Majigo
JF-Expert Member
- Feb 23, 2012
- 5,519
- 1,831
Kabla Sijadondokea Kiini cha tatizo, niwape mkasa mfupi Ili muweze kunielewa.Naimani ushauri wenu utaniongoza vyema.
Ni Binti ambaye sasa ni Mke Wangu.Nilisumbuka kidogo kumpata kwani nilipomuaproch alidai ana Mtu wake na anampenda sana hivyo niachane naye, kwakweli kwa mda wote sikuwahi kumuona huyo mtu wake hiyo ikazidi kunipa udadisi juu yake.''Kwa nini anikatae?''.Nikajipa kazi ya kiintelejensia, kumjua Mpinzani wangu.Nikagundua ni kweli ana Jamaa ila yuko Ughaibuni.
Angalau hii ikanipa matumaini na kurudisha kasi ya kuendeleza mashambulizi . Maneno Matamu hayakukauka Kichwani mwangu.Lengo ni kumshawishi Binti akubali ombi langu
Binti aliendelea na msimamo wake na safari hii alikuwa mkali kidogo,kuona hivyo nikaibuka na ombi la Urafiki wa kawaida. Alinielewa na nikafanya kila mbinu ili kumfanya ajisikie fahari kuwa nami.Ingawa sikuwa na Hela kivile,lakini ''izawadi ndogondogo''. Nilihakikisha havikomi kwake.
Maisha yakaendelea na tukawa tunaelewana sana.mida mingine anakuja gheto anapika na tunakula pamoja,kwa mtu wa nje angezani ni wapenzi kumbe lah!kwani mda mwingi tuliutumia tukiwa pamoja
Kuna siku mida ya jioni alikuja gheto akionekana kutokuwa sawa, nilijaribu kuuliza tatizo nini alidai yuko sawa nikajaribu kumdodosa akasisitiza nimuache na anaomba alale.
*******
Maisha yakasonga, Akili bado ilisumbuliwa na huyu binti, huku mara kwa mara nikiendelea kumkumbusha na kuonesha hisia za wazi kwake lakini sikufanikiwa
Nikaanza kuhisi tabia zake zikibadirika polepole mfano akaanza kuonesha kutofurahishwa, Anaponisaka Hewani usiku wa wanane na kukuta niko bize, basi atalalamika.
ooh! Majigo unajua siku hizi sikuelewi! unaongea na nani?
Hasa akiniona nimesimama na jinsia ya kike utamuona anavyokuwa mkali! hii kitu haikuwa kawaida yake. Kabla ilikuwa akiniuliza na kunitania kuwa tunapendezana na msichana huyo na angependa kupata wifi ka yule!! nilimjibu ''sina girl hivyo aache hayo maswali''
Kama Ilivyoada Siku nyingine tukiwa gheto, tunacheki Seres ya kifilipino huku tukitupia Popcon, Kuna kipengele katika ile seres kilihusu mapenzi tukajikuta tumeingia katika mjadala wa mahusiano.
Majigo unajua mpaka sasa sikuelewi, vipi umeshapata mwenzi?''aliuliza binti wakati huu kanigeukia na tunatazamana ana kwa ana''
''Hapana!''nilimjibu huku nami nikimtazama kwa jicho la nakutamani ujue''
''Unangoja nini?''aliendelea kuuliza binti wakati huo akiwa kaegemeza mikono yake mabegani mwangu
******
Siku hiyo tukajikuta tumefanya mchezo husiofaa kwa watoto wadogo basi ikawa zetu, tunajifungia Ndani na kumaliza yote humo
Maisha yalikuwa matamu sana hata kimasomo nilikuwa vizuri kwani hapo kabla ufaulu wangu haukuwa mzuri mi na mtoto mzuri kila kona ya mji, yeye mimi mimi yeye namna tulivyokuwa tunapeana mahaba, wakatupachika jina la ''njiwa'
Mambo yanabadirika baada ya jioni moja niko nae gheto huku tukiendelea kutomasana na kucheza michezo kama Wafanyavyo paka wadogo!...binti Akanipa taarifa iliyonistua sana alidai ana mimba yangu.
lilinipa wakati mgumu ukizingatia bado nlikuwa nasoma na mzazi wangu ni mtata sana endapo atasikia habari hizi itakuwaje.
