Baba Nakupenda

Baba Nakupenda

Tatizo la wamama hamuuhubiri upendo wa baba kwa mtoto.
Baba analipa ada, husemi mwanangu hii ada kalipa baba yako.
Baba anatoa poket mane, mama husemi, baba anatenda wema kwa watoto, mama husemi. Watoto wanabeba taswira kuwa ni wewe umetenda. Wanaanza kuwachukia wababa zao.
Na sisi kina baba tubadilike, kipaumbele chetu cha kwanza ziwe familia zetu.
Turudi nyumbani mapema, tuongee na watoto wetu, tushiriki kazi zao za masomo, tuwaambie NAKUPENDA, tucheze nao na tuwafanye watoto marafiki zetu.
Umemaliza!! bahati mbaya wengi wako hivyo. hata harusi nani anapewa zawadi ni mama!!
sana sana baba mtoto akikosa anaambniwa acha baba arudi. na ukirudi unaambiwa na mama mashtaka hhulizi unachukua bakora unachapa!! - sasa mbaya ni nani mama au baba? halafu mamaa anaanza kumbembeleza kukusema vibaya ulivyo mbaya huna huruma! visiting unatoa ada, pocket money , kila kitu na nauli ya mama!! na matumizi yake wewe huendi!! baba - kosa!! unajifanya uko busy!! halafu unataka upendwe!! - Imetosha!!!! akina baba mpo?
 
Pole sana mkuu.
Ndio alichosema na alipata watoto wengine kwa mwanamke alieishi nae lakini wamekufa wote nimebaki mimi tu na ndio alipokuja kuniomba msamaha
Nikamuuliza kosa langu au alilokosa mama kwake akadai hajawahi kumkosea kwani alipompa mimba tu alikataa na kukimbia kijijini hapo hivyo hawezi ongopa na nakumbuka tumeishi kwa shida sana sana na nilikua natembea kwa miguu siku nzima kwenda mjini kuomba msaada kwake ila alinifukuza kama mara nne hivyo nikachoka
Baada ya kufiwa na watoto na mke wake akabaki mwenyewe na alipata matatizo ya kutokuona vizuri ndio akaanz kunitafuta na kuja kumuangukia mama na mm
Ila nikikumbuka naumia sana niishie hapo

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndio alichosema na alipata watoto wengine kwa mwanamke alieishi nae lakini wamekufa wote nimebaki mimi tu na ndio alipokuja kuniomba msamaha
Nikamuuliza kosa langu au alilokosa mama kwake akadai hajawahi kumkosea kwani alipompa mimba tu alikataa na kukimbia kijijini hapo hivyo hawezi ongopa na nakumbuka tumeishi kwa shida sana sana na nilikua natembea kwa miguu siku nzima kwenda mjini kuomba msaada kwake ila alinifukuza kama mara nne hivyo nikachoka
Baada ya kufiwa na watoto na mke wake akabaki mwenyewe na alipata matatizo ya kutokuona vizuri ndio akaanz kunitafuta na kuja kumuangukia mama na mm
Ila nikikumbuka naumia sana niishie hapo

