Sabahu zipo nyinhi sana.
Ya kwanza kabisa ni ile ya asili ambayo ni "psychologically and physiologically imbedded" ya kuwa mwanamke ni mlezi wa asili. Hii hujionyesha wazi pale watoto wa kike wangali wadogo wanapokuwa karibu sana na baba zao. Automatically mtoto wa kike huanza kuchukuwa role ya u mama toka angali mdogo.
Wazazi wasipokuwa makini na kuweka mipaka ya watoto wangali wadogo hupelekea ukaribu sana wa mtoto wa kike kumganda baba'ke wakati wote anapokuwepo nyumbani, tokea angali mdogo mpaka anapokuwa. Hali kadhalika kwa watoto wa kiume kwa mama zao.
Chemicals tunazotengeneza mwilini mwetu ambazo ni za asili ni aina nyingi, nyinginezo ni hususan za mwanamke kumtia ashki mwanamme na mwanamme kumtia ashki mwanamke. Hizo hazizuiliki na haziepukiki hususan mkiwa na ukaribu wa ki magharibi (westernized).
Chemicals hizo ukiongezea na u magharibi wa binti kufikia kumtokea baba'ke na jeans za KK, khanga moja, vi mini au viguo vinavyoonyeesha zaidi ya nusu ya maungo yake, ajibadilishe sauti. Labda huyo baba awe si rijali asishikwe na ashki anapoyaona hayo mfululizo.
Kuna mipaka inabidi iwepo katika malezi kuanzia udogoni kabisa ili kuepuka hayo
Watoto wengi wa kike na wa kiume huanza kuharibiwa majumbani mwao na watu wao wa karibu kabisa. Wengi zaidi huzowea na kuona hicho ni kitu cha kawaida kabisa ndani ya familia kiasi kuwa ni siri za ndani ya familia.
Solution ipo katika Uislam kwa wenye kufuata mafunzo ya Kiislam.
Duh
FaizaFoxy aisee mimi hata dada yangu tu niliyempita miaka minne tu akikaa uchi sina ashki naye. Huu umagharibi tunausingizia mengi kwa kweli.
Hapa ndipo ninaposhawishika kuungana na wale wanaouliza, sisi waafrika kabla ya hizo nguo za kujisitiri kuja, ina maana kubakana kulikuwa nje nje? Najua hatukuwa tukitembea uchi, lakini fikiria nyakati ambazo sehemu zilizozibwa ni hapo kwa bibi/babu na kifuani tu.
Hapana sidhani kama binti kuvaa 'kimagharibi' ni kisingizio cha kutosha kuhalalisha ubakaji.
Pili, dada yangu mimi nilikuwa polisi (na hili ni kweli wala siandiki ili kujustify point yangu) na kesi nilizopokea zilikuwa na mchanganyiko wa watu wote, wakristo kwa waislamu. Waliovaa kimagharibi na waliojifunika hadi nikab. Wa vijijini na wa mjini.
Ingawa ni kweli unachosema (pamoja na kwamba umekisema kwa upande mmoja, na una haki hiyo), watu wakiwa na hofu ya Mungu maishani mwao haya mambo hayatajitokeza. Mimi ninaamini vitabu vyote vya dini vina maelekezo mazuri ya jinsi ya kuvaa, na kuishi. Mambo yaliyokatazwa kufanywa na yaliyo chukizo mbele za Mungu. Hivyo basi kila mmoja kwa imani yake arudi kwenye misingi hiyo, haya mambo hayatajitokeza.
Na kama yatajitokeza (maana hata yule mtoto wa Mfalme Daudi, Amnon, alimbaka dada yake, Tamari, na walikuwa watoto wa mtu aliyeitwa na Mungu - 'a man after God's own heart') basi ndipo ninarejea kwenye NINI KIFANYIKE. Hapa ndipo mimi na wewe tunapoweza kutoa michango chanya ya nini serikali na jamii vifanye ili kuhakikisha hawa Tamari wetu hawaathiriki zaidi na matukio haya.
Shetani akimwingia mtu hachagui dini wala kabila dada yangu. Ni muhimu sana kusisitiza kuhusu kumcha Mungu, na hili ni la kwanza! Lakini la muhimu la pili, ni nini kifanyike baada ya hawa mafedhuli kufungwa maana mabinti wanabaki bila mtu wa kuwasomesha, wanabaki na misongo ya mawazo, wanabaki na mimba, wanakuwa watoto wenye watoto. Nini kifanyike. Ni nini tufanye mimi na wewe? Ni nini serikali na taasisi zake husika inaweza kukifanya kuwasaidia hawa?
Tukijibu hilo, hasa hapa kwa nini tunaweza kufanya kama jamii ya Watanzania basi naamini jibu la huyu binti mtoa mada litakuwa limepatikana.
MWISHO: Tumche Mungu jamani, tumuombe sana hizi tamaa zisitutafune. Shetani yupo kila mahali kila wakati akitafuta upenyo wa kutushawishi tuingie mtegoni mwake, tumshinde!!!