Nililikabili Kiume kwani sikujutia kwa namna yoyote tena nikamwambia sitaki kusikia habari za kuitoa hiyo mimba nitafanya juhudi zote ili kusolv mambo.
******
sikumjulisha mtu.. Ila nilishangaa siku kuitwa na kuwekwa kikaangoni na mzee akintuhumu kumpachika mimba binti wa watu, na kusahau kilichonipeleka shule....akawa mbogo na kudai kuanzia siku hiyo hatotoa hela yake kwa masuala yangu ikiwamo ada!.
Sikuamini kama hii mzee angetoa maamuzi ya namna hiyo, ukizingatia tulikuwa karibu kufanya mitihani ya kuhitimu Chuo.. hivyo ningehitaji sana mchango wake kama mzazi
Nilijaribu kuwashirikisha watu mbalimbali ikiwamo mama ili kumshawishi mzee...lakini Haikusaidia
wakati huo tayari kitumbo cha binti kinaendelea kuchanua, kutokana na mgogoro na mzee, hata chuo nikasimama nikaanza kufanya vibarua ili kuweza kujijenga kimaisha kwani nilishajua naenda kuwa baba mda si mrefu
siku moja binti alikuja gheto akiwa analia ...Nilishajua kimenuka kwao kwani amekuwa akiniambia wazazi wake walianza kumuhisi tofauti Hivyo nikamuuliza nini kinaelendea...akaniambia ''wazazi wanataka kumjua muhusika wa ujauzito ule'' nikamwambia awape ukweli wala hasihofu kuhusu hilo
basi basi siku ya siku nikapata ugeni ,nilifaham kinachoendelea kwani wazazi waliongozana na bint...akili yangu ilishavurugika hivyo nikawa tayari kwa lolote.
Ni mkasa unaoniumiza sana hivyo naomba nitulize akili kwa mda itaendelea Wakuu.
Asanteni JIgo.
Ni Binti ambaye sasa ni Mke Wangu.Nilisumbuka kidogo kumpata kwani nilipomuaproch alidai ana Mtu wake na anampenda sana hivyo niachane naye, kwakweli kwa mda wote sikuwahi kumuona huyo mtu wake hiyo ikazidi kunipa udadisi juu yake.''Kwa nini anikatae?''.Nikajipa kazi ya kiintelejensia, kumjua Mpinzani wangu.Nikagundua ni kweli ana Jamaa ila yuko Ughaibuni.
Angalau hii ikanipa matumaini na kurudisha kasi ya kuendeleza mashambulizi . Maneno Matamu hayakukauka Kichwani mwangu.Lengo ni kumshawishi Binti akubali ombi langu
Binti aliendelea na msimamo wake na safari hii alikuwa mkali kidogo,kuona hivyo nikaibuka na ombi la Urafiki wa kawaida. Alinielewa na nikafanya kila mbinu ili kumfanya ajisikie fahari kuwa nami.Ingawa sikuwa na Hela kivile,lakini ''izawadi ndogondogo''. Nilihakikisha havikomi kwake.
Maisha yakaendelea na tukawa tunaelewana sana.mida mingine anakuja gheto anapika na tunakula pamoja,kwa mtu wa nje angezani ni wapenzi kumbe lah!kwani mda mwingi tuliutumia tukiwa pamoja
Kuna siku mida ya jioni alikuja gheto akionekana kutokuwa sawa, nilijaribu kuuliza tatizo nini alidai yuko sawa nikajaribu kumdodosa akasisitiza nimuache na anaomba alale.
*******
Maisha yakasonga, Akili bado ilisumbuliwa na huyu binti, huku mara kwa mara nikiendelea kumkumbusha na kuonesha hisia za wazi kwake lakini sikufanikiwa
Nikaanza kuhisi tabia zake zikibadirika polepole mfano akaanza kuonesha kutofurahishwa, Anaponisaka Hewani usiku wa wanane na kukuta niko bize, basi atalalamika.
ooh! Majigo unajua siku hizi sikuelewi! unaongea na nani?