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu pole sana kwa maswahibu yaliyokukumba katika maisha yako hadi umefikia hapo ambapo una uwezo wa kumpa mtu msaada ni jambo la kumshukuru Mungu. Baada ya hayo machache ningependa nishee jambo na wewe ambalo kama utaona ni la busara utaweza kulifanyia kazi
Binafsi baba yangu alikua ameoa mke miaka hiyooooo, sasa kutokana na ubize wa kazi maana yeye na mke wake wote walikua waajiriwa wa serikalini tena mzee akiwa mtu wa masafari ya nje mara kwa mara hatulii home so mkewe akatafuta msaidizi wa kusaidia watoto wake kipindi hiko ana watoto wanne. Mama ndio alikua binti mdogo tu kijijini ameishia darasa la nne wazazi wake wakashindwa kumsomesha sababu walikua mafukara wa kutupwa na mama ndio mzao wa kwaza kwao so ikabidi apambane wadogo zake angalau wale. Maza ndio akachukuliwa kua beki tatu wa familia hiyo ya kishua sasa enzi hizo wanaishi Upanga, kutokana na uchakarikaji wa maza basi wakampenda sana na mzee alivyohamishiwa kikazi Italy zali likamwangukia wakaenda kuishi naye miaka tisa. Hapo ndio tatizo lilianza wakiwa kule mzee akaanza kumbungua beki tatu mara ujauzito, wapo nchi za watu ikabidi watu wawe wapole tu. Miaka tisa waliyoishi kule maza akatunukiwa watoto watanoooo imagine mbaba mmoja kazaa na beki tatu watoto watano huku mkewe wa ndoa anao watoto sita wakati huo.
Tatizo ni kwamba walivyorudi huku ukweli ukawekwa mezani mzee akakubali kishingo upande ila kwangu akagoma kata kata kua sio mwanae simply mtoto wa mwisho na inadaiwa mimba aliidaka kule kama siku kadhaa kabla ya kurudi huku so mzee kuunga unga tarehe akili ikamkatalia. Wale ndugu zangu wakubwa wakachukuliwa na mzee wakawa wanakula maisha hatari huku mimi na mama tumefukuzwa kwenda kijijini kwa babu, eeeeh bwana we tukaishi kwenye umasikini ambao sitaki kuukumbuka mapaka kesho. Yule mke wa mzee huruma ikamjia akaja kijijini kunichukua akasema atanilea kama baba na mama yangu na nimwite mama mkubwa na mzee nimuite baba mkubwa. Hela ya ada na ya matumizi mpaka namaliza la saba mama huyo mkubwa ndio alikua akitoa na mzee nilikua namsalimia baba mkubwa na hata jina situmii la ukoo wake. Ila kumaliza la saba miaka ile nikachaguliwa kuingia sekondari jumlisha na mabadiliko ya mwili nikaanza kufanana na watoto wa mke wake ndio hapo mashangazi wakaweka kikao tukapime DNA, majibu yanatoka 99.9 ni baba yangu, akainamisha kichwa chini kwa aibu na hapo ninajitambua fika tu maana nilichelewa kuanza shule hivyo nikiwa form one nilikua na miaka 18. Mzee akajaribu sana kuomba msamaha ila mazoea ya kumuita baba hayakuwepo kabisa mpaka hivi leo siwezi kumuita baba na wala sijawahi ingawa nilimsamehe kwa moyo wote na kuanzia hapo akawa anawaambia watu huyu kidume changu cha mwisho bwana
Nachotaka kushea na wewe ni kwamba despite majaribu gani umepitia iwapo ukiendelea kuhold a grudge moyoni mwako unajifunganisha na maroho ya kisasi na same thing itakuja kuhapen kama sio kwako kwa uzao wako, so jiachilie na msamehe kabisa na uvunje minyororo hiyo utajikuta umepata amani ambayo umeikosa miaka yote
Respect to all dads na mie leo naitwa baba so hakuna kitu kinauma kama kuendelea kumuona baba yako halafu una machungu naye HUFANIKIWI trust me
Ni hayo tu na mchana mwema
 
Kuna wale ambao baba zao baada tu ya kuwakojolea shahawa mama zao na kunasa ujauzito wakawatelekeza , sidhani kama watawapenda baba zao zaidi ya kuwachukia
 
ila watoto ukiwauliza wanawapenda sana akina mama japo sisi Wababas kutwa stress kutafuta ada zao za english medium
 
Ndio alichosema na alipata watoto wengine kwa mwanamke alieishi nae lakini wamekufa wote nimebaki mimi tu na ndio alipokuja kuniomba msamaha
Nikamuuliza kosa langu au alilokosa mama kwake akadai hajawahi kumkosea kwani alipompa mimba tu alikataa na kukimbia kijijini hapo hivyo hawezi ongopa na nakumbuka tumeishi kwa shida sana sana na nilikua natembea kwa miguu siku nzima kwenda mjini kuomba msaada kwake ila alinifukuza kama mara nne hivyo nikachoka
Baada ya kufiwa na watoto na mke wake akabaki mwenyewe na alipata matatizo ya kutokuona vizuri ndio akaanz kunitafuta na kuja kumuangukia mama na mm
Ila nikikumbuka naumia sana niishie hapo

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwa hili alilikoroga mwenyewe,
kwanza kakimbia sawa,
pili bila shaka ulienda kujipeleka kujitambulisha kuwa wewe ni mwanae ili akupe msaada maisha magumu lkn akakataa na kukutimua,

tatu, ulipozidi sana kumfuata akupe msaada maisha yako magumu akakutimua tena mara nne na kukutaka usitumie hata ubini wake.

Nne ulitaabika sana kumfuata umbali wa siku nzima kutembea na akakunyima msaada ambao anaweza kukupa. Bila kujali ulivyo mdogo na mhitaji. Ukachoka na ukaacha kumfuata

Tano. Umekua mkubwa amekufuata yeye akiomba msaada. Baada ya kupata shida yaani maisha magumu.

Ushauri Fuata maneno ya mama, MUOMBEE REHEMA KWANI HAKUNA BINADAMU ALIYEKAMILIKA. msaidie ukiweza ili Mungu akubariki kwa kutomtupa kabisa na kwakutolipiza kisasi, inauma sana.
 
