Baba Nakupenda

Baba Nakupenda

Alinichukia kwa dhati kabisa tena bila hiyana, aliapa hatakaa apokee msaada wangu hata kama ndio tone la mwisho la misaada. Yaani aliapa kwa kila njia. LAKINI huwezi amini. Alinifia mikononi, alikaa kwangu 17 yrs. Tena nikampenda kupita.
Ndiyo kishatangulia mbele ya haki lakini nasema; BABA NAKUPENDA. Sioni cha kinitenga na mzazi wangu kwani, nadhani kuna siku aliwahigi kunipa zawadi yoyote hata kama ilikuwa haki yangu.
Ni chizi tu ambaye hampendi BABAKE.
Acha tu mi niwe chizi. MAANA SIMPENDI BABA YANGU
 
Na alishakuja kuniomba msamaha kwa kunikataa anadai alikua anaogopa kuchekwa na wenzie kwa kuzaa na mama kisa mama alikua fukara sana kwao

Sent using Jamii Forums mobile app
Nakuomba usilipize ubaya kwa ubaya,Hata kwenye vitabu vitakatifu maandiko yanasema tunatakiwa kusamehe kama unaamini ni baba yako hiyo kauli haina afya machoni pa Bwana,Katika zile amri kumi za Mungu mojawapo inasema Waheshim baba na mama ili upate kuishi milele.
 
Baba yangu alitangulia mbele za haki nikiwa Mdogo mama nae miaka kazaa ilopita kamfuata baba stowasahau wazazi wangu kamwe napenda kuwaambia yakua mwanenu siku hizi nimezoea kujitegemea japo nawa miss
 
Kwa
Ndio alichosema na alipata watoto wengine kwa mwanamke alieishi nae lakini wamekufa wote nimebaki mimi tu na ndio alipokuja kuniomba msamaha
Nikamuuliza kosa langu au alilokosa mama kwake akadai hajawahi kumkosea kwani alipompa mimba tu alikataa na kukimbia kijijini hapo hivyo hawezi ongopa na nakumbuka tumeishi kwa shida sana sana na nilikua natembea kwa miguu siku nzima kwenda mjini kuomba msaada kwake ila alinifukuza kama mara nne hivyo nikachoka
Baada ya kufiwa na watoto na mke wake akabaki mwenyewe na alipata matatizo ya kutokuona vizuri ndio akaanz kunitafuta na kuja kumuangukia mama na mm
Ila nikikumbuka naumia sana niishie hapo

Sent using Jamii Forums mobile app
Nadhani ulikuwa enzi za ujana wake kumbuka alikimbia kesi na alikuwa hajajiaandaa hakuna kitu kigumu kwa kijana girl friend wake kuambiwa ni mjamzito lazima utatikisika tu hata kama ulimpenda vipi
 
Duh, samahani kwa kuuliza, baba yako alisema hivyo kweli?
Yaani alikosa kabisa sababu nyingine ya kujitetea?
Jamaa hana baba hapo Malafyale,zee linashindwa hata kujitetea!zee limekosa hekima na busara! Mkazie mkuu aende akachukue msaada kwa rafiki zake.
 
Na ambao baba zetu walitukataa na hawakujali hata tulikua tukilala njaa na kuvaa chupi zenye matobo na wao wanakula bata mjini tunacoment neno gani
Sijawahi kumpenda na sitompenda japo simchukii ila sitaki ukaribu nae maana alinambia kwa kinywa chake nisitumie hata ubini wake ila leo ananitafuta eti nimpe matumizi
Nampa kama navoweza kuwapa ombaomba ila si kwa heahima ya ubaba
Nakupenda mama

Sent using Jamii Forums mobile app
Kinyume cha kutokupenda kitu ni kukichukia.
 
Watu wenye matatizo km yako hata kauli zenu huwa zinafanana utadhani huwa mnaambizana. Pole sana mkuu. Lkn me nataka nikuambie na kukupa ushauri ambao si lazima uuchukue. Pamoja na kwamba sijapata maelezo ya upande wa Baba yako lkn ukweli hicho unachosema kuhusu weakness za Baba yako ni 15%tu.

Hizo sababu zingine unazotoa unatuonyesha tu kwa hisia kuwa Baba yako alikuwa mbaya sana..na kwa bahati mbaya sana mpaka leo unaamini hivyo na unaposema jambo hilo kwa watu na wakakuonea huruma ww ndo unapata nafuu.

Hasira zako zote zinatokana na sumu aliyokulisha mama yako ambaye ndo alikulea na kwa sababu mlikuwa na shida sana wakati huo,ile sumu iliyokuwa inapandwa na mama yako ilikuwa rahisi tu kukuingia na kusema kweli imekuumiza mno!

