passion_amo1
JF-Expert Member
- Dec 3, 2023
- 1,578
- 3,148
Wakuu habari za uzima?
Unajua Jamii forums ni ni sehemu ya kuvuna maarifa, kuburudika, na hata kutengeneza marafiki na uhusiano miongoni mwetu.
Ndugu zangu na wapendwa wote jamii forum, kuna baadhi ya mambo huenda yakawa yanachukuliwa katika hali ya utani lakini yakawa na madhara hasi pasi na mtu kulitambua hilo.
Embu Tazama mfano;
Kijana mmoja anasema, singo maza ndio wanaongoza kutoa mbususu hovyo, na pia singo maza ndio wanaongoza kujiuza kwenye madanguro?
Fikiria hii sentensi ameandika akitaka kuonyesha kwamba yupo sahihi lakini kinyume chake ni kuendelea kuvua wanaume nguo.
Kama singo maza chanzo chake kikubwa ni sisi WANAUME, mwanamke mtu kamzalisha wameshindwana labda kwa sababu mwanamke ajatulia sawa, je hayo majukumu ya mtoto wako unamuachia nani?
Huyu singo maza kila atakapoenda kutafuta kazi ataombwa rushwa ya ngono, mwanaume tayari kashakimbia na hakuna huduma yoyote anayoitoa kwa mtoto wake.
Unafikiri huyu mwanamke atafanya nini kuendelea kumpa huduma muhimu mtoto wake? Mwisho wa siku ataishia kutafuta njia za kujirahisisha ili tu aendelee kumtunza mtoto wake kwasababu tu ya mwanaume mpumbavu asiyejua kwamba kuwa mwanaume kuna ambatana na majukumu mazito.
Wanasema chizi hufurahisha anapokuwa si nduguyo, ila kama ni nduguyo hicho ni kilio. Tumuulize tu kama dada yake akamkuta katika madanguro sababu ya mwanaume ambaye alimtelekeza yeye atajisikiaje?
Kama kijana huyu sasahiv ngozi bado imenyooka, damu bado ya moto, ananyoa anapendeza akifikiri kwamba ujana utakuwepo tu basi ni kujidanganya.
Ipo siku mtoto wako wakike na yeye atakuwapo katika madanguro kwa sababu ya mwanaume mpumbavu kama wewe ambaye ulishindwa kutimiza majukumu yakiume.
Embu fikiria huu mfano;
KATAA NDOA, UMIZA MWANAMKE.
Huyu ni mtu ambaye anasema umiza mwanamke, ambaye kaja kwa kupitia kati kati ya mapaja ya mwanamke huyo!
sasa tumuulize kama amesema umiza mwanamke je mama yake aliyemzaa alishamuumiza? Hivi wanaume huwa mnajaribu kufikiri mnachoandika hapa?
Je huyu aliyesema umiza mwanamke yupo tayari kumuona mama yake akinyanyasika mbele yake na akampongeza huyo anayemnyanyasa?
Jamani ndugu zangu embu tujaribu kufikiri japo kwa uchache mambo tunayoongea, hii sehemu inafika watu wengi sana.
Tunaweza kuonekana wengi ni wapumbavu wasio na maana sababu tu ya wachache ambao wanahitaji watu wakuwaweka busy kwa kusoma maoni yao.
Kama unahitaji kuumiza mwanamke aidha kwa kihisia, hawa wanawake wasipokuwapo unafikiri tutaendelea vipi kuongezeka?
Hao watu wakufanya kazi ya kuliendeleza taifa watatoka wapi na tayari mtu anasema umiza mwanamke?
Naomba tu ndugu zangu tujaribu kufikiri tunachokiandika hata kama ID tunazotumia ni feki, embu tujitahidi tu.
Yaani kila siku wanaume tunaendelea kuvuliwa nguo sababu ya watu wachache , tunaendelea kuonekana si lolote sababu ya mambo haya!
Unajua Jamii forums ni ni sehemu ya kuvuna maarifa, kuburudika, na hata kutengeneza marafiki na uhusiano miongoni mwetu.
Ndugu zangu na wapendwa wote jamii forum, kuna baadhi ya mambo huenda yakawa yanachukuliwa katika hali ya utani lakini yakawa na madhara hasi pasi na mtu kulitambua hilo.
Embu Tazama mfano;
Kijana mmoja anasema, singo maza ndio wanaongoza kutoa mbususu hovyo, na pia singo maza ndio wanaongoza kujiuza kwenye madanguro?
Fikiria hii sentensi ameandika akitaka kuonyesha kwamba yupo sahihi lakini kinyume chake ni kuendelea kuvua wanaume nguo.
Kama singo maza chanzo chake kikubwa ni sisi WANAUME, mwanamke mtu kamzalisha wameshindwana labda kwa sababu mwanamke ajatulia sawa, je hayo majukumu ya mtoto wako unamuachia nani?
Huyu singo maza kila atakapoenda kutafuta kazi ataombwa rushwa ya ngono, mwanaume tayari kashakimbia na hakuna huduma yoyote anayoitoa kwa mtoto wake.
Unafikiri huyu mwanamke atafanya nini kuendelea kumpa huduma muhimu mtoto wake? Mwisho wa siku ataishia kutafuta njia za kujirahisisha ili tu aendelee kumtunza mtoto wake kwasababu tu ya mwanaume mpumbavu asiyejua kwamba kuwa mwanaume kuna ambatana na majukumu mazito.
Wanasema chizi hufurahisha anapokuwa si nduguyo, ila kama ni nduguyo hicho ni kilio. Tumuulize tu kama dada yake akamkuta katika madanguro sababu ya mwanaume ambaye alimtelekeza yeye atajisikiaje?
Kama kijana huyu sasahiv ngozi bado imenyooka, damu bado ya moto, ananyoa anapendeza akifikiri kwamba ujana utakuwepo tu basi ni kujidanganya.
Ipo siku mtoto wako wakike na yeye atakuwapo katika madanguro kwa sababu ya mwanaume mpumbavu kama wewe ambaye ulishindwa kutimiza majukumu yakiume.
Embu fikiria huu mfano;
KATAA NDOA, UMIZA MWANAMKE.
Huyu ni mtu ambaye anasema umiza mwanamke, ambaye kaja kwa kupitia kati kati ya mapaja ya mwanamke huyo!
sasa tumuulize kama amesema umiza mwanamke je mama yake aliyemzaa alishamuumiza? Hivi wanaume huwa mnajaribu kufikiri mnachoandika hapa?
Je huyu aliyesema umiza mwanamke yupo tayari kumuona mama yake akinyanyasika mbele yake na akampongeza huyo anayemnyanyasa?
Jamani ndugu zangu embu tujaribu kufikiri japo kwa uchache mambo tunayoongea, hii sehemu inafika watu wengi sana.
Tunaweza kuonekana wengi ni wapumbavu wasio na maana sababu tu ya wachache ambao wanahitaji watu wakuwaweka busy kwa kusoma maoni yao.
Kama unahitaji kuumiza mwanamke aidha kwa kihisia, hawa wanawake wasipokuwapo unafikiri tutaendelea vipi kuongezeka?
Hao watu wakufanya kazi ya kuliendeleza taifa watatoka wapi na tayari mtu anasema umiza mwanamke?
Naomba tu ndugu zangu tujaribu kufikiri tunachokiandika hata kama ID tunazotumia ni feki, embu tujitahidi tu.
Yaani kila siku wanaume tunaendelea kuvuliwa nguo sababu ya watu wachache , tunaendelea kuonekana si lolote sababu ya mambo haya!