawili hapohapo ni taabani.Muda ukipita hivi,Serikali itawajibika.Kweli tena...

Mbona tunashindwa kuwa Great Thinkers,kwani nani alisema kikombe cha babu kinazuia kifo ?! kwa bahati mbaya sana binafsi kuna watu ambao sijui wangeona hii post yako wangekutendaje,kwani wakikumbusha maisha kabla ya kikombe yalivyokuwa yamejaa mateso na maisha baada ya kikombe,hakika watakulaani,binafsi mama mkwe wangu ambaye sukari na moyo kupanuka ilimfanya awe na maisha ya kitandani karibu kila siku atakushangaa na kukusikitia sana,ni bahati mbaya sana wote waliotumia kikombe hawana uwezo wa kuandika shuhuda zao JF,lakini shuhuda nyingi zingetolewa hapa,waliopona ni wengi sana ukilinganisha na hao waliokufa ambao wangekufa anyway kwani hata waliopona sasa bado watakufa.Let us think Great...
 
Na 2tambuwe kwamba ukienda kwa Babu ukiwa na mambo yako ya kichawi,kinafiki hakika itakula kwako tu. Inatakiwa uende na uwe umejitakasa. Wengi wameenda na wakapigwa STOP wasiguse KIKOMBE na wakang'ang'ania na hatima yao ni kutangulia kaburi. Kwa mfano hapa kwe2 Arusha Mjini kuna mama mmoja alienda na kupigwa STOP akiambiwa akajirekebishe ndiyo aje lakini akazunguka upande wa pili na akapata kikombe akaambiwa okey umeng'ang'ania kunywa haya nenda zako. Baada ya wiki 3 kwenda ya 4 kapatwa na ugonjwa wa ghafla na ikampiga chini na baada ya mazishi niliohudhuria mimi na washikaji hakika mama huyo kazikwa na baada ya muda kama saa kumi na moja jioni kwa sabbu yule mama ni mkristo na aliwekewa msalaba ikiwa ishara ya ukombozi, hakika msalaba ikaanza kuungua moto mpaka ikaisha yote wa2 walijitahidi kuuzima bila ya mafanikio. Kwa hiyo mambo ya kule Samunge ni ya IMANI tu. NAWAKILISHA!
 
Jamani mniwie radhi.Hili siwezi kulinyamazia.Babu wa Loliondo 'ameshaua' watu wanne waliotoka kwake kupata kikombe katika Mtaa wa Visiga Kati,Kibaha Pwani.Watu hao ambao wote walikwenda kwa Babu wakiwa na afya ya kawaida,wamefariki kwa kufuatana.Majina ya Marehemu wote ninayo.Arobaini ya mmoja wao ni leo.Naiomba Serikali itamke tena kuhusu tiba hii ya Babu kuwa au kutokuwa na uwezo wa kuponya magonjwa yanayopigiwa upatu kuponywa:UKIMWI,Kisukari na Kansa.Wapo wengine wawili hapohapo ni taabani.Muda ukipita hivi,Serikali itawajibika.Kweli tena...

Kama ni mchawi ukienda kwa babu kupiga ki-cup huponi ndugu lazima ufe!!!
 
Wapo wengine wengi wamekunywa wapo fit majina tunayo mfano Mrema wa TLP.
Pole kwa wafiwa na mungu awapumzishe kwa amani waliotangulia.
Sote tusafari moja!
Nina Mdogo wangu aliyekuwa na kifafa ambacho alikuwa kwa wiki si chini ya mara moja lazima aanguke. Lakini tangu arudi toka kwa Babu March mwaka huu mpaka leo hajawahi kuanguka na anaendelea kukata Kili yake bariiiiiiiiiiid billa wasiwasi wowote na leo tunakwenda kula nae Mbusi saaafi pale Marangu bar Kimara.
 
Waliokwenda kwa ujumla ni watu nane kwa safari ya kwanza.Wakakaa karibu miezi mitatu ndipo walipoanza kufa mmoja baada ya mwingine.Waliosalia kwa safari ya kwanza ni wanne,nao ni wagonjwa sana.Wako wengine walikwenda kwa safari ya pili.Sasa wamejaa mashaka mno.Ni kweli kufa hakuzuiwi na Tiba ya Babu.Lakini,ndio wafe waliokwenda huko tu?! Hivi Mrema ndio yuko fit kweli? Ndio kipimo cha wote kweli? Hilisi jambo la mzaha hata kidogo....it is a serious issue than you can cheaply imagine.
ni lazima wajae mashaka inawezekana wote walipanga njama "kumjaribu babu" so imekula kwao .ofkoz washauri wapigwe sala ya toba wlobaki hai ili wafe kifo kitakatifu. kuhusu wenye nguvu za giza kujitaksa kwanza ni very true kwani yupo mama mmoja after kunywa on da way home kichaa hadi leo NI KWELI NA AMINA
 
Back
Top Bottom