Baba mkwe Shahidi wa Yehova kakataa mahari ya pesa, anataka apelekewe magovi matano ya watu wazima

Bujibuji Simba Nyamaume

JF-Expert Member
Feb 4, 2009
74,991
156,280
Ukiusikia usemi wa watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa basi sasa ndio amini kuwa usemi huo upo na unafanya kazi.

Jumapili iliyopita nilimsindikiza mpwa wangu ( mtoto wa dada yangu yangu) kwenda kujitambulisha na kupangiwa mahari huko kijijini kwa binti (Bibi harusi mtarajiwa)

Kwa kweli mapokezi yalikuwa baridi sana, na tukadhania huenda tungeitiwa wezi. Binti alifichwa na hatukuwa na mwenyeji hata mmoja.

Wenyeji walitupokea, wakatukaribisha chini ya mti na kutuacha kwa zaidi ya masaa manner, huku wao wakiwa ndani wakiendelea na kikao chao.

Baada ya masaa manne kupita hatimaye wakaja tulipo na kuanza kutuuliza maswali ya kebehi sana kuhusu imani yetu.

Wakatuambia wao ni Mashahidi wa Yehova, kwanini tumeenda kumposa binti yao tusitafute binti wa dhehebu letu?

Tukajibu kuwa sisi wote ni Wakristo, lakini hawakuridhishwa na jibu hilo. Dhihaka na kebehi zikaendelea.

Hatukupewa chakula wala maji hadi tunaondoka, tulaambiwa majibu yetu yatafuata kwa barua.

Leo jioni mshenga katuletea barua yenye jibu la ombi letu. Tunatakiwa kupeleka magovi matano ya wanaume watu wazima.

Isome mwenyewe hiyo barua.

Wito wangu kwenu wazazi, kama hamtaki binti yenu aolewe na mtu msiye mtaka, muwe wawazi, sio mnaleta mambo ya ajabu ajabu.

20220908_204202.jpg
 
Hivi mpaka leo hii bado kuna vijana wanahangaishwa na mahari?

Hakuna sababu ya kulumbana na wazee wa binti, wewe jipangie mahari unayoona inakufaa, kisha mwambie binti akawaambie wazazi wake, wakikataa basi sepa zako, baada ya muda ninakuhakikishia binti mwenyewe (tena akisisitizwa na wazazi wake) atakusaka popote ulipo ili umuoe bila hata mahari.
 
Ukiusikia usemi wa watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa basi sasa ndio amini kuwa usemi huo upo na unafanya kazi.

Jumapili iliyopita nilimsindikiza mpwa wangu ( mtoto wa dada yangu yangu) kwenda kujitambulisha na kupangiwa mahari huko kijijini kwa binti (Bibi harusi mtarajiwa)
Buji nyanaume unaniangusha Kikolo mbona kuna kampeni za kudodosha mikono ya sweta kwa nini usiongee na Dr wakupatie mzigo wa kutosha!!!. Jiongeze Kikolooo
 
Ukiusikia usemi wa watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa basi sasa ndio amini kuwa usemi huo upo na unafanya kazi.

Jumapili iliyopita nilimsindikiza mpwa wangu ( mtoto wa dada yangu yangu) kwenda kujitambulisha na kupangiwa mahari huko kijijini kwa binti (Bibi harusi mtarajiwa)

Kwa kweli mapokezi yalikuwa baridi sana, na tukadhania huenda tungeitiwa wezi. Binti alifichwa na hatukuwa na mwenyeji hata mmoja.

Wenyeji walitupokea, wakatukaribisha chini ya mti na kutuacha kwa zaidi ya masaa manner, huku wao wakiwa ndani wakiendelea na kikao chao.

Baada ya masaa manne kupita hatimaye wakaja tulipo na kuanza kutuuliza maswali ya kebehi sana kuhusu imani yetu.

Wakatuambia wao ni Mashahidi wa Yehova, kwanini tumeenda kumposa binti yao tusitafute binti wa dhehebu letu?

Tukajibu kuwa sisi wote ni Wakristo, lakini hawakuridhishwa na jibu hilo. Dhihaka na kebehi zikaendelea.

Hatukupewa chakula wala maji hadi tunaondoka, tulaambiwa majibu yetu yatafuata kwa barua.

Leo jioni mshenga katuletea barua yenye jibu la ombi letu. Tunatakiwa kupeleka magovi matano ya wanaume watu wazima.

Isome mwenyewe hiyo barua.

Wito wangu kwenu wazazi, kama hamtaki binti yenu aolewe na mtu msiye mtaka, muwe wawazi, sio mnaleta mambo ya ajabu ajabu.

View attachment 2350522
Moja ya dhehebu gumu kabisa kuishi nao hata kwa ujirani tu ni hilo. Na kama wamekolea katika hiyo dini kuoa haiwezekani asilani. Hao hata kuimba mwimbo wa taifa kwao ni dhambi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom