Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,504
- 911,249
- Thread starter
- #21
Hofu ya vifo yatanda kwa Babu
na David Frank, Arusha
HOFU ya kutokea kwa vifo tena katika kijiji cha Samunge, wilayani Ngorongoro imeanza kupanda baada ya ongezeka la idadi ya watu na wagonjwa kwa kile kilichoelezwa hali hiyo imetokana na kituo cha Bunda kulegeza masharti.
Habari zilizopatikana na kuthibitishwa na baadhi ya wadau wa habari zimeeleza kituo cha Bunda kiliwaachia watu na wagonjwa wengi kupita bila udhibiti wowote tangu Alhamisi iliyopita na kusababisha msongamano mkubwa katika kijiji cha Samunge huku msururu wa magari ukifikia kijiji cha Yandito.
Hazi hizo zimeeleza kutokana na msongamano uliyopo, ni wazi vifo vinaweza kutokea katika eneo hilo kwani hakuna uwezekano wa mgonjwa kupata tiba ndani ya siku mbili huku uhaba wa chakula na uchafuzi wa mazingira ukiendelea kuongezeka.
Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro, Elias Wawa Lali, alithibitisha kuwepo kwa hali hiyo huku akiwatahadharisha wagonjwa ambao hawajaanza safari kusitisha mara moja, kwani watakachokipata huko ni mateso ya siku zaidi ya mbili badala ya kusubiri wakiwa katika miji kunakopatikana huduma zote muhimu.
"Hali si shwari, Bunda wanadai wamelegeza masharti eti wamechoka kulaumiwa, sasa hali huku ni mbaya yawezekana kutokea tena kwa maafa na matatizo mengine makubwa …ni vizuri wale ambao hawajaanza safari wasitishe kwanza na sisi tumesimamisha safari kwa vituo vya Arusha na Babati kusubiri hali iwe nzuri," alisema Lali.
Aidha, baadhi ya watu waliozungumzia hali hiyo wameutoa shutuma zao kwa viongozi wanaosimamia kituo cha Bunda na kudai iwapo hali hiyo itaendelea basi vifo visivyotarajiwa vitatokea na tiba hiyo itakuwa katika mashaka.
"Naamini iwapo taratibu zitafuatwa hakuna tena wasiwasi wala mashaka juu ya tiba ya mchungaji huyo…vipi tena watu wa Kanda ya Ziwa wavunje utaratibu uliokuwa na manufaaa kwa jamii yote?" alihoji Jonathan Humbe, mkazi wa Arusha.
Naye Sitta Tumma, anaripoti kutoka Mwanza kuwa tabibu mwingine ameibuka jijini Mwanza ambaye anadai anatibu magonjwa mbalimbali sugu ukiwemo ukimwi, ugonjwa wa akili (vichaa), kisukari na kupooza mwili.
Mganga huyo, Muhangwa Kapeji maarufu kwa jina la Babu wa ‘Glasi' anadai kutibu magonjwa mengine kadhaa na kwamba wagonjwa anaowatibu anawapatia glasi moja ya dawa iliyochemshwa, na baada ya siku 15 mgonjwa anatakiwa anywe tena dawa ya unga atakayopewa na kisha atakuwa amepona.
Akizungumza na waandishi wa habari jana nyumbani kwake katika Kijiji cha Mwamilolelwa, Kata ya Bugogwa, Kapeji alisema tiba anayoitoa ni sawa na ile ya Babu wa Loliondo, na tayari ameshawatibu maelfu ya wagonjwa wakiwemo wagonjwa watano waliokuwa na maambukizi ya virusi vya ukimwi.
Kapeji alisema anatumia miti miwili ambayo ni Ntundwa na Mpandayonzo au kwa jina jingine Mg'holu, ambapo amekuwa akichimba mizizi yake kisha kuichemsha na kuwapa wagonjwa kisha kupona maradhi yao ndani ya muda mfupi, na kati ya miti hiyo, mti wa Mg'holu haupatikani sehemu nyingine mkoani Mwanza, bali unapatikana katika Wilaya ya Sengerema pekee.
"Kazi hii ya kutibu na kuponya wagonjwa nina miaka 20 sasa...watu wengi wanakuja kupata glasi wakiwemo wagonjwa wa ukimwi na wanapona hadi leo wako salama! Wapo wagonjwa wameletwa hapa wamepooza miguu na mwili wote, vichaa, kisukari lakini wakipata glasi moja wanapona.
