Baba Mbasha: Flora alichoka kuishi na mwanangu

Baba Mbasha: Flora alichoka kuishi na mwanangu

Hiyo hakika mimi sijaiona, nilichoona hapo ni maneno ya wazazi yasiyo na chembe ya hekma! Inatia aibu na ni aibu kwa Mbasha kuwa na wazee kama hawa!

Hivi kesho ikatokea Mbasha na Frola wakarudiana, hawa wazazi watajificha wapi??

Afadhari umejinasua kwenye hilo tego dada Frola, maana kama ushauri ndio mlikuwa mnaupata kwa huyu mzee ndio sishangai kwahaya yaliyotokea, huenda BRO Maneno ndio aliemshauri BRO Emma apige tu shem.


Usikie hivyo hivyo yasikupate ......
 
Mzee anasema mwanae alikuwa mkoani kumsalimia ndugu ambae ni mgonjwa..hapa flora ana kosa maana alivopigiwa simu na baba mkwe wake akampokee alikua na uwezo wa kusema kuwa hawezi kuja kumpokea na mzee wa watu akatafuta njia nyingine..sasa Flora yeye akamjibu nakuja baba wa watu akakaa stand masaa matano anasubiri...alivoona kimya akajua Flora kaingia mitini which is not good.
Huyu ana mambo mengi yaliojificha tusioyajua...

Kama alijua mwanae alikuwa mkoani, alikuja kumpatanisha Frola na nani sasa? Kama sio unafiki ni nini, yeye alijua kuna ugomvi kwa wawili hao alafu anakuja kupatanisha ilhali akijua mwanae yupo mkoani! Hayupo sawa huyu mzee
 
Kabisa kabisa...iz ndizo nyakat za mwisho yaliyoandikwa kwenye biblia hatimae yanatimia..mungu si kanisa bal mung ni iman yako rohon kwako..kutanga tanga na makanisa akufai
 
Sina shaka hapa ile laana ya Moses Kulola inawatafuna.:embarrassed:
Hapo mzee umesema ukweli tupu, kwani aliwaaambia kuwa yeyote atakaye kimbilia makanisa haya mapya ndio mwisho wake utakuwa umefika, na Flora alihamia kwenye kanisa alilopo baada ya babu yake kufa, hivyo laana inamaliza.
 
Hiyo hakika mimi sijaiona, nilichoona hapo ni maneno ya wazazi yasiyo na chembe ya hekma! Inatia aibu na ni aibu kwa Mbasha kuwa na wazee kama hawa!

Hivi kesho ikatokea Mbasha na Frola wakarudiana, hawa wazazi watajificha wapi??

Afadhari umejinasua kwenye hilo tego dada Frola, maana kama ushauri ndio mlikuwa mnaupata kwa huyu mzee ndio sishangai kwahaya yaliyotokea, huenda BRO Maneno ndio aliemshauri BRO Emma apige tu shem.
Kumbe Joyce kiria mko wengi!!!
 
Hawa wazazi naona kama ndio wanaharibu kabisa!

Inawezekana concern za mzee zina ukweli ila kuingilia ndoa ya mtu ni tatizo kubwa...litamgharimu sana mzee. Bora angesema nyuma ya pazia
 
  • Thanks
Reactions: SMU
Kuna pepo linaiandama hii ndoa ya hawa jamaa, hivi sasa huwezi kumtofautisha kati ya Frola na Wema sepetu tena hadi wema ana afadhali kabisa.
 
Kuna pepo linaiandama hii ndoa ya hawa jamaa, hivi sasa huwezi kumtofautisha kati ya Frola na Wema sepetu tena hadi wema ana afadhali kabisa.
Duuh mkuu umeenda mbali, Ahahaaa.
 
Kumbe Mbasha dini sio ya kurithi naona wazazi sio wakristo safi sana ukiwa upo kwenye dini kwa utashi wako na sio mapokeo
 
Umemsikia brother Francis anachokifanya Rome lkn! Je yule Padri aliemuingilia kijana wa watu kinyume na maumbile, au umesahau yule askofu wa katoriki aliekamatwa akiwanga kusini! Ukristo ni mtu na moyo wake, changamoto zipo kila mahali! Au utajietea kwamba katoliki ni kawaida...

No argument with you brother!
 
Huyu baba ana wake wangapi?Uaminifu wake una mashaka sana.Mwanae hakuwepo.tena anajua ameenda kutizama bibi yake aliyevunjika mguu.sasa alienda kwa Mbasha kuwapatanisha nani?Kwa nini yeye hakwenda kumuona mgonjwa?

Aisee mzee naye ni polygamist lol! Like father like son!
 
Mlango wa sita ni jicho la kati hapa kwenye paji la uso ambalo kimsingi ndie yule mpinga kristo alieandikwa sana kwenye kitabu cha ufunuo katika biblia takatifu! No wonder unamsema hivyo huyo dada!
Hiyo ni tafsiri yako kulingana na mitazamo yenu mnayofundishwa na manabii wenu wa leo....
 
Hiki ni kipindi cha mzazi kuonyesha hekima yake kwa kuchagua nini cha kuongea, ukiwa mpayukaji unaharibu zaidi badala ya kutengeneza

Familia ya wapayukaji/waropokaji! Baba mpayukaji mtoto mropokaji
 
Frola hakuwahi kuwa mlokole ila alitumia kivuli cha ulokole na nyimbo za 'dini' kama njia ya kupata umaarufu na mafanikio... uvaaji wake na kujipodoa kwake hasa ile style ya kutinda nyusi na kuweka wanja mreefu juu kabisa ya macho viliwakilisha uchangu zaidi kuliko uchaji kwa Mungu. Kwangu mimi uso wa Flora ulikuwa uso wa ibilisi
100% sahihi mkuu....
 
Mhhh kweli uchungu wa mwana aujua mzazi..

Inauma sana.
Inaonesha Flora kaota mapembe. Nilitarajia kwamba, kwa kuwa wazazi wamesafiri kutoka Mwanza kuja Dar kwa ajili ya suala la usuluhishi, ilitakiwa Flora afunguke na kusema kila kitu, iwapo mumewe ndio mkosaji. Lakini ukisikiliza maelezo ya wazazi, inaonesha binti hakutaka suluhu yoyote wala kusema kwa undani yanayomsibu.
 
Kama alijua mwanae alikuwa mkoani, alikuja kumpatanisha Frola na nani sasa? Kama sio unafiki ni nini, yeye alijua kuna ugomvi kwa wawili hao alafu anakuja kupatanisha ilhali akijua mwanae yupo mkoani! Hayupo sawa huyu mzee

Pengine alikuwa anawahi Dar kumsihi Flora arudi nyumbani kuliko kukaa kwa watu au hotelini na kama Flora nagekubali basi mumewe Mbasha ambae alikuja baadae ingekua rahisi kukaa chini kama familia na kusuhulisha..sasa Flora yeye kila kitu anakataa...kalaaniwa huyu dada si bure
 
Inauma sana.
Inaonesha Flora kaota mapembe. Nilitarajia kwamba, kwa kuwa wazazi wamesafiri kutoka Mwanza kuja Dar kwa ajili ya suala la usuluhishi, ilitakiwa Flora afunguke na kusema kila kitu, iwapo mumewe ndio mkosaji. Lakini ukisikiliza maelezo ya wazazi, inaonesha binti hakutaka suluhu yoyote wala kusema kwa undani yanayomsibu.

Labda mzazi mwinngine na sio huyu Maneno na mamsapu.hakuna kitu kwa hawa.hawana sifa na tusiwasikie na vioja vyao tena.Warudi Mwanza wakafundwe
 
Back
Top Bottom