Baba Nakupenda

Baba Nakupenda

Wazazi wangu nawapenda sana. Sina mamlaka ya kulaani bali kusamehe. Babangu hakunilea ila alisababisha niwepo hivi leo.

Hukumu ya alichotenda kama alikusudia au mama alisababisha akimbie mimi sijui na huwa sipendi wala kufuatilia hilo maana najua mamangu japo nampenda kuliko mfano basi atamkandia kwa maneno ya kweli kidogo na uongo mwingi.

Hivyo huwa nasema siku zote asante wazazi wangu kwa kunileta duniani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Na ambao baba zetu walitukataa na hawakujali hata tulikua tukilala njaa na kuvaa chupi zenye matobo na wao wanakula bata mjini tunacoment neno gani
Sijawahi kumpenda na sitompenda japo simchukii ila sitaki ukaribu nae maana alinambia kwa kinywa chake nisitumie hata ubini wake ila leo ananitafuta eti nimpe matumizi
Nampa kama navoweza kuwapa ombaomba ila si kwa heahima ya ubaba
Nakupenda mama

Sent using Jamii Forums mobile app
Duuuh hii sasa Kali..

am better here
 
Waheshimu baba na mama upate miaka mingi na heri duniani................ingawaje nililelewa na mzazi mmoja..tena baba,alikua akinifanyia kila kitu,na hakuwahi kuniambia tatizo hata moja la ma a yangu.....Mama alinifia mikononi pale bugando baada ya kumuuguza kwa miezi minne.Nawapenda wazazi wangu wote.....
 
Yes. ninasemaga hum mara kibao..majorty ya wanaume humu 80%hv wanakandiaga sana single moms..kumbe mmelelewq na mzaz m1..lakini kutwa kuwaponda wamama masingle parent hahhaa !
mie nashukuru sijawah mchukia baba wala nn...nampendq sana baba!waishi miaka mingi
Asante. Nimelelewa na mamangu hadi namaliza masomo ya chuo kikuu ila sijawahi kumchukia babangu maana sijui nn kilimfanya akimbie na kwenda kufia mbali. Na mwaka huu naenda kujengea kaburi lake na huwa sipendi kumzungumzia sana maana mama anaujua ukweli na hawezi kuusema.

Nawapenda wazazi wangu maana bila wao wawili nisingekuwepo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Na ambao baba zetu walitukataa na hawakujali hata tulikua tukilala njaa na kuvaa chupi zenye matobo na wao wanakula bata mjini tunacoment neno gani
Sijawahi kumpenda na sitompenda japo simchukii ila sitaki ukaribu nae maana alinambia kwa kinywa chake nisitumie hata ubini wake ila leo ananitafuta eti nimpe matumizi
Nampa kama navoweza kuwapa ombaomba ila si kwa heahima ya ubaba
Nakupenda mama

Sent using Jamii Forums mobile app
Hizo ni exceptions zipo. Hata mama kuna waliowatupa watoto wao baada ya kuwazaa. Ila kwa wale ambao hawakutupwa hawawezi kuacha kumpenda mama eti kwa kiwa kuna mama mwingine alimtupa mtoto.

Sisi wenye baba zetu usitulazimishe tuwachukie kwa ajili yako wewe uliyepigwa chini na baba yako kwa ajili ya uzembe au matatizo ya mama yako.

NAKUPENDA BABA

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni kama msosi mezani tu, kinachokupa shibe ni ugali ila kinachodetermine kufurahia chakula ni mboga au viambata vingine vidogo vidogo.

Kwenye majukumu ya familia (zilizo nyingi) ni baba ndo awajibike, baba utalipa ADA za wanao kisha mama atawaita jikoni (mafichoni) na kuwashikisha kiasi kidogo cha ziada kwa siri (kwa sharti la kutomwambia mzee)..... hiki kiasi cha ziada ndo hubeba furaha ya mtoto kuliko ada ambayo ni JUKUMU lako.

Usile Mbegu.
Nafikiri ni sababu ya utoto tu....hicho anachokupa mama usikute kapewa na mzee...kwa akili za utu uzima unaona hamna maana....na pia kwa nini akupie jikoni, si atoe tu kwa uwazi hata mbele ya baba....Nafikiri wanawake huwa wana-brain wash watoto....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Asante. Nimelelewa na mamangu hadi namaliza masomo ya chuo kikuu ila sijawahi kumchukia babangu maana sijui nn kilimfanya akimbie na kwenda kufia mbali. Na mwaka huu naenda kujengea kaburi lake na huwa sipendi kumzungumzia sana maana mama anaujua ukweli na hawezi kuusema.

Nawapenda wazazi wangu maana bila wao wawili nisingekuwepo

Sent using Jamii Forums mobile app


Pole sana best..wala usitake kujua nn kiliwasibu..kamjengee baba
 
Pole sana best..wala usitake kujua nn kiliwasibu..kamjengee baba
Hakika bect huwa sipendi kabisa kuwatenga wazazi wangu najua kwenye ndoa kila mtu anamapungufu ila mama najua atajitetea kwa kumkandia baba hivyo huwa sitaki kabisa kumpa nafasi mama azungumzie nini kiliwatenganisha.

Ila yaani mamangu huwa napiga nae stori na mwisho huwa nasema asante wazazi kunileta duniani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hizo ni exceptions zipo. Hata mama kuna waliowatupa watoto wao baada ya kuwazaa. Ila kwa wale ambao hawakutupwa hawawezi kuacha kumpenda mama eti kwa kiwa kuna mama mwingine alimtupa mtoto.