Ndio alichosema na alipata watoto wengine kwa mwanamke alieishi nae lakini wamekufa wote nimebaki mimi tu na ndio alipokuja kuniomba msamaha
Nikamuuliza kosa langu au alilokosa mama kwake akadai hajawahi kumkosea kwani alipompa mimba tu alikataa na kukimbia kijijini hapo hivyo hawezi ongopa na nakumbuka tumeishi kwa shida sana sana na nilikua natembea kwa miguu siku nzima kwenda mjini kuomba msaada kwake ila alinifukuza kama mara nne hivyo nikachoka
Baada ya kufiwa na watoto na mke wake akabaki mwenyewe na alipata matatizo ya kutokuona vizuri ndio akaanz kunitafuta na kuja kumuangukia mama na mm
Ila nikikumbuka naumia sana niishie hapo

Sent using Jamii Forums mobile app
Pole sana......nakuelewa kabisa....pole kwa wote.
 
Baba ni Baba tu......Mama zaidi, sijawahi kutofautisha upendo wa Baba na Mama yangu daima.......wote nawapa 100%
 
Ndio alichosema na alipata watoto wengine kwa mwanamke alieishi nae lakini wamekufa wote nimebaki mimi tu na ndio alipokuja kuniomba msamaha
Nikamuuliza kosa langu au alilokosa mama kwake akadai hajawahi kumkosea kwani alipompa mimba tu alikataa na kukimbia kijijini hapo hivyo hawezi ongopa na nakumbuka tumeishi kwa shida sana sana na nilikua natembea kwa miguu siku nzima kwenda mjini kuomba msaada kwake ila alinifukuza kama mara nne hivyo nikachoka
Baada ya kufiwa na watoto na mke wake akabaki mwenyewe na alipata matatizo ya kutokuona vizuri ndio akaanz kunitafuta na kuja kumuangukia mama na mm
Ila nikikumbuka naumia sana niishie hapo

Sent using Jamii Forums mobile app
Pole sana ndg ila hunabudi kumsamehe 7×70 hayo mengine Mungu ataamua ila wewe hupaswi kuhujumu

$ There's clear light at the end of the Tannel $
 
Umemaliza!! bahati mbaya wengi wako hivyo. hata harusi nani anapewa zawadi ni mama!!
sana sana baba mtoto akikosa anaambniwa acha baba arudi. na ukirudi unaambiwa na mama mashtaka hhulizi unachukua bakora unachapa!! - sasa mbaya ni nani mama au baba? halafu mamaa anaanza kumbembeleza kukusema vibaya ulivyo mbaya huna huruma! visiting unatoa ada, pocket money , kila kitu na nauli ya mama!! na matumizi yake wewe huendi!! baba - kosa!! unajifanya uko busy!! halafu unataka upendwe!! - Imetosha!!!! akina baba mpo?
Wakija wote ada inatoka wapi

