Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,174
Babu Loliondo awaonya wanaomuiga
Imeandikwa na Na Grace Chilongola, Loliondo;
Tarehe: 15th April 2011
MCHUNGAJI Ambilikile Masapila wa Kijiji cha Samunge Loliondo maarufu kama Babu, amewataka wananchi wajihadhari na matapeli wanaoibuka na kudai wanatoa tiba ya kikombe kama ya kwake.
Pia alisema maofisa wanaotumia fursa ya utoaji wa vibali vya kwenda kwake kunywa dawa (kikombe) kwa kujinufaisha na rushwa, ni maadui wa Mungu na kwamba fedha wanazopokea zitaisha bila kufanyia kitu cha maana na wao kubaki hohehahe.
Aliyasema hayo Alhamisi wakati akizungumza na timu ya waandishi wa habari kutoka mkoani Mwanza waliomtembelea nyumbani kwake Samunge, wilayani Ngorongoro kuona adha mbalimbali wanayoipata abiria wanaokwenda kwa ‘Babu' kupata tiba ya kikombe.
"Wananchi wajihadhari na watu wa sehemu nyingine wanaodai wameoteshwa na Mungu na kutoa tiba ya kikombe, ni matapeli tena wauaji," alisema na kuwaonya wananchi kujihadhari nao.
Alidai, wakati Mungu anamuotesha dawa hiyo alikuwa peke yake, watu wanaompinga wakiwemo wachungaji wa madhehebu mengine, wanapingana na Mungu aliyempa dawa ya kuponya watu bila kujali itikadi zao, dini, kabila au vyama vyao vya siasa.
"Wanaotoa vibali katika njia yoyote waache kutumia nafasi hiyo kujipatia utajiri kwa rushwa, yeyote anayefanya hivyo hela anayoipata haitamsaidia, atafilisika na kuwa na hali ambayo hajawahi kuipata maishani," alieleza Mchungaji Mwasapile.
Awali msimamizi wa Kituo cha tiba cha babu aliyejitambulisha kwa jinala Fredrick Nsajile aliwaambia waandishi hao kuwa wananchi wafuate utaratibu uliowekwa na serikali bila kutoa rushwa na waratibu wa safari katika vituo mbambali watende haki.
Nsajile alieleza kwamba, Mchungaji Mwasapile hapendi wagonjwa wasafirishwe kwa malori, wanaumia na kuteseka sana njiani na kudai kuna baadhi ya magari yanayotoa rushwa ambayo yanaonekana kupendelewa kuruhusiwa mara kwa mara kupeleka wagonjwa Samunge.
Msimamizi huyo alieleza kuwa, idadi ya watu wanaopata tiba (kunywa kikombe) kwa siku wanafikia 8,000 na sio 2,000 kama ambavyo vyombo vya habari vimekuwa vikieleza.
Wakiwa katika ziara ya kumtembelea babu waandishi hao walishuhudia malori zaidi ya manane wilayani Serengeti mkoani Mara likiwemo maalum kwa ajili ya kubeba samaki yakiwa yamebeba watu na kuwatelekeza kwenye mageti kwa zaidi ya wiki baada ya kukosa kibali cha kuwavusha.
Imeandikwa na Na Grace Chilongola, Loliondo;
Tarehe: 15th April 2011
MCHUNGAJI Ambilikile Masapila wa Kijiji cha Samunge Loliondo maarufu kama Babu, amewataka wananchi wajihadhari na matapeli wanaoibuka na kudai wanatoa tiba ya kikombe kama ya kwake.
Pia alisema maofisa wanaotumia fursa ya utoaji wa vibali vya kwenda kwake kunywa dawa (kikombe) kwa kujinufaisha na rushwa, ni maadui wa Mungu na kwamba fedha wanazopokea zitaisha bila kufanyia kitu cha maana na wao kubaki hohehahe.
Aliyasema hayo Alhamisi wakati akizungumza na timu ya waandishi wa habari kutoka mkoani Mwanza waliomtembelea nyumbani kwake Samunge, wilayani Ngorongoro kuona adha mbalimbali wanayoipata abiria wanaokwenda kwa ‘Babu' kupata tiba ya kikombe.
"Wananchi wajihadhari na watu wa sehemu nyingine wanaodai wameoteshwa na Mungu na kutoa tiba ya kikombe, ni matapeli tena wauaji," alisema na kuwaonya wananchi kujihadhari nao.
Alidai, wakati Mungu anamuotesha dawa hiyo alikuwa peke yake, watu wanaompinga wakiwemo wachungaji wa madhehebu mengine, wanapingana na Mungu aliyempa dawa ya kuponya watu bila kujali itikadi zao, dini, kabila au vyama vyao vya siasa.
"Wanaotoa vibali katika njia yoyote waache kutumia nafasi hiyo kujipatia utajiri kwa rushwa, yeyote anayefanya hivyo hela anayoipata haitamsaidia, atafilisika na kuwa na hali ambayo hajawahi kuipata maishani," alieleza Mchungaji Mwasapile.
Awali msimamizi wa Kituo cha tiba cha babu aliyejitambulisha kwa jinala Fredrick Nsajile aliwaambia waandishi hao kuwa wananchi wafuate utaratibu uliowekwa na serikali bila kutoa rushwa na waratibu wa safari katika vituo mbambali watende haki.
Nsajile alieleza kwamba, Mchungaji Mwasapile hapendi wagonjwa wasafirishwe kwa malori, wanaumia na kuteseka sana njiani na kudai kuna baadhi ya magari yanayotoa rushwa ambayo yanaonekana kupendelewa kuruhusiwa mara kwa mara kupeleka wagonjwa Samunge.
Msimamizi huyo alieleza kuwa, idadi ya watu wanaopata tiba (kunywa kikombe) kwa siku wanafikia 8,000 na sio 2,000 kama ambavyo vyombo vya habari vimekuwa vikieleza.
Wakiwa katika ziara ya kumtembelea babu waandishi hao walishuhudia malori zaidi ya manane wilayani Serengeti mkoani Mara likiwemo maalum kwa ajili ya kubeba samaki yakiwa yamebeba watu na kuwatelekeza kwenye mageti kwa zaidi ya wiki baada ya kukosa kibali cha kuwavusha.