Sisi wenye baba zetu usitulazimishe tuwachukie kwa ajili yako wewe uliyepigwa chini na baba yako kwa ajili ya uzembe au matatizo ya mama yako.

NAKUPENDA BABA

Sent using Jamii Forums mobile app
Akili zako ulisahau tumboni kwenye maelezo yangu wapi umesoma kwamba muwachukie baba zenu au wapi ninesema kwamba mababa wote ni wabaya
Acha utoto
Kumbuka kwa sasa mimi ni mama wa watoto watatu na ninaishi ndani ya ndoa safi wala sijasema hakuna baba wazuri

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Na ambao baba zetu walitukataa na hawakujali hata tulikua tukilala njaa na kuvaa chupi zenye matobo na wao wanakula bata mjini tunacoment neno gani
Sijawahi kumpenda na sitompenda japo simchukii ila sitaki ukaribu nae maana alinambia kwa kinywa chake nisitumie hata ubini wake ila leo ananitafuta eti nimpe matumizi
Nampa kama navoweza kuwapa ombaomba ila si kwa heahima ya ubaba
Nakupenda mama

Sent using Jamii Forums mobile app
Huyo sio baba yako. We mpende tu mama yako, lakini ujue mama yako si mwaminifu...

Mwambie akuambie baba yako halisi ni nani, usimlaumu mzee wa watu...

Afu mwambie mama ajutie dhambi yake ya uzinzi...

Nakupenda baba yangu, jembe hodari na pambanaji lililotukuka.
 
Kiukweli nakubaliana na mtu anayesema mama zetu wanapenda sana kuvutia kamba upande wao

Inreality hakuna mtu atakae farakana na mtu mwingine alafu aje akusimulie kwa namna ambayo itaonyesha yeye ana kosa...lazima aelezee kwa namna ambayo mwenzie ndio mwenye kosa

Kwa sasa nina wazazi wote ila kwa situation inayoendelea nazidi kumshkuru mungu sipo karibu nao maana kwa jinsi mother anavyonielezea anayoyafanya mzee nahisi ningeshaingilia kati kitu ambacho sio kizuri kuingilia ugomvi wa wazazi...

Kwa sasa bado nasoma ila kila nikipata likizo nikaenda home cha kwanza ninachokutana nacho kwa maza ni mabaya yote anayoyafanya mzee na anachotaka ni mimi nichukue hatua kumwambia mzee anachokifanya sio kizuri kitu ambacho ni kigumu mimi kukifanya kama mtoto kwa sababu pia sina uhakika na anayosema maza kama kweli ni ya kweli

Unakuta maza analalamika sana kuusu mzee kuwa amjali kwa kua anaumwa au atoi matumizi ...kwa swala la matumizi napingana na maza kwa kuwa mara nyingi mzee anakua hana ela ila yeye maza anashindwa kulitambua ilo....

Kwa hali ii nimejikuta nabaki dillema nifanye nini...mother anataka nimface mzee nimchane live anayoyafanya sio mazuri wakati mimi sijaprove kama kweli mzee anayafanya na ata kama kweli anayafanya siwezi kumface mimi kama maza anavyotaka maana ni kama nitakua nawaachanisha kabisa

Kwa ili limenifanya nisiwaamini sana mama zetu kwa kile wanachotwambia kuusu baba zetu

Kwa wanaowachukia baba zao nadhani ni swala la kutokuchambua yap ya kuchukua na yap ya kuyapotezea kutoka kwa mather

Kwa ufupi tu ninachotaka kushauri kabla ujamchukia mzazi mmoja jaribu kufatilua kwanza pande zote kama kweli yanayosemwa ni kweli

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Na ambao baba zetu walitukataa na hawakujali hata tulikua tukilala njaa na kuvaa chupi zenye matobo na wao wanakula bata mjini tunacoment neno gani
Sijawahi kumpenda na sitompenda japo simchukii ila sitaki ukaribu nae maana alinambia kwa kinywa chake nisitumie hata ubini wake ila leo ananitafuta eti nimpe matumizi
Nampa kama navoweza kuwapa ombaomba ila si kwa heahima ya ubaba
Nakupenda mama

Sent using Jamii Forums mobile app
Hutakiwi kumhukumu mzazi, mwenye kumhukumu ni Mungu peke yake, kumbuka kuwa mzazi ni Mungu wako wa pili, na vile vile unapokua unalalamikalalamika unakua unaupandiikiza huo ubaya aliokufanyia, kumbuka kua hivyo vitu hua vinatembea kizazi hadi kizazi, visipokukuta wewe ukawafanyia ubaya huo wanao basi wanao watawafanyia ubaya huo wajukuu zako, kwa hiyo sasa msamehe na usiendelee kuvikumbuka hivyo vitu.
 
Mimi kitendo tu cha mzee wangu kumpanda mother nikazaliwa kinatosha kumshukuru ayo mambo mengine ni matokeo tu.Inawezekana siku hiyo mzee anataka vyombo mother alikua anazingua au mother ndo alikua tayar mzee anazingua ila yote kwa yote niwashukuru tu kwakutimiza majukumu yao yakunifyatua,mambo ya malezi hapa kila mmoja ana historia yake kwasababu dunia ina mengi.
Mkuu umenena.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom