Baadhi ya wahindi na hizi biashara

Baadhi ya wahindi na hizi biashara

SABABU KUBWA NI KUOANA MTOTO WA MJOMBA BABA MKUBWA SHANGAZI UNAOA ILI UTAJIRI UBAKI NYUMBANI. HII INALETA KURITHI UZEZETA?
Zinaitwa incest marriages (first cousin's marriages) zipo common sana kwa wahindi na waaarabu na ndio sababu kuu ya mamatizo ya akili maana watu wa ukoo m'moja yaani mabinamu kuoana ina biological effect
 
Msitusakame hivyo jamani. Wengine wazazi wetu walizaliwa Tz nasi tukazaliwa hapa. Sisi sote ni ndugu, ni watanzania kama walivyo blacks USA hivyo tupendane.
 
Na walidhumiwa izo nyumba wkt wa utawala wa kwanza nyingi zisomeni juu utakuta majina yao na waliachwa wakae walipe kodi na ndio wako mpk leo
Hizo Nyumba zilijengwa kwenye aridhi ya Tanganyika, Wao walikuwa RAIA wa India...

Nadhani umepata Jibu
 
Na walidhumiwa izo nyumba wkt wa utawala wa kwanza nyingi zisomeni juu utakuta majina yao na waliachwa wakae walipe kodi na ndio wako mpk leo
Walidhulumiwa au waliridisha mali za wazawa ujue enzi za ukoloni kulikua na societal classes, 1st class ilikua Europeans, 2nd class walikua Indians & Arabs na 3rd class and the least in relevant walikua watanzania wenye nchi.

Kazi ya second class ilikua ni kutekeleza order kutoka first class hata hizo nyumba mnazosema zenu waliozijenga ni watanzania kwa mali na nguvu zao cha India zilikua ramani tu na usimamizi ila gharama zote ni rasilimali za watanzania.
 
Jamaa alifukuzwa kazi kisa kaanza kuingia ndani kabla ya muhindi, jamaa akakuta kimdoli akakisogeza muhindi kukuta kimdoli kimesogezwa wacha alie hadi kamasi zikamtoka,, jamaaa akaona eeh makubwa si akakishika tena kimdoli akirudishe alipokitoa, mhindi fasta katoa Bastola ntakuua, Juma ikabidi atoke nduki na kazi basi.
😀😀😀😀😀😀😀😀😀😀😀
 
Kama kuna rushwa nadhani rushwa inavyotembea sasa ivi haijawahi kutokea katika tawala zote zilizopita apa Tz.Wanaosema magu kaweza nimuongo make yeye anaruhusu.
 
Nchi ambazo hakuna rushwa au kiwango kidogo mno hakuna wahindi wanafanya biashara
 
Wakuu mbona mna hasira sana na hawa watanzania wenzetu!

Hawa ni ndugu zetu hawana pengine wanapo pajua kama kwao ila ni hii hii Tanzania ya East Africa. Hata wakiwa nje ya Tanzania kama watanzania wengine wakipata likizo huja nyumbani Tanzania kusalimia wazee, ndugu, jamaa na marafiki.

Pia wakiwa nje ya nyumbani Tanzania hujitambulisha kwa fahari kabisa kuwa ni East African Asian toka Tanzania. Kumbukeni kuna West Indies Asian kule Barbados n.k kuna wa kule Durban South Africa n.k

Indian sub continent "kwao" ni sehemu wasioijiua na pia hawa watanzania wenzetu wa asili ya kihindi huchukiwa sana na wale tunaowaona wanafanana naona toka India proper.

Ugumu wa maisha usitufanye tuwachukie ndugu zetu na kuwabagua, hawa ni wenzetu kabisa kama makabila mengine zaidi ya 120 Tanzania.

Kama imetokea kuwa wengi wapo mijini tena mjini kati hiyo ni kutokana na historia kama vile ukikuta waManyema wengi wanaishi mjini kati Dsm au watoto-wa-mjini familia zao zipo mjini siku nyingi na ndiyo "kwao".

Hii siyo kosa lao ni historia tu kama wadau wengine walivyoeleza kuhusu dola ya utawala wa kikoloni au serikali au biashara , elimu n.k ulivyosambaza watu ulimwenguni / nchini .
 
Msitusakame hivyo jamani. Wengine wazazi wetu walizaliwa Tz nasi tukazaliwa hapa. Sisi sote ni ndugu, ni watanzania kama walivyo blacks USA hivyo tupendane.
Usisikilize kelele hizi mkuu. Hakuna atakaefukuzwa Tanzania. Sisi wote ni watanzania na hapa ndio nyumbani.

Hawa wanaosema wahindi waondoke na kama ikitokea basi watasema wahaya ni waganda waondoke au wachaga ni wakenya waondoke, n.k.