$ There's clear light at the end of the Tannel $
 
Mkuu pole sana kwa maswahibu yaliyokukumba katika maisha yako hadi umefikia hapo ambapo una uwezo wa kumpa mtu msaada ni jambo la kumshukuru Mungu. Baada ya hayo machache ningependa nishee jambo na wewe ambalo kama utaona ni la busara utaweza kulifanyia kazi
Binafsi baba yangu alikua ameoa mke miaka hiyooooo, sasa kutokana na ubize wa kazi maana yeye na mke wake wote walikua waajiriwa wa serikalini tena mzee akiwa mtu wa masafari ya nje mara kwa mara hatulii home so mkewe akatafuta msaidizi wa kusaidia watoto wake kipindi hiko ana watoto wanne. Mama ndio alikua binti mdogo tu kijijini ameishia darasa la nne wazazi wake wakashindwa kumsomesha sababu walikua mafukara wa kutupwa na mama ndio mzao wa kwaza kwao so ikabidi apambane wadogo zake angalau wale. Maza ndio akachukuliwa kua beki tatu wa familia hiyo ya kishua sasa enzi hizo wanaishi Upanga, kutokana na uchakarikaji wa maza basi wakampenda sana na mzee alivyohamishiwa kikazi Italy zali likamwangukia wakaenda kuishi naye miaka tisa. Hapo ndio tatizo lilianza wakiwa kule mzee akaanza kumbungua beki tatu mara ujauzito, wapo nchi za watu ikabidi watu wawe wapole tu. Miaka tisa waliyoishi kule maza akatunukiwa watoto watanoooo imagine mbaba mmoja kazaa na beki tatu watoto watano huku mkewe wa ndoa anao watoto sita wakati huo.
Tatizo ni kwamba walivyorudi huku ukweli ukawekwa mezani mzee akakubali kishingo upande ila kwangu akagoma kata kata kua sio mwanae simply mtoto wa mwisho na inadaiwa mimba aliidaka kule kama siku kadhaa kabla ya kurudi huku so mzee kuunga unga tarehe akili ikamkatalia. Wale ndugu zangu wakubwa wakachukuliwa na mzee wakawa wanakula maisha hatari huku mimi na mama tumefukuzwa kwenda kijijini kwa babu, eeeeh bwana we tukaishi kwenye umasikini ambao sitaki kuukumbuka mapaka kesho. Yule mke wa mzee huruma ikamjia akaja kijijini kunichukua akasema atanilea kama baba na mama yangu na nimwite mama mkubwa na mzee nimuite baba mkubwa. Hela ya ada na ya matumizi mpaka namaliza la saba mama huyo mkubwa ndio alikua akitoa na mzee nilikua namsalimia baba mkubwa na hata jina situmii la ukoo wake. Ila kumaliza la saba miaka ile nikachaguliwa kuingia sekondari jumlisha na mabadiliko ya mwili nikaanza kufanana na watoto wa mke wake ndio hapo mashangazi wakaweka kikao tukapime DNA, majibu yanatoka 99.9 ni baba yangu, akainamisha kichwa chini kwa aibu na hapo ninajitambua fika tu maana nilichelewa kuanza shule hivyo nikiwa form one nilikua na miaka 18. Mzee akajaribu sana kuomba msamaha ila mazoea ya kumuita baba hayakuwepo kabisa mpaka hivi leo siwezi kumuita baba na wala sijawahi ingawa nilimsamehe kwa moyo wote na kuanzia hapo akawa anawaambia watu huyu kidume changu cha mwisho bwana
Nachotaka kushea na wewe ni kwamba despite majaribu gani umepitia iwapo ukiendelea kuhold a grudge moyoni mwako unajifunganisha na maroho ya kisasi na same thing itakuja kuhapen kama sio kwako kwa uzao wako, so jiachilie na msamehe kabisa na uvunje minyororo hiyo utajikuta umepata amani ambayo umeikosa miaka yote
Respect to all dads na mie leo naitwa baba so hakuna kitu kinauma kama kuendelea kumuona baba yako halafu una machungu naye HUFANIKIWI trust me
Ni hayo tu na mchana mwema
nimependa story yako saaana!!
 
Wababa huwa tunajinyima sana kufanikisha malengo ya watoto wetu,pale inapotokea tu kutokuelewana na mke labda baadaye kutengena,mtoto anamezeshwa sumu(maneno ya chuki kuhusu baba yake)
 
Watu wenye matatizo km yako hata kauli zenu huwa zinafanana utadhani huwa mnaambizana. Pole sana mkuu. Lkn me nataka nikuambie na kukupa ushauri ambao si lazima uuchukue. Pamoja na kwamba sijapata maelezo ya upande wa Baba yako lkn ukweli hicho unachosema kuhusu weakness za Baba yako ni 15%tu.

Hizo sababu zingine unazotoa unatuonyesha tu kwa hisia kuwa Baba yako alikuwa mbaya sana..na kwa bahati mbaya sana mpaka leo unaamini hivyo na unaposema jambo hilo kwa watu na wakakuonea huruma ww ndo unapata nafuu.

Hasira zako zote zinatokana na sumu aliyokulisha mama yako ambaye ndo alikulea na kwa sababu mlikuwa na shida sana wakati huo,ile sumu iliyokuwa inapandwa na mama yako ilikuwa rahisi tu kukuingia na kusema kweli imekuumiza mno!

Me nakuhakikishia mama yako pamoja na kukulea,lkn ndo alikuwa mbaya sana aliyesababisha hadi Baba yako awatelekeze. Me nakushauri ufanye jambo moja kubwa sana,msamehe Baba yako na muoneshe upendo utakuja kusikia vitu ambavyo hukutarajia kuhusu mama yako. Wanaume huwa ni wastaarabu sana huwa wanajizuia mambo mengi sana kuyasema kwa watoto wao.

Usiangalie sana mafanikio uliyoyapata,hayo mafanikio yamepatikana kutokana na hilo tukio. Pengine ungekuwa unapata kila kitu kwa Baba na mama ungebweteka na usingefika hapo ulipo leo. Hayo mapungufu ya wazazi wako ndo yaliyokujenga na kukupa hasira ya kupambana. Natamani kuandika sana,lkn Acha niishie hapa. Lkn unahitaji ushauri mkuu,hicho kitu kitakutesa maisha yako yote. Na kimsingi ww ndo unaumia kuliko hata Baba yako.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu wewe ni genius,nikiri wazi toka nijiunge na jamii forum,nimekutana,nimejadiri na magreat thinker,lakini wewe kupitia uzi huu,kwa maneno yako haya,nakupa No yangu ya juu. BAHATI MBAYA SAAAANA HICHO ULICHOONGEA WENGI HAWAKIJUI. Wengi wanaishia kulalamika kama huyu,bila kujua,kufuatilia source ni nini?

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom