Dar es Salaam. Kuna kila dalili kwamba
mwimbaji maarufu wa muziki wa Injili nchini,
Flora Mbasha na mumewe Emmanuel Mbasha
wanatamani kurudiana, baada ya kuwapo
mgogoro katika uhusiano wao wa ndoa,
ulioingia katika vyombo vya habari yapata
mwezi mmoja sasa.
Kwa nyakati tofauti jana, kila mmoja wao
alimwambia mwandishi wetu kwamba yupo
tayari kurudiana na mwenzake, hatua ambayo
inaweza kuondoa mgogoro huo ambao
umefifisha taswira yao ya kiutumishi.
Akizungumza nyumbani kwake Tabata
Kimanga, Dar es Salaam, Mbasha alisema
ameshamsamehe mkewe na kwamba
anamsubiri muda wowote arudi nyumbani
kusuluhisha mgogoro wao.
Nawapenda Watanzania wote wazidi
kutuombea ili mimi na mke wangu turudiane.
Kauli hiyo ni sawa na ile aliyoitoa Flora wiki
iliyopita pale aliposema: Ninawaomba
Watanzania waendelee kuniombea ili niweze
kushinda majaribu haya, kilichotokea ni
sehemu tu ya kupimwa imani yangu.
Jana, Flora alirudia kauli hiyo kupitia kwa
wakili wake, Addo Mwasongwe ambaye
alisema mwimbaji huyo yupo tayari kukutana
na mumewe na ndugu ili waondoe tofauti zao.
Maelezo ya Mbasha
Kwa upande wake Mbasha alisema: Mi
namwomba Flora ajishushe akubali, aje home
(nyumbani) tuyamalize na maisha yaendelee.
Yeye ni mke wangu namtaka. Kama
ananipenda arudi, tuite wazazi tutatue
mgogoro huu.
Aliongeza kuwa hakuna binadamu yeyote
asiyesamehewa na kwamba kilichotokea
katika ndoa yao ni sehemu ya maisha ambayo
wengi hupitia.
Siku zote naamini tunachotakiwa ni kujenga
na siyo kubomoa
Flora asinganganie kwa
watu arudi hapa
apige hodi
mume wangu
nimerudi
na mimi nitampokea tuendelee
kulea watoto.
Mbasha anakabiliwa na tuhuma za kumbaka
shemejiye wa miaka 17 na kesi yake
inaendelea katika Mahakama ya Wilaya ya
Ilala na sasa yupo nje kwa dhamana.
Kauli ya Flora
Wakili Mwasongwe alisema: Flora amesema
ameshayatoa rohoni masuala yote ya
mgogoro na mumewe na leo (jana) aliniambia
anataka kusuluhishwa hata kesho (leo) lakini
nimeshindwa kuwakutanisha kwa sababu nipo
busy.
Ila nilimwambia Ijumaa hii nitafanya hivyo
kwa kuwakutanisha yeye (Flora), Mbasha na
wazazi wake ili kumaliza tofauti hizo.
Wakili huyo alisema awali alikutana na wazazi
wa Mbasha lakini hawakufikia mwafaka, lakini
kwa sasa anaamini mambo yatakwenda vizuri.
by: MCL