Dhambi ya ubaguzi haiwezi kumuacha mtu salama (Nyerere). Kama kufukuzana kutatokea basi kutatokea sehemu nyingine lakini sio Tanzania.

Watu wakipatwa na ugumu wa maisha mara nyingi wanatafuta kisingizio au mchawi (mara wahindi, mara mafisadi wa CCM, mara ACACIA). Mkuu wewe endelea tu kuijenga nchi yako Tanzania.
 
Wakati wakoloni wa kiingereza wanaondoka walitakiwa waondoke na wahindi wao kwani ndo waliowaleta, kama alivyofanya Idi amini kule uganda. Badala yake wameendelea kubana fursa za wazawa kufanya biashara kubwa kuwawezesha kuwa business tycoons. Pia pamoja na kuishi muda mrefu nchini wameshindwa kuchanganyikana na wazawa kwa kuendekeza ubaguzi, wengine hawapendi hata kuongea kiswahili ili mradi waonekane wapo tofauti na wazawa. Something has to be done...
 
Mleta uzi acha kusema "Hawa ndugu zetu" wahindi sio ndugu zako/zetu.

Ubaguzi hauishi kwa kulalamika lalakika tu inabidi na sisi tuanze ubaguzi tukiwabagua na wao watatia akili. Unakuta mtu analalamika eti wahindi hawataki tuoe Binti zao, kwanini usioe mweusi mwenzako na kumthamini. Kama unaona mke wa kihindi ni Bora kuliko mweusi basi una haki ya kubaguliwa sababu hata wewe huoni thamani ya mweusi mwenzio. Mbona wao hawao weusi. Wamezaliwa hapa vizazi na vizazi ila hawajui hata kiswahili. Thamini chako utathaminiwa. Utumwa upo vichwani mwetu

Kwa miaka mingi wahindi walikua wameshika uchumi na bado wanaendelea kushika sababu mfumo ulikua unawasapoti, basically ndiyo walioachiwa nchi baada ya Uhuru kama skilled labor. Wengi wanapesa za kurithi toka kwa mababu zao, zamani Enzi za ujamaa wakati mtanzania kumiliki biashara ilikua haiwezakani wahindi ndiyo walikua supplier wakubwa wa bidhaa. Sasa mambo ni tofauti na wahanga wakubwa wa Magufuli ni wahindi sababu ujanja ujanja, rushwa umepungua, woga umeingia na dola imeimarika ikizingatiwa hakuna watu waoga wa dola kama hawa jamaa
 
Wahindi wana muda sana na familia , baba akifunga duka jioni anakaa na familia na kama mgeni amekuja wamaongelea biashara itaongelewa sebuleni watoto wakisiliza. Hii inawafanya watoto kujifunza mbinu za biashara bila kwenda shule,

Sisi baba akifunga duka anakwenda baa au kwa mchepuko. Kuna mali ambazo ni siri hata mke na watoto hawazifahamu baba akifa ghafla zinaweza kupotea.

Uchumi wa Uganda uliyumba sana baada ya kufukuza wahindi, waganda hawa kuwa na ujuzi wa kutosha wa kuendesha biashara zilizoachwa na wahindi.
 
Wahindi wako vizuri sana kwenye "Financial Literacy" na wengi wanasurvive sababu ya Generational Wealth a.k.a Old Money hivyo viduka wengi vipo kwa ajili ya kuwakeep busy tu lkn mpunga mrefu walitafuta Babu zao na umewekezwa kwenye Bonds na Biashara mbalimbali kubwa za Ukoo nk. Waswahili tuna mambo mengi sana ya kujifunza toka kwa hawa wenzetu, Chuki dhidi yao haitatusaidia na tunazidi kuwa Duni sababu ya Chuki na Roho Mbaya Miongoni mwetu. Binafsi nimewahi fanya kazi na wahindi na walikiwa wananilipa vizuri tu kutokana na kazi niliyokuwa nawafanyia. Usitegemee kuwa mvivu na goigoi alafu ufanye kazi na Muhindi na asikudharau. Waswahili tuna matatizo sana lkn hatutaki kujikubali tutaishia kujenda chuki zisizo na msingi.
Tubadilike!
 
Kama yupo anayewafahamu hawa ndugu zetu vizuri naye atiririke hapa.

Wahindi sio ndugu zako. Mnapenda sana kuita watu ndugu zenu wakati they despise you.

Wahindi walikua second class citizen enzi za ukoloni hivyo walihodhi mali, ardhi na mifumo baada ya uhuru so they had a head start kulinganisha na watanganyika.

Ni wakwepa kodi na watoa rushwa wakubwa.
 
Back
Top Bottom