Awali, mwenyekiti wa taasisi ya utafiti wa dawa za asilia nchini Medicinac-Plant Foundation (TMF), Gonzaga Ndege, alisema utafiti walioufanya unaonyesha tiba inayotolewa na mganga Kapeji imekuwa ikiwaponya wagonjwa, hivyo wanatarajia kuchukua sampuli ya dawa na miti inayotumiwa kwa ajili ya kuipeleka hospitali ya Muhimbili kwa ajili ya uchunguzi zaidi.
na David Frank, Arusha
Habari zilizopatikana na kuthibitishwa na baadhi ya wadau wa habari zimeeleza kituo cha Bunda kiliwaachia watu na wagonjwa wengi kupita bila udhibiti wowote tangu Alhamisi iliyopita na kusababisha msongamano mkubwa katika kijiji cha Samunge huku msururu wa magari ukifikia kijiji cha Yandito.
Hazi hizo zimeeleza kutokana na msongamano uliyopo, ni wazi vifo vinaweza kutokea katika eneo hilo kwani hakuna uwezekano wa mgonjwa kupata tiba ndani ya siku mbili huku uhaba wa chakula na uchafuzi wa mazingira ukiendelea kuongezeka.
Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro, Elias Wawa Lali, alithibitisha kuwepo kwa hali hiyo huku akiwatahadharisha wagonjwa ambao hawajaanza safari kusitisha mara moja, kwani watakachokipata huko ni mateso ya siku zaidi ya mbili badala ya kusubiri wakiwa katika miji kunakopatikana huduma zote muhimu.
"Hali si shwari, Bunda wanadai wamelegeza masharti eti wamechoka kulaumiwa, sasa hali huku ni mbaya yawezekana kutokea tena kwa maafa na matatizo mengine makubwa …ni vizuri wale ambao hawajaanza safari wasitishe kwanza na sisi tumesimamisha safari kwa vituo vya Arusha na Babati kusubiri hali iwe nzuri," alisema Lali.
Aidha, baadhi ya watu waliozungumzia hali hiyo wameutoa shutuma zao kwa viongozi wanaosimamia kituo cha Bunda na kudai iwapo hali hiyo itaendelea basi vifo visivyotarajiwa vitatokea na tiba hiyo itakuwa katika mashaka.
"Naamini iwapo taratibu zitafuatwa hakuna tena wasiwasi wala mashaka juu ya tiba ya mchungaji huyo…vipi tena watu wa Kanda ya Ziwa wavunje utaratibu uliokuwa na manufaaa kwa jamii yote?" alihoji Jonathan Humbe, mkazi wa Arusha.
Naye Sitta Tumma, anaripoti kutoka Mwanza kuwa tabibu mwingine ameibuka jijini Mwanza ambaye anadai anatibu magonjwa mbalimbali sugu ukiwemo ukimwi, ugonjwa wa akili (vichaa), kisukari na kupooza mwili.
Mganga huyo, Muhangwa Kapeji maarufu kwa jina la Babu wa ‘Glasi' anadai kutibu magonjwa mengine kadhaa na kwamba wagonjwa anaowatibu anawapatia glasi moja ya dawa iliyochemshwa, na baada ya siku 15 mgonjwa anatakiwa anywe tena dawa ya unga atakayopewa na kisha atakuwa amepona.
Akizungumza na waandishi wa habari jana nyumbani kwake katika Kijiji cha Mwamilolelwa, Kata ya Bugogwa, Kapeji alisema tiba anayoitoa ni sawa na ile ya Babu wa Loliondo, na tayari ameshawatibu maelfu ya wagonjwa wakiwemo wagonjwa watano waliokuwa na maambukizi ya virusi vya ukimwi.
Kapeji alisema anatumia miti miwili ambayo ni Ntundwa na Mpandayonzo au kwa jina jingine Mg'holu, ambapo amekuwa akichimba mizizi yake kisha kuichemsha na kuwapa wagonjwa kisha kupona maradhi yao ndani ya muda mfupi, na kati ya miti hiyo, mti wa Mg'holu haupatikani sehemu nyingine mkoani Mwanza, bali unapatikana katika Wilaya ya Sengerema pekee.
"Kazi hii ya kutibu na kuponya wagonjwa nina miaka 20 sasa...watu wengi wanakuja kupata glasi wakiwemo wagonjwa wa ukimwi na wanapona hadi leo wako salama! Wapo wagonjwa wameletwa hapa wamepooza miguu na mwili wote, vichaa, kisukari lakini wakipata glasi moja wanapona.
Awali, mwenyekiti wa taasisi ya utafiti wa dawa za asilia nchini Medicinac-Plant Foundation (TMF), Gonzaga Ndege, alisema utafiti walioufanya unaonyesha tiba inayotolewa na mganga Kapeji imekuwa ikiwaponya wagonjwa, hivyo wanatarajia kuchukua sampuli ya dawa na miti inayotumiwa kwa ajili ya kuipeleka hospitali ya Muhimbili kwa ajili ya uchunguzi zaidi.