Umetoka shule kwa likizo. Umefika nyumbani unamkuta mama, unamuuliza mama, baba yuko wapi anakujibu yuko kazini.
Muda mwingi uko na mama ako tu. Ni siku ya Jumapili, baba anaingia chumbani kwako anakukuta ukipanga mabegi kwani kesho unarudi shuleni (likizo imeisha) anakupatia laki 8 za ada.
Ile anataka kuondoka, unamuomba laki moja ya matumizi. Anakwambia "hali ni ngumu mwanangu" ila anakupatia elfu 80, kisha anaondoka.
Unatoka chumbani kwako ukiwa umenuna, unaenda sitting room, unamkuta mama. Mama anakuuliza "mbona umenuna", unamjibu, "baba
amenipa elfu 80 badala laki kwa matumizi". Mama anafungua hand bag, anakupa elfu 30.
Wewe kwa akili yako mbovu, unakimbilia simu, unaingia FB unapost "HAKUNA KAMA MAMA". Umesahau kwamba baba yako leo ameenda kazini kwa mguu kwa sababu hana nauli? Umesahau kwamba jasho lake ndilo linalokuweka shule? Umesahau kwamba, hela aliyokupa mama kapewa na baba?
ACHA UBAGUZI WA WAZAZI!
Wazazi wote ni sawa ndugu. Kama umezoea kupost 'hakuna kama Mama", leo comment hapa chini "BABA NAKUPENDA SANA" Niwatakie siku njema ndugu zangu.
Mulanga
Michael mwakibete