Ralphryder
JF-Expert Member
- Nov 16, 2011
- 4,933
- 1,294
Hao mitume na manabii, wakiwapata wanawake wenye shida za aidha uzazi, migogoro ya ndoa, au magonjwa, wanawatoa ufahamu kabisa na kuwaaminisha kwamba wao ni bora kuliko imani walizokua nazo hao wamama, kama mama alikuwa aidha mkatoliki, au kkkt au Lutheran au muislam, anabadilika na anakosa heshima hata kwa mumewe na ndoa yake anaaminishwa haikua nzuri na anaanza kufundishwa ujinga ujinga wa imani mpya mpaka ndoa zinavunjika.
Mke anakuwa kiburi, hana tena imani na dini aliyozaliwa nayo na anakuwa kama msukule kwa hao mitume na manabii , yuko radhi atekeleze maelekezo ya wachungaji hao kuliko ya mume, watu wa ustawi wa jamii fanyieni uchunguzi jambo hili, ndoa nyingi sana zinavunjika kwa sababu ya watu hao.
Mke anakuwa kiburi, hana tena imani na dini aliyozaliwa nayo na anakuwa kama msukule kwa hao mitume na manabii , yuko radhi atekeleze maelekezo ya wachungaji hao kuliko ya mume, watu wa ustawi wa jamii fanyieni uchunguzi jambo hili, ndoa nyingi sana zinavunjika kwa sababu ya watu hao.