Hasa akiniona nimesimama na jinsia ya kike utamuona anavyokuwa mkali! hii kitu haikuwa kawaida yake. Kabla ilikuwa akiniuliza na kunitania kuwa tunapendezana na msichana huyo na angependa kupata wifi ka yule!! nilimjibu ''sina girl hivyo aache hayo maswali''
Kama Ilivyoada Siku nyingine tukiwa gheto, tunacheki Seres ya kifilipino huku tukitupia Popcon, Kuna kipengele katika ile seres kilihusu mapenzi tukajikuta tumeingia katika mjadala wa mahusiano.
Majigo unajua mpaka sasa sikuelewi, vipi umeshapata mwenzi?''aliuliza binti wakati huu kanigeukia na tunatazamana ana kwa ana''
''Hapana!''nilimjibu huku nami nikimtazama kwa jicho la nakutamani ujue''
''Unangoja nini?''aliendelea kuuliza binti wakati huo akiwa kaegemeza mikono yake mabegani mwangu
******
Siku hiyo tukajikuta tumefanya mchezo husiofaa kwa watoto wadogo basi ikawa zetu, tunajifungia Ndani na kumaliza yote humo
Maisha yalikuwa matamu sana hata kimasomo nilikuwa vizuri kwani hapo kabla ufaulu wangu haukuwa mzuri mi na mtoto mzuri kila kona ya mji, yeye mimi mimi yeye namna tulivyokuwa tunapeana mahaba, wakatupachika jina la ''njiwa'
Mambo yanabadirika baada ya jioni moja niko nae gheto huku tukiendelea kutomasana na kucheza michezo kama Wafanyavyo paka wadogo!...binti Akanipa taarifa iliyonistua sana alidai ana mimba yangu.
lilinipa wakati mgumu ukizingatia bado nlikuwa nasoma na mzazi wangu ni mtata sana endapo atasikia habari hizi itakuwaje.
Nililikabili Kiume kwani sikujutia kwa namna yoyote tena nikamwambia sitaki kusikia habari za kuitoa hiyo mimba nitafanya juhudi zote ili kusolv mambo.
******
sikumjulisha mtu.. Ila nilishangaa siku kuitwa na kuwekwa kikaangoni na mzee akintuhumu kumpachika mimba binti wa watu, na kusahau kilichonipeleka shule....akawa mbogo na kudai kuanzia siku hiyo hatotoa hela yake kwa masuala yangu ikiwamo ada!.
Sikuamini kama hii mzee angetoa maamuzi ya namna hiyo, ukizingatia tulikuwa karibu kufanya mitihani ya kuhitimu Chuo.. hivyo ningehitaji sana mchango wake kama mzazi
Nilijaribu kuwashirikisha watu mbalimbali ikiwamo mama ili kumshawishi mzee...lakini Haikusaidia
wakati huo tayari kitumbo cha binti kinaendelea kuchanua, kutokana na mgogoro na mzee, hata chuo nikasimama nikaanza kufanya vibarua ili kuweza kujijenga kimaisha kwani nilishajua naenda kuwa baba mda si mrefu
siku moja binti alikuja gheto akiwa analia ...Nilishajua kimenuka kwao kwani amekuwa akiniambia wazazi wake walianza kumuhisi tofauti Hivyo nikamuuliza nini kinaelendea...akaniambia ''wazazi wanataka kumjua muhusika wa ujauzito ule'' nikamwambia awape ukweli wala hasihofu kuhusu hilo
basi basi siku ya siku nikapata ugeni ,nilifaham kinachoendelea kwani wazazi waliongozana na bint...akili yangu ilishavurugika hivyo nikawa tayari kwa lolote.
Ni mkasa unaoniumiza sana hivyo naomba nitulize akili kwa mda itaendelea Wakuu.
Asanteni JIgo.