Me nakuhakikishia mama yako pamoja na kukulea,lkn ndo alikuwa mbaya sana aliyesababisha hadi Baba yako awatelekeze. Me nakushauri ufanye jambo moja kubwa sana,msamehe Baba yako na muoneshe upendo utakuja kusikia vitu ambavyo hukutarajia kuhusu mama yako. Wanaume huwa ni wastaarabu sana huwa wanajizuia mambo mengi sana kuyasema kwa watoto wao.

Usiangalie sana mafanikio uliyoyapata,hayo mafanikio yamepatikana kutokana na hilo tukio. Pengine ungekuwa unapata kila kitu kwa Baba na mama ungebweteka na usingefika hapo ulipo leo. Hayo mapungufu ya wazazi wako ndo yaliyokujenga na kukupa hasira ya kupambana. Natamani kuandika sana,lkn Acha niishie hapa. Lkn unahitaji ushauri mkuu,hicho kitu kitakutesa maisha yako yote. Na kimsingi ww ndo unaumia kuliko hata Baba yako.

Sent using Jamii Forums mobile app

utakuwa umetelekeza watoto somewhere, unaongea unahisi ni kitu cha kawaida
 
Baba ata atembee kwa miguu kila cku, hafikii tabu aipatayo mama kubeba mtoto miez sita kuzaa na kumnyonyesha..
Ukija kwenye kulea hasa pale ambapo hujitambui, .
Mda wote mama upo attention kumuangalia mtoto asile uchafu, asishike vtu vya hatari kama moto.

Mababa huwa mnaongea tu but mkipata chance ya kulea mtoto kpnd anazaliwa hadi anakuja kujitambua hamtoweza.
Kwa mda wa zaid ya miaka mitatu unakuwa mda wote unamchunga mtoto ata hupat mda wa kpumzika .
Ata mfanyaje wababa..NANI KAMA MAMA ITABAKI PALEPALE..
ndo mana waislam wanaamin pepo ipo kwa mama

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watu wenye matatizo km yako hata kauli zenu huwa zinafanana utadhani huwa mnaambizana. Pole sana mkuu. Lkn me nataka nikuambie na kukupa ushauri ambao si lazima uuchukue. Pamoja na kwamba sijapata maelezo ya upande wa Baba yako lkn ukweli hicho unachosema kuhusu weakness za Baba yako ni 15%tu.

Hizo sababu zingine unazotoa unatuonyesha tu kwa hisia kuwa Baba yako alikuwa mbaya sana..na kwa bahati mbaya sana mpaka leo unaamini hivyo na unaposema jambo hilo kwa watu na wakakuonea huruma ww ndo unapata nafuu.

Hasira zako zote zinatokana na sumu aliyokulisha mama yako ambaye ndo alikulea na kwa sababu mlikuwa na shida sana wakati huo,ile sumu iliyokuwa inapandwa na mama yako ilikuwa rahisi tu kukuingia na kusema kweli imekuumiza mno!

Me nakuhakikishia mama yako pamoja na kukulea,lkn ndo alikuwa mbaya sana aliyesababisha hadi Baba yako awatelekeze. Me nakushauri ufanye jambo moja kubwa sana,msamehe Baba yako na muoneshe upendo utakuja kusikia vitu ambavyo hukutarajia kuhusu mama yako. Wanaume huwa ni wastaarabu sana huwa wanajizuia mambo mengi sana kuyasema kwa watoto wao.

Usiangalie sana mafanikio uliyoyapata,hayo mafanikio yamepatikana kutokana na hilo tukio. Pengine ungekuwa unapata kila kitu kwa Baba na mama ungebweteka na usingefika hapo ulipo leo. Hayo mapungufu ya wazazi wako ndo yaliyokujenga na kukupa hasira ya kupambana. Natamani kuandika sana,lkn Acha niishie hapa. Lkn unahitaji ushauri mkuu,hicho kitu kitakutesa maisha yako yote. Na kimsingi ww ndo unaumia kuliko hata Baba yako.

Sent using Jamii Forums mobile app

Huwa mnahisi tunalishwa sumu!???


Binafsi sijawahi kujadili chochote na mama kumuhusu baba
Ila mpaka kesho sina namna mtu anaweza kunishawishi kuhusu kumpenda baba.

Note: watoto huwa wanajifunza kupitia wanayoyaona kuliko wanayoyasikia.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huwa mnahisi tunalishwa sumu!???


Binafsi sijawahi kujadili chochote na mama kumuhusu baba
Ila mpaka kesho sina namna mtu anaweza kunishawishi kuhusu kumpenda baba.

