Baba yake Ben Saanane aiangukia serikali

Baba yake Ben Saanane aiangukia serikali

Daah nilikuwa sijui kumbe Ben nae ni mchaga?? Sasa pale Ufipa ni nani mwenye kabila tofauti?
Kwa hiyo kwa kuwa Ben ni mchagga ndio mmeamua kumshughulikia ... ?

Huko unakoabudu wewe hakuna wachagga ...?

Kwa hiyo, wewe na genge lenu ndio mpango wenu wa kuwaharibu, kuwapoteza wachagga wote kwa kuwa hawaungi mkono siasa za chama chenu ... ?!
 
Apeleke taarifa polisi na ITV wamuonyeshe kwenye kipindi cha jiji letu kuwa kapotea, vinginevyo aache porojo!!
 
unasali wapi?
Chumbani kwangu! Imeandikwa; "Tena msalipo msiwe kama wanafiki kwa maana wao hupenda kusali hali wamesimama katika masinagogi na katika pembe za njia ili waonekane na watu. Bali wewe usalipo ingia katika chumba chako cha ndani na ukiisha kufunga mlango wako, usali mbele za BABA yako aliye sirini, na BABA yako aonaye sirini atakujazi". Soma MATHAYO 6:5 - 6.
 
Mungu mpiganie Ben
[HASHTAG]#freemaxencemelo[/HASHTAG]
[HASHTAG]#TunamtakaBenAkiwaHai[/HASHTAG]
[HASHTAG]#JusticeForLema[/HASHTAG]
[HASHTAG]#usirudiekosa2020[/HASHTAG]
 
Chumbani kwangu! Imeandikwa; "Tena msalipo msiwe kama wanafiki kwa maana wao hupenda kusali hali wamesimama katika masinagogi na katika pembe za njia ili waonekane na watu. Bali wewe usalipo ingia katika chumba chako cha ndani na ukiisha kufunga mlango wako, usali mbele za BABA yako aliye sirini, na BABA yako aonaye sirini atakujazi". Soma MATHAYO 6:5 - 6.
hapo sawa maana nackia wengne wanasali palepale lumumba
 
Moshi. Focus Saanane, baba mzazi wa Ben Saanane ambaye ametoweka kwa mwezi mzima sasa, ameiangukia Serikali akiisihi imtafute na kumrejesha mwanae akiwa hai.

Ben ambaye ni msaidizi wa mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe inasadikiwa ametoweka tangu mwanzoni mwa Novemba.

Hiyo itakuwa mara ya pili kwa familia hiyo kuomba msaada huo. Wiki tatu baada ya Ben kutoonekana, mzazi huyo alitoa ombi hilo kwa niaba ya familia katika mitandao ya kijamii, akieleza kupotea kwa kijana wao na kuomba msaada kwa Mtanzania yeyote mwenye taarifa za mahali alipo.

Juzi, akizungumza na gazeti hili, mzazi huyo alisema familia haina chombo cha uchunguzi wala mamlaka ya kufanya uchunguzi, hivyo wajibu huo unapaswa kufanywa na Serikali kwa kutumia vyombo vyake kama Jeshi la Polisi.

“Hatuna la kufanya zaidi ya kumuomba Mungu,” alisema mzazi huyo.

Hii ni Tanzania tu! sijawahi ona sehemu, labda Rombo?
Badala ya kupeleka malalamiko yako vyombo husika (Polisi) wewe unalalamika kupitia mitandao ya kijamii na kwenye magazeti! hivi unategemea polisi wakufuate kuja kuandikisha maelezo yako huko?
Na ndio maana polisi wamepiga kimya hili swala, kwani hakuna kesi yoyote iliofunguliwa katika kituo chochote ya kupotea kwa Ben.!
hii inshu ipo kisiasa zaidi na chadema wanajua kinachoendelea.
 
Siasa hizi....!!!

Jamaa angekuwa anajihusisha na shughuli nyingine tofauti na siasa huenda haya yote yasingetokea.
Only cowards fears death, real men fears nothing.

Kama akina mtemi mkwawa, mirambo, isike, sina, Bwana heri, kimweri, makunganya, Songea wasingeazisha harakati za ukombozi na kufa wakitetea uhuru wa nchi hii, leo tungekuwa wapi?
 
Na bora wangekuwa wanafanya siasa za kutumia akili pia yasinge mkuta....mtu anashindwa anzisha mada juu ya kiongozi wake mbowe anataka kujua cv ya magufuri ili iwe nini,waende wamwulize Mbowe si ndo bosi wake.....watanzania wajinga sana sisi.
Cv ya mbowe anaifahamu na ndio maana alitaka kuijua ya magufuli.

Kujua cv ya kiongozi tuliye mchagua si kosa la kisheria.

Ukiwa mtu unayejiamini hutakasirika ukiulizwa yaliyomo kwenye Cv yako.
 
Back
Top Bottom