Baba yangu hataki nimsaidie pesa mke wake

Baba yangu hataki nimsaidie pesa mke wake

danhoport

JF-Expert Member
Joined
May 20, 2020
Posts
2,099
Reaction score
4,802
Habari jamaa zangu, ipo hivi baba angu mzazi ana watoto watano(5) kati ya hao watano mimi nipo peke yangu kwa mama(marehemu) na hao wengine wanne mama yao ni mmoja.

Huyo mama ameshatengana nae, hapo juzi alikuwa na shida akanitafuta kwenye simu nikamsaidia pesa kiasi, sasa sijajua baba kajuaje kama nimempa pesa nashangaa siku nampigia baba kumsalimia ndo anaanza kunisomea risala ananiambia hataki kusikia nimemtumia pesa tena na kama akiwa na shida awaambie watoto wake wa kuwazaa.
 

Attachments

  • Screenshot_20260119_174655_Messages.jpg
    Screenshot_20260119_174655_Messages.jpg
    19.5 KB · Views: 13
Huwei kujua baba yako kwa nini amekukataza, je ni kwa sababu tu ya ugomvi wao uliopelekea kuachana au kuna kitu amekiona, je hao ndugu zako wana uwezo wa kumsaidia Mama yao? kama hawako vzr kimaisha kiasi cha kushindwa kumsaidia Mama yao unaweza kumsaidia ila asitangaze....ila tafakari mara mbili kama kweli ni msaada anataka kwako au ana lengo baya na wewe huwezijua baba yako ameona/anajua nini mpk akukataze kumsaidia
 
1. Baba yako anamjua mkewe kuliko wewe, kwa hiyo lazma ujitahidi kujua dhumuni la kukukataza

2. Inategemea mliishije. Kama alikulea kama mwanae wa kumzaa. Hiyo inakuwa case tofauti kwa sababu kama yeye hakukufanyia ubaya, ukianza wewe, si tu utavunja mahusiano nae lakini pia kwa watoto wake.

Jaribu kuongea na mzee ujue sababu
 
Huyo mama mi scammer, stay away asaidiwe ma na watoto wa kuwazaaa la sivyo utamuuza mzee wako kuendelea kufanya hayo
Vipi Kama wanawe hawana uwezo au roho mbaya?
Vipi Kama huyo mama alimlea vizuri Sana huyu mdau mfano wa mwanawe wa kumzaa?
Mimi nililelewa vizuri sana na mama wa kambo. Sikuona tofauti yangu na waliolelewa na mama zao wa kuwazaa.
 
Kitendo tu cha dingi kujua umemsaidia mama ako mdogo inaonesha wazi huyo mama siyo mtu mzuri.

Naamini dingi ako hajashindwa kumsadia mzazi mwenzie kama kweli kulikuwa na changamoto serious.

Ila inavyoonekana alikuomba msaada makusudi ili dingi ako ajue, ili tu awafarakanishe.

Yani kuna li scenario hapo kati anataka kulitengeneza!
 
Huwei kujua baba yako kwa nini amekukataza, je ni kwa sababu tu ya ugomvi wao uliopelekea kuachana au kuna kitu amekiona, je hao ndugu zako wana uwezo wa kumsaidia Mama yao? kama hawako vzr kimaisha kiasi cha kushindwa kumsaidia Mama yao unaweza kumsaidia ila asitangaze....ila tafakari mara mbili kama kweli ni msaada anataka kwako au ana lengo baya na wewe huwezijua baba yako ameona/anajua nini mpk akukataze kumsaidia
Uwezo wanao ila hawampokelei simu
 
Vipi Kama wanawe hawana uwezo au roho mbaya?
Vipi Kama huyo mama alimlea vizuri Sana huyu mdau mfano wa mwanawe wa kumzaa?
Mimi nililelewa vizuri sana na mama wa kambo. Sikuona tofauti yangu na waliolelewa na mama zao wa kuwazaa.
Huyu mama nimekaa nae kwa mda mwezi mmoja tu kwenye maisha yangu mpaka sasa ila sasa nachojiuliza kwanini mzee anikataze kumsaidia
 
Vipi Kama wanawe hawana uwezo au roho mbaya?
Vipi Kama huyo mama alimlea vizuri Sana huyu mdau mfano wa mwanawe wa kumzaa?
Mimi nililelewa vizuri sana na mama wa kambo. Sikuona tofauti yangu na waliolelewa na mama zao wa kuwazaa.
Huyu mama nimekaa nae kwa mda mwezi mmoja tu kwenye maisha yangu mpaka sasa ila sasa nachojiuliza kwanini mzee anikataze
Kwa hekima uliyokuwanayo wewe maoni yako yapi katika hili
Nataka nimwambie bi mkubwa nilichoambiwa na mtalaka wake
 
1. Baba yako anamjua mkewe kuliko wewe, kwa hiyo lazma ujitahidi kujua dhumuni la kukukataza

2. Inategemea mliishije. Kama alikulea kama mwanae wa kumzaa. Hiyo inakuwa case tofauti kwa sababu kama yeye hakukufanyia ubaya, ukianza wewe, si tu utavunja mahusiano nae lakini pia kwa watoto wake.

Jaribu kuongea na mzee ujue sababu
Kuhusu kunilea ki ukweli sikuwahi kuishi nae kwa mda mrefu
 
Huyu mama nimekaa nae kwa mda mwezi mmoja tu kwenye maisha yangu mpaka sasa ila sasa nachojiuliza kwanini mzee anikataze

Nataka nimwambie bi mkubwa nilichoambiwa na mtalaka wake
Mbali na maneno ya baba yako bado unaona kuna uzuri aliyenao mama huyo. Endelea wewe kuona uzuri au upendo huo kwa mama huyo. Wengine tunaishi mbali na wazazi wetu na tunakutana na wamama wanaotuonyesha upendo kama walivyokuwa nao kwa watoto wao.
 
Back
Top Bottom