Note: watoto huwa wanajifunza kupitia wanayoyaona kuliko wanayoyasikia.


Sent using Jamii Forums mobile app
Sasa km Baba yako amekutelekeza na hajakulea utajifunza vp kwa kumuona!?? Nnachokueleza mm,ndo ukweli wenyewe. Hasira zenu ni matokeo ya chuki iliyopandwa kwenu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sasa km Baba yako amekutelekeza na hajakulea utajifunza vp kwa kumuona!?? Nnachokueleza mm,ndo ukweli wenyewe. Hasira zenu ni matokeo ya chuki iliyopandwa kwenu.

Sent using Jamii Forums mobile app

Soma vizuri ukichoandika unaandika kwa hisia unashindwa kuhusianisha sentensi zako.
Sasa hizo chuki zinapandwa na nani?



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yes. ninasemaga hum mara kibao..majorty ya wanaume humu 80%hv wanakandiaga sana single moms..kumbe mmelelewq na mzaz m1..lakini kutwa kuwaponda wamama masingle parent hahhaa !
mie nashukuru sijawah mchukia baba wala nn...nampendq sana baba!waishi miaka mingi
 
Hii sasa kali
Na ambao baba zetu walitukataa na hawakujali hata tulikua tukilala njaa na kuvaa chupi zenye matobo na wao wanakula bata mjini tunacoment neno gani
Sijawahi kumpenda na sitompenda japo simchukii ila sitaki ukaribu nae maana alinambia kwa kinywa chake nisitumie hata ubini wake ila leo ananitafuta eti nimpe matumizi
Nampa kama navoweza kuwapa ombaomba ila si kwa heahima ya ubaba
Nakupenda mama

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Soma vizuri ukichoandika unaandika kwa hisia unashindwa kuhusianisha sentensi zako.
Sasa hizo chuki zinapandwa na nani?



Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu nilichoandika ndicho nilichokusudia hakuna nilipokosea. Hizo chuki unalishwa na walezi wako. Iwe mama,mjomba nk. Athari za wazazi kutengana watoto huwa wanabaki upande mmoja.

Bahati mbaya huwa wakibaki upande wa mama wengi ndo hupatwa na tatizo km hilo la kwako na wengine. Me ngoja nikuambie,me mwenyewe nimelelewa na mama.

Baba aliachana na mama me nikiwa na miaka 4 tu na mdogo wangu akiwa ananyonya. Baba alikuwa mkulima mzuri tu,na alikuwa anapata mazao ya kutosha kabisaa lkn alikuwa mlevi kupindukia. Na alikuwa anampiga mama hujawahi kuona duniani.

Kuna wakati alipigwa mpaka akavunjwa mkono,ndo hapo babu akasema inatosha akamchukua mwanaye ambaye ni mama yetu na sisi tukafuatana na mama. Tangu wakati huo,hatukuwahi kumuona Baba hata akija tu kutusalimia achilia mbali kutusaidia.

Lkn kwenye maisha yetu kwa wakati wote,hakuna siku hata moja tuliyowahi kuelezwa zuri hata moja la Baba. Mara zote tulikuwa tukielezwa ubaya na ukatili wa Baba. Hii kitu me ilikuwa inanishangaza sana,nikawa najiuliza huyu mzee alikuwa binadamu wa aina gani asiye na jema hata moja...!?? Mpaka nimemaliza primary bila kumuona baba. Baada ya kusoma o-level na kwa shida sana,sikupata matokeo mazuri nikaamua kuwa mjasiriamali.

Mwaka 1998.nikaamua kuoa,nikalazimika kumtafuta Baba. Nilimtafuta mpaka nikampata sehemu moja inaitwa bukoli wilaya ya geita akiwa nzwiii...yaani alikuwa amelewa chakariii. Nilibaki naye mpaka asbh pombe zilipoisha na tukaongea vizuri sana na nikasafiri naye kuja kwenye makazi yangu ya wakati huo.

Ni story ndefu lkn kwa kifupi pamoja na mapungufu ya Baba lkn mambo mengi alisingiziwa. Na kisa cha Baba kuwa mlevi lilikuwa ni tatizo la kisaikolojia baada ya kubomolewa nyumba yake nzuri sana wakati huo baada ya yeye kukataa kujenga kwa kutumia mkopo wa serikali.

Serikali ikaamua kumkomoa na kwa kuivunja nyumba yake. Baba alikuwa anahama na familia yake pamoja na duka lake kuja kuishi kwenye ile nyumba anafika nyumba yote imezolewa. Ndo maana nakuambia hizo huwa ni sumu tunazolishwa na bila kutafakari tunajenga chuki isiyofutika mioyoni mwetu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom