Wandugu nimekuja. Humu kuomba ushauri kwa hili swala linalonisumbua.
Ni mida sasa umepita tangu kuachana na dume langu nililokuwa naishi nalo baada ya mzozo wa hapa Na pale.
Wazazi wakatuita kusuluisha lakini Baba mkwe akakomalia hataki kuona tukirudiana huku akitoa sababu ambazo hazina msingi wa maana, wazazi wangu kuona vile wakaamsha popo tukaondoka namimi nikaelekea kwangu.
Sasa Ni muda Baba mkwe amekuwa akinilaghai anataka tuanzishe Uhusiano Na badae ikiwezekana tuanze kuishi pamoja, mkewe alifariki katika ajali ya gari miaka 7 iliyopita.
Wanajamii hii kitu ndo kwanza naisikia kutoka kwa huyu Baba naona sio kawaida,.
Nikamshtaki kwenye ukoo au?